Wizi wa Escrow: Albert Marwa ni nani?

Wizi wa Escrow: Albert Marwa ni nani?

plz yeriko tutaftie majina hayo ya stanbic

Sure Yeriko inabidi afanye kazi yake. Atusaidie majina. Mie ningekuwa nafanya kazi kule hata nungeiba japo kwa kuyapiga picha kama mdau mmija alifanya kule kwa Mkimbozi
 
Hii nchi watu wanapiga hela at the expenses of wananchi wa hali ya chini,ila maufisadi mengine ni kujitafutia laana tu.

Juzi ofisini alinijia mzee mmoja mstaafu wa jumuiya ya africa mashariki upande wa ttcl(alikuja kuniomba nauli),anasema hadi leo wanadai pensheni yao hawajalipwa.

Anasema serikali ilifanya uhuni wakalipwa pensheni kwa hesabu za mishahara ya zamani badala ya scale ya mshahara waliyostaafu nayo.

Wakapeleka kesi mahakamani,wakashinda,hivyo serikali ikaamriwa iwalipe.

Wakaambiwa watalipwa kwa awamu tatu(miaka mitatu) kuanzia last year.

Malipo ya mwaka jana wamelipwa mwaka huu robo tatu tu,hiyo robo iliyobaki hawajamaliziwa hadi leo.

Awamu ya pili ilikuwa walipwe mwezi uliopita,tena wameambiwa watapewa nusu tu(kumbuka ile robo ya mwaka jana bado hawajalipwa).

Juzi juzi hazina wamewaambia hakuna fedha za kuwalipa hadi liidhinishwe fungu lingine.

Pesa wanayodai haizidi bilioni 2!na hii ni halali yao kwa sababu ni jasho lao,wala haina mjadala.

Kilianzishwa kitengo kinaitwa "Simu 2000" ambacho kazi yake ilikuwa kuuza mali za ttcl ili kuwalipa wazee hawa.

Zikauzwa mali nyingi,sote tunajua,pale Ilala flats,hapa karibu na mawasiliano tower ,chuo kikuu,tena tunajua ambaye alichukua mali hizi nyingi ni mtu mmoja,na jamaa zake kutoka familia ya juu ya awamu iliyopita.

Walisema zimepatikana bilioni 15 kuwalipa hawa wazee,lakini watu wakachakachua mahesabu na kuwapunja wazee wa watu.

Wazee wakastuka,wametumia sheria kudai stahili zao,wameshinda.

Leo hii malipo wanalipwa nusu nusu,tena kwa kupigwa dana dana hivi.!

Wazee wa watu wamejichokea,hawana means za maisha,wanategemea hivyo vihela ambavyo hata wakivipata vitawasaidia kwa muda mfupi tu lakini bado wanavisotea hivi?!

Pesa za simu 2000 ziko wapi?
Kwa nini serikali iliua CHC wakati bado kuna issues hizi zilizokuwa zikienda vizuri chini ya kitengo hicho kuliko hazina?

Kuna mtu kapewa bilioni moja za escrow peke yake,tena zote kwa wakati mmoja,bila chenga,tena kama ziada tu,lakini wazee hawa wanadai 2 billioni iliyo jasho lao,wanasoteshwa kwa malipo nusu nusu yanayocheleweshwa hivi?

Wengine ni wagonjwa n.k
Mmewasumbua kudai haki mahakamani,wamesota miaka yote hadi mahakama imewatetea,halafu bado mnawasumbua hivi,MNATAKA WOTE WAFE,PESA ZAO MPELEKE WAPI?

Serikali acheni kutafuta laana,mmetuibia fedha escrow,bado na hawa wazee maskini wa Mungu mnawadhalilisha hivi?

Wana jf,hivi ukiwa kiongozi serikalini huwa roho ya kibinadamu inaondoka au?

Nauliza hivi manake kuna mambo nashindwa kuyaelewa jamani,dah!
 
Amezaa na salama Kikwete.
Yeye na jamaa mwingine aitwaye shaban gurumo ndiyo walichota za escrow za kumpeleka kwa mkuu wa kata.
Kucha zangu na meno miye.

