Wizara ya Katiba na Sheria Special thread: Tupe maoni, maswali, malalamiko na ushauri

1.) Ni kwanini Serikali ya Tanzania inapinga kwa nguvu zote uwepo wa Uraia Pacha huku Nchi nyingine zikinufaika kupitia Uraia Pacha huo huo katika nyanja mbalimbali mfano. Uwekezaji, biashara, michezo, nk?....
Ndugu Tate Mkuu,

Tunaomba tujibu maswali yako kama ifuatavyo:

1. Masuala ya uraia wa Tanzania yanasimamiwa na Sheria ya Uraia Namba 6 ya mwaka 1995 ambayo imebainisha kuwa uraia wa Tanzania upo katika makundi matatu; uraia wa kuzaliwa, uraia wa kurithi na uraia wa tajinisi. Aidha, sheria hii kupitia kifungu cha 7(4)(a)(b) kimeeleza bayana kuwa raia wa Tanzania anaacha kuwa raia kwa kigezo cha kuchukua uraia wa nchi nyingine. Hivyo basi, kutokana na sheria hii na sera ya Tanzania kuhusu uraia ambayo hairuhusu wala kutambua uraia wa nchi mbili, Serikali haiwezi kuweka sheria ya uraia pacha kwa sasa.

Suala hili lilijadiliwa pia wakati wa mchakato wa upatikanaji wa Katiba Mpya ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Bunge Maalum la Katiba ambalo lilijadili pendekezo hili liliona Tanzania bado haipo tayari kwa sasa na Bunge hilo Maalum likatoa pendekezo kwamba; “Mtu yeyote mwenye asili au nasaba ya Tanzania na ambaye ameacha kuwa raia wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kupata uraia wa nchi nyingine atakapokuwa katika Jamhuri ya Muungano atakuwa na hadhi maalum kama itakavyoainishwa katika sheria za nchi.”

Nukuu hii imebainishwa katika Sura ya 6, Ibara ya 72 ya Katiba Inayopendekezwa ya Oktoba, 2014.

2. Suala la Mgombea Binafsi halipo kwa mujibu wa katiba na sheria zetu. Hoja hii lilipendekezwa kwenye mjadala wa katiba mpya ambayo bado haijakamilika. Hivyo hatuwezi kusema ni lini serikali itaruhusu, labda mpaka pale tutakapokuwa na sheria hiyo.

3. Katiba Mpya ni ajenda ya kitaifa. Ni dhahiri taifa letu linahitaji katiba mpya itakayoakisi mahitaji yetu ya sasa na baadae.

Kwa kulitambua hilo, kama itakumbukwa, mchakato wa Katiba Mpya ulifikia pazuri ambapo serikali kwa nia njema iliitisha bunge maalum la katiba likihusisha wadau wanaowakilisha makundi mbalimbali.

Kwa bahati mbaya, baadhi ya makundi muhimu yanayowakilisha wananchi yaligoma kuendelea kuhudhuria bunge hilo wakati mchakato wa kupatikana katiba mpya ukiendelea, hivyo kukwamisha zoezi zima na serikali kulazimika kusitisha.

Vipaumbele vya Serikali kwa sasa, kama ilivyotangazwa na Mheshimiwa Rais John Pombe Magufuli mara kadhaa, ni kushughulikia kero zinazogusa wananchi moja kwa moja na kuboresha utoaji huduma bora ikiwemo kuweka miradi ya kimkakati itakayokuza uchumi wa taifa letu.

Ajenda ya Katiba Mpya itafikiwa tena pale itakapofika wakati wake kwani Katiba ni hitaji la nyakati.

4. Wizara hairidhishwi na uvunjifu wowote wa sheria unaofanywa na askari au mtumishi yeyote kwani sheria ziko wazi. Makosa ya jinai yote yanashughulikiwa na mahakama zetu kwa mujibu wa sheria bila kuangalia mtendaji ni nani.

Asante.
 
Kuna masuala matatu ninayoomba wizara iweze kuyafanyia kazi: 1. Law School. Vyuo vikuu vingi kwa sasa vina programmes ambazo zinawa'accomodate' wanafunzi wanaosoma asubuhi hadi mchana na pia masomo ya jioni. Ukichukulia kwamba kuna wanafanyakazi wanaosoma sheria na wangetaka kusoma law school, lakini kwa sababu ya utaratibu wa kazi, hawawezi kusoma law school. Je, haiwezekani kuwa na masomo ya jioni kama ilivyo kwa UDSM?...
Asante kwa maoni mazuri.

Ni kawaida ya wizara kusikiliza ushauri na maoni ya wananchi kisha kuyachambua na kuyafanyia kazi.

Haya tumeyapokea na tutayafikisha kwenye idara zinazohusika.
 
Ni uamuzi wa busara kwa Wizara hii kufungua ukurasa wake na JF karibuni sana,swali langu sheria inasemaje kwa mtuhumiwa kuwa mtu huru hadi pale atakapokutwa na hatia na mahakama?na why mashitaka ya uhujumu uchumi,murder,hayana dhamana?tunayoyona hapa ni haki ya suspect(s) kutozingatiwa.
 
Wizara Katiba Na Sheria mimi nina mengi sana kuhusu sheria zetu nyingi. Lakini naomba nilifikishe kwenu hili kama maoni, juu ya sheria mbalimbali haswa zinazohusu matumizi ya Teknolojia. Sote tunakubaliana kuwa matumizi ya mitandao yanakuja na matumizi mabaya, lakini sheria zetu nyingi ni blanket kwa maana zinawakumba wote bila kuwa na speciation. Nitatoa mfano mmoja japo ipo mingi....
Asante kwa maoni mazuri Ndugu Stefano Mtangoo.

Kwa bahati nzuri, wadau mbalimbali wameshawasilisha kwetu maoni ya aina hii pia, hivyo yatapitiwa kwa pamoja na kuangaliwa kwa jicho chanya.

Asante.
 
Ndugu Tate Mkuu,

Tunaomba tujibu maswali yako kama ifuatavyo:

1. Masuala ya uraia wa Tanzania yanasimamiwa na Sheria ya Uraia Namba 6 ya mwaka 1995 ambayo imebainisha kuwa uraia wa Tanzania upo katika makundi matatu; uraia wa kuzaliwa, uraia wa kurithi na uraia wa tajinisi...
Ukijibu swali No.3 umesema, nakunukuu; "ni dhahiri taifa letu linahtaji Katiba mpya kwa sasa", lakini ili ukwepe unasema " katiba ni hitaji la Wakati, ukifika italetwa Katiba mpya".

Unataka tuelewe nini sisi tunaohtaji kujua lini mchakato wa katiba mpya utarejeshwa mbali ya baadhi ya washiriki kususia mchakato? Na mbona mlipobaki CCM peke yenu mliendelea hadi hatua ya katiba inayopendekezwa, halafu Leo unasingizia serikali ilisitisha baada ya baadhi ya wadau kujitoa?
 
Asante kwa maoni mazuri Ndugu Stefano Mtangoo.

Kwa bahati nzuri, wadau mbalimbali wameshawasilisha kwetu maoni ya aina hii pia, hivyo yatapitiwa kwa pamoja na kuangaliwa kwa jicho chanya.

Asante.
Tunasubiria matokeo chanya. Maoni mengine nitayaleta kadri muda utakavyoniruhusu. Hasa kuhusu sera za biashara. Ambazo naamini mkishirikiana na Wizaraza Tamisemi, Fedha na Viwanda/Biashara tutakuwa na nchi bora zaidi kwa uwekezaji
 
Ni uamuzi wa busara kwa Wizara hii kufungua ukurasa wake na JF karibuni sana,swali langu sheria inasemaje kwa mtuhumiwa kuwa mtu huru hadi pale atakapokutwa na hatia na mahakama?na why mashitaka ya uhujumu uchumi,murder,hayana dhamana?tunayoyona hapa ni haki ya suspect(s) kutozingatiwa.
 