Aliwahi muoa sophia mang'enya.mtoto wa waziri mang'enya .alimuumiza roho sister wangu mshenzi huyu.Na Albert Kama unasoma hapa lile Gari Enzi zile ukatoa kwa Bi (dev) na kumpa sada shaha mwanamke aliyezaa na KINJE.Dada angu huku akifua shule mshenzi opportunist wewe.NA usinipigie kwa sababu unanijui haswa mie nani .wewe na omar kimbau
 
Jamani mbona kama mnang'ang'aniza tu na familia ya rais iwemo kwenye hii scandal??? Waliomo si mliwasikia kina kilaini na wengine?

Kuhusu Albert marwa ni mtoto wa mkuu wa majeshi wa zamani Mzee Mwita Marwa,alimuona salama kikwete dadake riz wanaezaliwa kwa mama mmoja,mama yao alifariki siku nyingi,ili kumuoa salama na kwa taarifa tu Albert ni muislam siku nyingi alibadili dini kabla ya kumuoa salama,walijuana na salama akiwa tayari muislam tena swala tano tofauti na kina riz,
Wewe Albert ni mtoto alilelewa tu wala jenerali hakuwa babaake.The dude wanted to Marry my sissy.yaani alitangaza harusi na Sophia mang'enya kanisani na wakati hapo hapo anawachumba kibao .Sasa ndoa na Sophia mang'enya imeishia wapi Jesus .Sophia mtoto wa waziri mang'enya Yule mama .Dah duniani
 
attachment.php




Huyu SI MTANZANIA wa kulaziwa wala wa wazazi...lakini mtanzania PLASTIC wa kupewa.

inasemekana ni yatima hana baba wala mama ila aliokotwa huko Uganda na mmoja wa wakuu wa majeshi na kuletwa Tanzania

Nadhani alioa kama mara 3 hizi na mabinti aliooa ni watoto wa wakubwa ndio maana watu wanadai ameoa kwa ajili ya line

Shule aliyooenda haijuilikani

JKT haijulikani kama pia alikwenda

Ndio ofisi zake zilikuwa mtaa wa samora pale juu ya SAPNA na zamani nadhani India walikuwa wanatoa viza pale...just opposite SALAMANDA

connection yake ilikuwa ni kufanya biashara ya ulanguzi wa mafuta kwenda Rwanda, Congo na burundi miaka ya 90 na lile dula la duty free la jeshi (jina limentoka).

alikuwa anaingiza mafuta na kudai yanenda cross country tax free kumbe baadae wanayarudisha Dar kuuza kwa bei ya juu zaidi

Ofisi yake alikuwepo Ippy Malecela, Omari Kimbau, MAO Mwaura (sie tulikuwa tunamjua kama MAO Flex), Abdul Msomali (japo marehem alikuwa na pesa zaidi kwa madili yake ya unga kule Zambia na akina marehem AKASHA ) Chale Mtawali (enzi zile chale dada yake alikuwa mkurugenzi Immigration), Kinje na yule KIM KIMBANGAMBAGA (kiboko ya wanawake wa mjini kama kina Dr MWELE MALECELA, MANGE KIMAMBI etc), na watoto wengine wa wakubwa.

Salama sijui kamtoa wapi lakini kwa wanaomjua huyo dada unaambiwa hata haieleweki alimkubali vipi huyu jamaaa

Ndoa yake haikukubalika na Professa kwa sababu ya historia yake ya kuwalaghai watoto wengine wa wakubwa aliokuwa nao. Jamaa alikuwa kama MARIO fulani kwanza kama sikosei alioa GENERAL STWEWART MANGENYA ambaye ana uhusiano wa kifamilia na akina BOMANI (old money)...Kama sijakosea alikuwa anatoka na RITA MLAKI wa enzi hizo alipokuwa na saloon (VASANDRA) pale juu SAMORA.



Huyu inasemekana alisilimu ili kupata ukaribu zaidi na mama salma, na pia ndiye moja ya waanzilishi wa redio mmoja ya kiislam hapa Dar

Connections zake china ndio zinatisha zaidi kwa sababu anatajwa kuhusika kwenye kashfa za UPANUZI WA BANDARI, BOMBA LA GESI LA MTWARA ambazo amekula si chini ya dola milioni 300 peke yake na bila kusahau kashfa zingine kama hii ya escrow

Pamoja na yote haya huyu jamaa HAJAKUBALIKA kwenye familia na wala kwa watu walio karibu na familia....kwa kuongeza tuu ni kuwa yule Myemen ambaye simpendi wa homeshopping centre (SALAAH WA GUANGZJOU) anakubalika zaidi kwenye familia

Watu wa kitengo wa Usalama nao hawawezi kumfanya kitu kwa sababu ya hizo connections zake (lakini sina hakika kama huwa anarudi kwao UGANDA) au inawezekana ikawa familia yake ni ya KINYARWANDA , hilo hatulijui lakini ndio hivyo

Watu wake wa karibu wanasema kuwa huyu jamaa ni mtu poa lakini ARROGANT kwa sababu kazungukwa na wajinga wajinga wengi ambao wanamtia ujinga so in essence he's not that smart kwenye kuficha huo mkono wake kwenye madili


Pia wafanyakazi wa wizara ya fedha pia hawampeni kwa sababu safari za kuserikali huwa anaongozana nao kutokana na instructions toka JUU kuwa wakifika Beijing kupiga hayo madili na EXIM BANK lazima LABERT awepo japo shule na elimu yake ndogo.

Mawaziri nao wanamgopa sana kwa sababu ya connection yake na familia ya JK.

Miradi yake mingi ni hiyo ya kuunganisha unganisha ya real estate....na inaendana na hao washauri wake ambao nao pia ni watu wa kunganisha unganisha tuuu

rough estimate ni kuwa huyu Albert ana Net worth $500 million.

Philemeon Michael anamjua sana huyu jamaa.

Huyu jamaa mimi simchukii naomwona kama vile akina Juma Pinto, lakini huyu badala ya blah blah ameunganisha damu...hivyo ukinuliza simchukii bali naona ni mtu aliyepata nafasi na kaitumia vilivyo. Ningepata mimi ningekuwa ni BILIONEA na sio hivyo vijisenti na nisingeandikwa humu JF (hii ni another weakness ya kuwa na washauri wabovu wenye njaa, wasio na influence wala network)

Huyu jamaaa amekuwa kama mbuyu wenzake wanaendela na maisha ya hapa na pale huyu yeye anaongea na rais wa china, na kama u mario bas huyu kafuzu kwa sababu ukiangalia wenzake akina OMARI KIMBAU, IDDI JANGUO, JUMA PINTO, CHALE MUTAWALI, na wengineo yeye huyu aliamua kutumia ile formula ya FREEMAN MBOWE kuoa alipomwoa mtoto wa GAVANA EDWIN MTEI.

Dont hate the playa, hate the game


Nimeelewa why Ikulu ilibidi wakijibu kuhusu yule mwarabu wa home shopping center
 
Watu mnachimba!!
Kamwoa nani?

Kamuoa Salama. Alianza kama utani, kapiga mzigo hadi tumbo likajibu, binti kuulizwa akamtaja mshikaji, basi ndo akasogezewa mzigo. Sasa anapiga deal tu kupitia nyumba nyeupe.
Ova
 
Kamuoa Salama. Alianza kama utani, kapiga mzigo hadi tumbo likajibu, binti kuulizwa akamtaja mshikaji, basi ndo akasogezewa mzigo. Sasa anapiga deal tu kupitia nyumba nyeupe.
Ova
Hii habari mbona msemaji wao hapa JF, FaizaFoxy, hajajitokeza kukanusha? Au anajifanya hamjui Albert Marwa! Hivi huyu FaizaFoxy ni nani hasa...ni taasisi, mafia au ni jini? Kwa mbali nayakumbuka yale majini aliyotuonya marehemu Sheikh Yahya Hussein kwamba yatatoa ulinzi!
 
Last edited by a moderator:
Unaweza kufanya yako sawa, ila mambo yamezidi kuwa magumu. Leo nimeenda bank moja exchange rate ya usd leo ni 1805, unategemea nini? Inabidi tuwatoe hawa jamaa.

Duuu
Kweli fedha zinatakatishwaa
 
Wewe Albert ni mtoto alilelewa tu wala jenerali hakuwa babaake.The dude wanted to Marry my sissy.yaani alitangaza harusi na Sophia mang'enya kanisani na wakati hapo hapo anawachumba kibao .Sasa ndoa na Sophia mang'enya imeishia wapi Jesus .Sophia mtoto wa waziri mang'enya Yule mama .Dah duniani

Unamsema waziri Mang'enya au General Mang'enya au Chief Erasto Mang'enya?
 