Ndugu Tate Mkuu,

Tunaomba tujibu maswali yako kama ifuatavyo:

1. Masuala ya uraia wa Tanzania yanasimamiwa na Sheria ya Uraia Namba 6 ya mwaka 1995 ambayo imebainisha kuwa uraia wa Tanzania upo katika makundi matatu; uraia wa kuzaliwa, uraia wa kurithi na uraia wa tajinisi. Aidha, sheria hii kupitia kifungu cha 7(4)(a)(b) kimeeleza bayana kuwa raia wa Tanzania anaacha kuwa raia kwa kigezo cha kuchukua uraia wa nchi nyingine. Hivyo basi, kutokana na sheria hii na sera ya Tanzania kuhusu uraia ambayo hairuhusu wala kutambua uraia wa nchi mbili, Serikali haiwezi kuweka sheria ya uraia pacha kwa sasa.

Suala hili lilijadiliwa pia wakati wa mchakato wa upatikanaji wa Katiba Mpya ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Bunge Maalum la Katiba ambalo lilijadili pendekezo hili liliona Tanzania bado haipo tayari kwa sasa na Bunge hilo Maalum likatoa pendekezo kwamba; “Mtu yeyote mwenye asili au nasaba ya Tanzania na ambaye ameacha kuwa raia wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kupata uraia wa nchi nyingine atakapokuwa katika Jamhuri ya Muungano atakuwa na hadhi maalum kama itakavyoainishwa katika sheria za nchi.”

Nukuu hii imebainishwa katika Sura ya 6, Ibara ya 72 ya Katiba Inayopendekezwa ya Oktoba, 2014.

2. Suala la Mgombea Binafsi halipo kwa mujibu wa katiba na sheria zetu. Hoja hii lilipendekezwa kwenye mjadala wa katiba mpya ambayo bado haijakamilika. Hivyo hatuwezi kusema ni lini serikali itaruhusu, labda mpaka pale tutakapokuwa na sheria hiyo.

3. Katiba Mpya ni ajenda ya kitaifa. Ni dhahiri taifa letu linahitaji katiba mpya itakayoakisi mahitaji yetu ya sasa na baadae.

Kwa kulitambua hilo, kama itakumbukwa, mchakato wa Katiba Mpya ulifikia pazuri ambapo serikali kwa nia njema iliitisha bunge maalum la katiba likihusisha wadau wanaowakilisha makundi mbalimbali.

Kwa bahati mbaya, baadhi ya makundi muhimu yanayowakilisha wananchi yaligoma kuendelea kuhudhuria bunge hilo wakati mchakato wa kupatikana katiba mpya ukiendelea, hivyo kukwamisha zoezi zima na serikali kulazimika kusitisha.

Vipaumbele vya Serikali kwa sasa, kama ilivyotangazwa na Mheshimiwa Rais John Pombe Magufuli mara kadhaa, ni kushughulikia kero zinazogusa wananchi moja kwa moja na kuboresha utoaji huduma bora ikiwemo kuweka miradi ya kimkakati itakayokuza uchumi wa taifa letu.

Ajenda ya Katiba Mpya itafikiwa tena pale itakapofika wakati wake kwani Katiba ni hitaji la nyakati.

4. Wizara hairidhishwi na uvunjifu wowote wa sheria unaofanywa na askari au mtumishi yeyote kwani sheria ziko wazi. Makosa ya jinai yote yanashughulikiwa na mahakama zetu kwa mujibu wa sheria bila kuangalia mtendaji ni nani.

Asante.
Kero zipi sasaaa, ikiwa swala la dhamana kwa mtuhumiwa lime washinda kutatua.au watu kukaa miongo kadhaa gerezani kwa zile hekaya za upelelezi kutokamilika.

Hivi wizara mnaona ni fahari kwenu mtu kukaa ndani miaka kumi kusubiri upelelezi ukamilike?.au nalo hili sio kipaumbele cha mtukufu magufuli.
 
Hongereni kwa kutufuata huku, naomba kuuliza kama mna mpango wa kupendekeza sheria inayolinda taarifa binafsi (faragha) za kila raia yaani "Personal Information Protection Act" ?
Asante sana Cannabis.

Ibara ya 16 ya Katiba ya JMT inalinda haki ya faragha na usalama wa mtu yakiwemo mawasiliano yake. Hivyo, tayari haki ya mtu inalindwa na sheria mama ambayo ni katiba.

Kuhusu swali lako, tuseme tu kwa ufupi wizara tayari inayo mapendekezo kadhaa juu ya sheria mbalimbali. Muda ukifika tutatoa taarifa rasmi.

Asante.
 
Swali zuri.

Sheria hii ilizingatia kwamba aliye na taaluma anayo nafasi kubwa ya kuajiriwa tena kutokana na taaluma yake, hivyo bado akawa anaendelea kujazia akiba yake hadi atakapostaafu, tofauti na asiye na taaluma.

Hizi asilimia 33 ni za kumpa unafuu wa kujikimu wakati akifuatilia kazi nyingine.

Asante.
Kwaiyo mnataka uyu Alie ajiriwa azidi kuajiriwa Miaka yake yote?

Hamuoni mnakua hamumtendei haki Kama anahitaji kujiajili kupitia iyo hela yake?

Mfano:
Mimi ni engineer wa umeme, niamua kuacha kazi ili nikaanzishe duka la vifaa vya umeme.
Huoni mnakua hamjanitendea haki kuninyima pesa yangu?
 
Kwaiyo mnataka uyu Alie ajiliwa azidi kuajiliwa Miaka yake yote?

Hamuoni mnakua hammtendei haki Kama anahitaji kujiajili kupitia iyo Ela yake?...
DeepPond,

Sheria Ya Mifuko Ya Hifadhi Ya Jamii ina malengo mengi, lakini la msingi zaidi ni kuwasaidia watumishi/wafanyakazi mmoja mmoja kuhakikisha wanaweka akiba kwa ajili ya maisha yao ya uzeeni. (Kifungu cha 7 cha sheria husika).

Akiba ya uzeeni, yaani maisha baada ya kustaafu, na si vinginevyo.

Asante.
 
Ndugu Tate Mkuu,

Tunaomba tujibu maswali yako kama ifuatavyo:

1. Masuala ya uraia wa Tanzania yanasimamiwa na Sheria ya Uraia Namba 6 ya mwaka 1995 ambayo imebainisha kuwa uraia wa Tanzania upo katika makundi matatu; uraia wa kuzaliwa, uraia wa kurithi na uraia wa tajinisi. Aidha, sheria hii kupitia kifungu cha 7(4)(a)(b) kimeeleza bayana kuwa raia wa Tanzania anaacha kuwa raia kwa kigezo cha kuchukua uraia wa nchi nyingine. Hivyo basi, kutokana na sheria hii na sera ya Tanzania kuhusu uraia ambayo hairuhusu wala kutambua uraia wa nchi mbili, Serikali haiwezi kuweka sheria ya uraia pacha kwa sasa.

Suala hili lilijadiliwa pia wakati wa mchakato wa upatikanaji wa Katiba Mpya ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Bunge Maalum la Katiba ambalo lilijadili pendekezo hili liliona Tanzania bado haipo tayari kwa sasa na Bunge hilo Maalum likatoa pendekezo kwamba; “Mtu yeyote mwenye asili au nasaba ya Tanzania na ambaye ameacha kuwa raia wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kupata uraia wa nchi nyingine atakapokuwa katika Jamhuri ya Muungano atakuwa na hadhi maalum kama itakavyoainishwa katika sheria za nchi.”

Nukuu hii imebainishwa katika Sura ya 6, Ibara ya 72 ya Katiba Inayopendekezwa ya Oktoba, 2014.

2. Suala la Mgombea Binafsi halipo kwa mujibu wa katiba na sheria zetu. Hoja hii lilipendekezwa kwenye mjadala wa katiba mpya ambayo bado haijakamilika. Hivyo hatuwezi kusema ni lini serikali itaruhusu, labda mpaka pale tutakapokuwa na sheria hiyo.

3. Katiba Mpya ni ajenda ya kitaifa. Ni dhahiri taifa letu linahitaji katiba mpya itakayoakisi mahitaji yetu ya sasa na baadae.

Kwa kulitambua hilo, kama itakumbukwa, mchakato wa Katiba Mpya ulifikia pazuri ambapo serikali kwa nia njema iliitisha bunge maalum la katiba likihusisha wadau wanaowakilisha makundi mbalimbali.

Kwa bahati mbaya, baadhi ya makundi muhimu yanayowakilisha wananchi yaligoma kuendelea kuhudhuria bunge hilo wakati mchakato wa kupatikana katiba mpya ukiendelea, hivyo kukwamisha zoezi zima na serikali kulazimika kusitisha.

Vipaumbele vya Serikali kwa sasa, kama ilivyotangazwa na Mheshimiwa Rais John Pombe Magufuli mara kadhaa, ni kushughulikia kero zinazogusa wananchi moja kwa moja na kuboresha utoaji huduma bora ikiwemo kuweka miradi ya kimkakati itakayokuza uchumi wa taifa letu.

Ajenda ya Katiba Mpya itafikiwa tena pale itakapofika wakati wake kwani Katiba ni hitaji la nyakati.

4. Wizara hairidhishwi na uvunjifu wowote wa sheria unaofanywa na askari au mtumishi yeyote kwani sheria ziko wazi. Makosa ya jinai yote yanashughulikiwa na mahakama zetu kwa mujibu wa sheria bila kuangalia mtendaji ni nani.

Asante.
Nawashukuru kwa majibu yenu. Kwa mtazamo wangu, karibia maswali yote yamejibiwa kwa tahadhari na umakini mkubwa. Hilo sina shaka nalo. Nyinyi ni Serikali na pia mnatekeleza ilani ya CCM pasipo na shaka yoyote ile.
Safari hii nimekuja tu kwa ajili ya kutoa ushauri kwa manufaa ya Taifa letu.

Mkiwa kama Serikali iliyopewa dhamana ya kuwaongoza/kuwatawala Watanzania zaidi ya milioni 50, mnatakiwa KUBADILIKA! Punguzeni au ikiwezekana acheni kabisa kitu kinachoitwa UHAFIDHINA!

Mimi ni mmoja kati ya watanzania wengi walioshiriki kwenye zoezi la mchakato wa Katiba Mpya kuanzia mwanzo mpaka mwisho. Nilibahatika kulifuatilia Bunge la Katiba kupitia luninga, na pia sarakasi zilizokuja kujitokeza kati ya pande mbili; CCM vs UKAWA kuhusu aina ya Serikali za kuiunda Tanzania Mpya!

Hakuna shaka yoyote ile kusema, mchakato ule ulivurugwa na Wanasiasa! Na mpaka leo sijapata jibu ni kwa nini Rais wa wakati ule aliamua kujaza Wanasiasa wengi (huku akitambua fika WANASIASA WOTE ni WABINAFSI na wengi wao wapo kwa ajili ya maslahi yao na ya vyama vyao) kuliko wataalamu wa makundi mbalimbali, huku hao wanasiasa wakibakia kuwa wachache.

Turudi kwenye mjadala:

1.) Naomba mfanyie kazi niliyo waeleza. Mkiwa kama Wizara, mna uwezo wa kumshauri Mh. Rais kuhusu umuhimu wa Katiba Mpya. Mwambieni Watanzania tulio wengi tunahitaji Katiba Mpya. Ikiendelea kutumika hii Katiba ya Chama Kimoja ya 1977, inaweza kuja kusababisha machafuko siku za usoni. Na hilo siliombei. Kisingizio cha kufanya maendeleo, hakina mashiko sana! Maendeleo bila Katiba Bora/mfumo imara wa kiutawala na mgawanyo mzuri wa madaraka, ni kazi bure!

By the way, hii ni awamu yake ya mwisho kutawala! hivyo hana cha kupoteza iwapo atatuachia Watanzania zawadi bora kabisa ya Katiba Mpya kama alivyojaribu Mtangulizi wake na mwisho kuishia kushindwa hatua za mwisho! Hayo madaraja mnayojenga, ndege mnazo nunua, flyovers, treni ya umeme, vitaishia tu kubomolewa na kuharibiwa vibaya! iwapo tu vitatokea vita vya wenyewe kwa wenyewe kwa sababu tu ya uwepo wa Katiba isiyo kidhi mahitaji ya wengi. Tujifunze kutoka LIBYA!

2.) Suala la Uraia Pacha, naomba nalo mlitafakari kwa kina. Mnaweza mkawapa haki zote hao Diaspora katika nyanja za uchumi na masuala ya kijamii na kuwabana sana kwenye masuala ya kisiasa kama mnaogopa hao kama watakuja kuwanyang'anya vyeo vyenu. Leo hii wenzetu wa Algeria, Morocco, Afrika Magharibi, nk. Wananufaika na Uraia Pacha kupitia michezo, uwekezaji, nk. Sisi tumekaza tu shingo huku tukiwa hatuna hata sababu zenye mashiko za kuzuia huo Uraia Pacha.

3.) Kuhusu suala la Mgombea Binafsi, Matokeo ya Rais kupingwa Mahakamani, nk. Ni vitu ambavyo havizuiliki kwa sasa! Haya mambo ya kumlazimisha mtu kudhaminiwa na Chama cha Kisiasa kugombea nafasi ya Uongozi, kunadumaza Demokrasia na pia kunaongeza kiwango cha UNAFIKI na kujipendekeza nchini.

4.) Kuhusu ishu ya baadhi ya watu mfano POLISI kuwa juu ya sheria, nalo mlitazame kwa kina. Kwa sasa POLISI wetu wamejigeuza kuwa MAHAKAMA! (Kwenye kuua watuhumiwa wanao dhaniwa kuwa ni majambazi, kupokea rushwa na pia kwenye utozaji wa faini ya makisa ya barabarani) Jambo hili halikubaliki! Maana hao polisi ni binadamu! Kuna ushahidi mwingi tu wa kukengeuka kwao. Na mfano mdogo tu ni huo wa Wafanyabiashara wa madini kutoka Mahenge.

Naomba kuwasilisha.
 
Ndugu Tate Mkuu,

Tunaomba tujibu maswali yako kama ifuatavyo:

1. Masuala ya uraia wa Tanzania yanasimamiwa na Sheria ya Uraia Namba 6 ya mwaka 1995 ambayo imebainisha kuwa uraia wa Tanzania upo katika makundi matatu; uraia wa kuzaliwa, uraia wa kurithi na uraia wa tajinisi. Aidha, sheria hii kupitia kifungu cha 7(4)(a)(b) kimeeleza bayana kuwa raia wa Tanzania anaacha kuwa raia kwa kigezo cha kuchukua uraia wa nchi nyingine. Hivyo basi, kutokana na sheria hii na sera ya Tanzania kuhusu uraia ambayo hairuhusu wala kutambua uraia wa nchi mbili, Serikali haiwezi kuweka sheria ya uraia pacha kwa sasa.

Suala hili lilijadiliwa pia wakati wa mchakato wa upatikanaji wa Katiba Mpya ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Bunge Maalum la Katiba ambalo lilijadili pendekezo hili liliona Tanzania bado haipo tayari kwa sasa na Bunge hilo Maalum likatoa pendekezo kwamba; “Mtu yeyote mwenye asili au nasaba ya Tanzania na ambaye ameacha kuwa raia wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kupata uraia wa nchi nyingine atakapokuwa katika Jamhuri ya Muungano atakuwa na hadhi maalum kama itakavyoainishwa katika sheria za nchi.”

Nukuu hii imebainishwa katika Sura ya 6, Ibara ya 72 ya Katiba Inayopendekezwa ya Oktoba, 2014.

2. Suala la Mgombea Binafsi halipo kwa mujibu wa katiba na sheria zetu. Hoja hii lilipendekezwa kwenye mjadala wa katiba mpya ambayo bado haijakamilika. Hivyo hatuwezi kusema ni lini serikali itaruhusu, labda mpaka pale tutakapokuwa na sheria hiyo.

3. Katiba Mpya ni ajenda ya kitaifa. Ni dhahiri taifa letu linahitaji katiba mpya itakayoakisi mahitaji yetu ya sasa na baadae.

Kwa kulitambua hilo, kama itakumbukwa, mchakato wa Katiba Mpya ulifikia pazuri ambapo serikali kwa nia njema iliitisha bunge maalum la katiba likihusisha wadau wanaowakilisha makundi mbalimbali.

Kwa bahati mbaya, baadhi ya makundi muhimu yanayowakilisha wananchi yaligoma kuendelea kuhudhuria bunge hilo wakati mchakato wa kupatikana katiba mpya ukiendelea, hivyo kukwamisha zoezi zima na serikali kulazimika kusitisha.

Vipaumbele vya Serikali kwa sasa, kama ilivyotangazwa na Mheshimiwa Rais John Pombe Magufuli mara kadhaa, ni kushughulikia kero zinazogusa wananchi moja kwa moja na kuboresha utoaji huduma bora ikiwemo kuweka miradi ya kimkakati itakayokuza uchumi wa taifa letu.

Ajenda ya Katiba Mpya itafikiwa tena pale itakapofika wakati wake kwani Katiba ni hitaji la nyakati.

4. Wizara hairidhishwi na uvunjifu wowote wa sheria unaofanywa na askari au mtumishi yeyote kwani sheria ziko wazi. Makosa ya jinai yote yanashughulikiwa na mahakama zetu kwa mujibu wa sheria bila kuangalia mtendaji ni nani.

Asante.
Umejitahidi sana kufafanua kwa uzuri,
Jibu namba 3 unasema kipaumbele cha serikali sasa ni kushughulikia kero zinazogusa wananchi moja kwa moja.

Swali langu ni kwamba, kwani ishu ya katiba Mpya sio kero ya wananchi? Unyanyasaji na uvunjifu wa haki unaoendelea hauwagusi wananchi moja kwa moja? Ninanachoona viongozi wa sasa hamuwezi kumshauri Rais afanye nini mpaka yeye mwenyewe atakapoamua.

Kama Wizara Katiba Na Sheria, hili ni jukumu lenu kuhakikisha mnamshauri Rais kuhusu katiba Mpya. Hii iliyopo imepitwa na wakati vitu vya 77 ni tofauti sana na sasa hivi.
 

Ndugu wana JamiiForums,

Tunashukuru kwa maoni yenu na mijadala inayoendelea hapa kila siku kuhusu masuala ya Katiba na Sheria za nchi yetu. Aidha kuhusu haki za binadamu, rushwa, utawala wa sheria na mengineyo.

Kupitia thread hii maalum; tutapokea maoni, ushauri na hata malalamiko yenu. Tunawahakikishia kuwa tutachukua hatua stahiki kwa haraka zaidi.

Unaweza kututumia pia Private Message (PM) na utajibiwa kwa haraka sana.

Fuatilia ukurasa rasmi wa Wizara ya Katiba na Sheria hapa JamiiForums kupata taarifa mbalimbali kuhusu utoaji wa huduma za Katiba na Sheria nchini Tanzania.

Tufuatilie pia kwenye mitandao yetu ya:

Instagram: @katibasheria_
Twitter: @sheria_katiba
Facebook: Wizara ya Katiba na Sheria

ANUANI ZETU NI:
Wizara ya Katiba na Sheria
Mji wa Serikali, Mtumba
S.L.P. 315,
Dodoma.

Masijala: barua@sheria.go.tz
Simu: +255 26 2310021
Nukushi: 255 26 2321679
Barua pepe: km@sheria.go.tz
Tovuti: www.sheria.go.tz
Naomba ufafanuzi kuhusu kauli ya Afisa Elimu Mkoa wa Kilimanjaro, Paulina Mkwama, ambae amesikika akisema kuwa wanafunzi watakaopata daraja la nne na sifuri (Division 4 & 0) katika shule ya sekondari ya Wavulana ya Umbwe iliyopo wilaya ya Moshi wajiandae kushtakiwa kwa kosa la uhujumu uchumi.
(Angalia video kwenye link hii, akiyasema hayo https://t.co/iEA6roeyzw)
Je, kama wizara yenye dhamana ya kusimamia sheria nchini mnasemaje juu ya hili? Kupata four na zero ni punishable offence in Tanzania as economic sabotage? Kama jibu ni hapana kama ambavyo uelewa wangu finyu unaniambia, je wizara ina mpango gani kuchukua hatua stahiki za kinidhamu/kisheria/kiutawala kwa kiongozi huyu na wengine ambao wamekua wakitoa matamko mbalimbali ambayo yanaleta taharuki na pia kupotosha sheria mbalimbali za nchi yetu?
Wizara Katiba Na Sheria
 
Nashukuru sana kukutana na thread hii hapa JF.. nilikuwa najipanga kumtafuta Waziri husika kwa kero mojawapo.

MAHAKAMA YA KAZI.
Migogoro ya kazi haishughulikiwa kwa muda unaokubalika kimantiki.
Chukulia mimi nimeachishwa kazi na Mwajiri, naenda Mahakama ya kazi kupitia CMA lakini inachukua mwaka miaka miwili bila shauri kukamilika!??
Waajiri wamekuwa wakitumia misuli yao kifedha kupiga danadana mashauri ya kazi ili kuwalazimisha walalamikaji kukata tamaa na mahakama iko compromised.
Katika hali ya kawaida mtumishi aliyekuwa anaishi kwa kukopa ili akutane na mshahara ujao hawezi kustahmili shauri kwenda miaka miwili bila kwisha wengi tunalazimika kuachana nayo hata kama tunajua tumeonewa na tutashinda.
Naomba muongozo nashughulikiaje shauri langu nililolitelekeza baada kwenda miaka 2 bila kumalizwa
 
Naomba ufafanuzi kuhusu kauli ya Afisa Elimu Mkoa wa Kilimanjaro, Paulina Mkwama, ambae amesikika akisema kuwa wanafunzi watakaopata daraja la nne na sifuri (Division 4 & 0) katika shule ya sekondari ya Wavulana ya Umbwe iliyopo wilaya ya Moshi wajiandae kushtakiwa kwa kosa la uhujumu uchumi.
(Angalia video kwenye link hii, akiyasema hayo https://t.co/iEA6roeyzw)
Je, kama wizara yenye dhamana ya kusimamia sheria nchini mnasemaje juu ya hili? Kupata four na zero ni punishable offence in Tanzania as economic sabotage? Kama jibu ni hapana kama ambavyo uelewa wangu finyu unaniambia, je wizara ina mpango gani kuchukua hatua stahiki za kinidhamu/kisheria/kiutawala kwa kiongozi huyu na wengine ambao wamekua wakitoa matamko mbalimbali ambayo yanaleta taharuki na pia kupotosha sheria mbalimbali za nchi yetu?
Wizara Katiba Na Sheria
Nasubiri majibu ya hili swali Wizara Katiba Na Sheria
 
Asante sana Cannabis.

Ibara ya 16 ya Katiba ya JMT inalinda haki ya faragha na usalama wa mtu yakiwemo mawasiliano yake. Hivyo, tayari haki ya mtu inalindwa na sheria mama ambayo ni katiba.

Kuhusu swali lako, tuseme tu kwa ufupi wizara tayari inayo mapendekezo kadhaa juu ya sheria mbalimbali. Muda ukifika tutatoa taarifa rasmi.

Asante.
Kuhusu jambo hilo linaleta utata pindi unapopeleka shauri/shtaka mahakamani. Napenda kutambua sheria inasemaje iwapo mtu au taasisi itakukuwa imekutendea vibaya iwe negligence au general damage mana inamlazimu mtu approve cost wakati kuna wakati damage zinazotokea huwezi prove. Hili linatokea nchi za wenzetu endapo mtu au taasisi imekuharibia taswira yako ama imekusumbua kwenye kupata huduma unaweza peleka shauri mahakamani na mahakama ikailazimu taasisi husika kukulipa general damages bila ya kuprove specific damages?
 
Back
Top Bottom