Marwa kam walivyosema wengi ni mkwe kwa kikwete. Jamaa anatumiwa tu na mkuu kupita wIzarani kwa madili. Kiatu kimemwisha pale waizara ya nishati. Hii wizara imekuwa backyard ya kikwete na marwa ndio anatumika. Na huko hata mali asili yupo.

Sasa ugunfue teuzi za kikwete sio anakosea.anajua anachofanya. Hachagui watu wenye misimamo. Unafikiri kwanini magufuli hakuwekwa nishati?
Watendaji wengi sana wa kikwete wako pale kwa lengo la kutimiza kile kikwete anataka.

Unadhani maswi na marwa ni coincidence? Na yule prof jinga kuliko wote na mwongo.

Unadhani kwanini muhongo alikuwa anapigana na mengi kuhusu gesi? Mengi hajui vita anaypoigana pale. Kikwete yuko kwenye biashara za gesi pia. Naomba waje hapa watu wabishe.
 
HNIC kesho nakupa reputation kubwa kabisa. Kifaa natumia kwa sasa sipati features zote. You nailed it. Usalama wa Taifa hili.mpooooooo?
Wawepo wapi? Siku hizi wote ni watoto wakishua wako states wanakula bata. Usalama umebakia mikononi mwetu na Mungu wetu.
 
Kaka huyo sio mtoto wa Mzee Marwa ili kalelewa na mzee Marwa,huyu jamaa hapo nyuma alikuwa mwanzilishi wa radio ya kiisalamu,kwa Marwa hakuna Mwislamu,kama mna bisha kuna mtoto wake mzee Marwa alikuwa anafanya kazi CRDB sijui kama baado yupo na watoto wa Mzee Marwa wote wananfanana na hakuna mweusi tii kama huyo mkwe
Huyu alikuwa Mkristo akibadili dini Ndio analamba Hiyo deal ya kupikea pesa Za kuanzisha radio ...toka amebadili dini haizidi miaka 10
 
Namshukuru sana mwenyezi Mungu kwa kuendelea kuwafungulia Watz kujua jinsi gani wanaibiwa na kunyanyaswa na viongozi wao waliowapa dhamana.
Ni jukumu la Watz kufanya maamuzi sahihi sasa ktk chaguzi za serikali za mtaa zonazoendelea na mwakani kwenye uchaguzi mkuu
 
Huo mtaa noma.

Unaweza kukaa hivi mara unamuona Lowassa anafuatilia hela zake mwenyewe kwa wahindi.

Au Benzi la Ikulu linamshusha Kiaro maskani.

Au mara tu Mengi katoka baru karuka ukuta Silver Oak kamkimbia mke wake akiwa nyumba ndogo.

Mara Makame Rashid kafuata za kununua kwa mafungu Las Vegas.

Mara kidogo Andrew "Ganesh" katokea kaja kutafsiri vitabu vya ki Buda kwenda kiswahili.

Mara Spartan karudi poa anaoga bia.

Imekuwaje tena? Nimerudi nimekuta viberiti vimepanda juu utasema Lower East Side.

Duu Ernest Mwita Kiaro ...mwanaye mmoja alikuwa Tambaza kwenye ile fujo kubwa ya Marehemu Puza ..Kina muro ...Vagi na Tambaza ....Sasa mwanaye naye aliongoza vurugu wakawa wanaogopa kumfukuzaa ....kwenda pale ...akasema " Kama chimefanya funnjo Chiende ...Chidief ( CDF ) ni Mimi sio yeye "
 
Hii habari mbona msemaji wao hapa JF, FaizaFoxy, hajajitokeza kukanusha? Au anajifanya hamjui Albert Marwa! Hivi huyu FaizaFoxy ni nani hasa...ni taasisi, mafia au ni jini? Kwa mbali nayakumbuka yale majini aliyotuonya marehemu Sheikh Yahya Hussein kwamba yatatoa ulinzi!

habari hizi atazijua wapi huyo ..ff..
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom