Wizara ya Katiba na Sheria Special thread: Tupe maoni, maswali, malalamiko na ushauri

Kuna baadhi ya kesi huwa zina ngazi ya kimahakama kusikilizwa.
Mfano kesi ya mauaji na uhujumu uchumi haiwezi kusikilizwa mahakama ya mwanzo,lakini wahalifu wamekuwa wakipelekwa katika mahakama hizo ,kesi inapotajwa mtuhumiwa anaambiwa haruhusiwi kuzungumza kwa vile mahakama haina uwezo wa kusikiliza kesi ya namna hiyo

Ushauri wangu
Kwa nini wasiwepo mahakama wenye hadhi ya kusikiliza kesi kama hizo ili aipandishe hadhi mahakama ile kwa muda au wahalifu wawe wanapelekwa moja kwa moja kwenye mahakama ambazo zina mamlaka ya kusilikiza kesi hizo kuliko kupoteza muda na fedha katika mahakama ambayo haina mamlala kisheria kusikiliza kesi hizo.?
Watu wanapiga pesa ndefu kujifanya wanapeleleza
 

Ndugu wana JamiiForums,

Tunashukuru kwa maoni yenu na mijadala inayoendelea hapa kila siku kuhusu masuala ya Katiba na Sheria za nchi yetu. Aidha kuhusu haki za binadamu, rushwa, utawala wa sheria na mengineyo.

Kupitia thread hii maalum; tutapokea maoni, ushauri na hata malalamiko yenu. Tunawahakikishia kuwa tutachukua hatua stahiki kwa haraka zaidi.

Unaweza kututumia pia Private Message (PM) na utajibiwa kwa haraka sana.

Fuatilia ukurasa rasmi wa Wizara ya Katiba na Sheria hapa JamiiForums kupata taarifa mbalimbali kuhusu utoaji wa huduma za Katiba na Sheria nchini Tanzania.

Tufuatilie pia kwenye mitandao yetu ya:

Instagram: @katibasheria_
Twitter: @sheria_katiba
Facebook: Wizara ya Katiba na Sheria

ANUANI ZETU NI:
Wizara ya Katiba na Sheria
Mji wa Serikali, Mtumba
S.L.P. 315,
Dodoma.

Masijala: barua@sheria.go.tz
Simu: +255 26 2310021
Nukushi: 255 26 2321679
Barua pepe: km@sheria.go.tz
Tovuti: www.sheria.go.tz
Je sheria inakataza kushitaki kampuni inayoishi mkoa A kushitakiwa katika mkoa b ambako ndipo ilipoingia makubaliano?katika mkoa b
 

Ndugu wana JamiiForums,

Tunashukuru kwa maoni yenu na mijadala inayoendelea hapa kila siku kuhusu masuala ya Katiba na Sheria za nchi yetu. Aidha kuhusu haki za binadamu, rushwa, utawala wa sheria na mengineyo.

Kupitia thread hii maalum; tutapokea maoni, ushauri na hata malalamiko yenu. Tunawahakikishia kuwa tutachukua hatua stahiki kwa haraka zaidi.

Unaweza kututumia pia Private Message (PM) na utajibiwa kwa haraka sana.

Fuatilia ukurasa rasmi wa Wizara ya Katiba na Sheria hapa JamiiForums kupata taarifa mbalimbali kuhusu utoaji wa huduma za Katiba na Sheria nchini Tanzania.

Tufuatilie pia kwenye mitandao yetu ya:

Instagram: @katibasheria_
Twitter: @sheria_katiba
Facebook: Wizara ya Katiba na Sheria

ANUANI ZETU NI:
Wizara ya Katiba na Sheria
Mji wa Serikali, Mtumba
S.L.P. 315,
Dodoma.

Masijala: barua@sheria.go.tz
Simu: +255 26 2310021
Nukushi: 255 26 2321679
Barua pepe: km@sheria.go.tz
Tovuti: www.sheria.go.tz
Mi naomba kuuliza,kwa nini kesi za Aridhi katika mabaraza ya Aridhi zinachukua muda mrefu sana!?
 
Ni ipi mipaka ya kiutendaji kati ya wizara hii na zingine kama ya mambo ya ndani au habari, utamaduni na michezo? Maana ni mara kadhàa tumeona waziri wa wizara hii akisimama na kutoa kauli ambazo zingefaa kutolewa na wizara zingine? Mf. Kuzuia usambazaji wa habari flani n.k
 
Tumeshuhudia watendaji wa Serikali wakitoa adhabu za viboko kwa watu waliowaona ni wakosaji(mwenye mamlaka ya kusema mtu amekosea ni mahakama tu).

Mfano, yule Naibu waziri wa walemavu, DC arusha na RC Mbeya.

Je, sheria inawaruhusu kufanya hivi?

Ninyi kama wizara yenye dhamana, wajibu wenu ni upi katika hili?
Kati ya wizara zilizo but, wizara yenu inaongoza. Mapungufu mengi ya kusheria yametokea mkiwa kimya, eg rais kuzuia uuzaji wa bia mchana huku sheria ya vileo ipo wazi, wakuu wa mikoa na wilaya kuwaweka watu sero, wakuu wa wilaya na watendaji kuwaweka sero walio kosa hela kulipa vitambulisho vya wajasiria mali. Ni mengi mno lakini hata mara moja hamjawahi sikika mkitoa japo ufafanuzi.
 
Ni maoni mazuri. Hata hivyo, sheria inampa nafasi ya kufungua kesi ya madai ili kulipwa fidia. Ni haki yake kisheria na atapatiwa stahiki zake akifuata utaratibu huo.
Wapo walio thubutu kufungua hayo madai, lakini hawakuwahi fika tena mahakamani mpaka kesi zinafutwa. Siku moja kabla ya siku ya kesi mhusika anashikwa na kuwekwa mahabusu! Kinadharia mfumo wetu wa sheria ni mzuri, kiuhalisia haufai.
 
Swali zuri.

Sheria hii ilizingatia kwamba aliye na taaluma anayo nafasi kubwa ya kuajiriwa tena kutokana na taaluma yake, hivyo bado akawa anaendelea kujazia akiba yake hadi atakapostaafu, tofauti na asiye na taaluma.

Hizi asilimia 33 ni za kumpa unafuu wa kujikimu wakati akifuatilia kazi nyingine.

Asante.
Mmezingatia Kweli suala la ukosefu wa Ajira na Upana wake kwa Tanzania?
 
Tumeshuhudia madaktari kushitakiwa pindi watendapo mabaya kwenye taaluma yao, wahandisi kushitakiwa pindi majengo yanapodondoka.... SHERIA INASEMAJE PALE ALIYEHUKUMIWA NA MAHAKAMA, THEN AKAKATA RUFAA NA KUSHINDA..!? Inasemaje kuhusu mahakama iliyotoa hukumu ya mwanzo!?
Hakuna wajanja kama wanasheria. Wamejivua majukumu yote na kulipa sheri. Hakimu anahukumu vibaya kwa kupokea rushwa, akishinda rufaa, anaambiwa hakimu wa mwanzo aliongozwa vibaya na sheria(s/he was mislead by the law!)
 
Ndugu Tate Mkuu,

Tunaomba tujibu maswali yako kama ifuatavyo:

1. Masuala ya uraia wa Tanzania yanasimamiwa na Sheria ya Uraia Namba 6 ya mwaka 1995 ambayo imebainisha kuwa uraia wa Tanzania upo katika makundi matatu; uraia wa kuzaliwa, uraia wa kurithi na uraia wa tajinisi. Aidha, sheria hii kupitia kifungu cha 7(4)(a)(b) kimeeleza bayana kuwa raia wa Tanzania anaacha kuwa raia kwa kigezo cha kuchukua uraia wa nchi nyingine. Hivyo basi, kutokana na sheria hii na sera ya Tanzania kuhusu uraia ambayo hairuhusu wala kutambua uraia wa nchi mbili, Serikali haiwezi kuweka sheria ya uraia pacha kwa sasa.

Suala hili lilijadiliwa pia wakati wa mchakato wa upatikanaji wa Katiba Mpya ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Bunge Maalum la Katiba ambalo lilijadili pendekezo hili liliona Tanzania bado haipo tayari kwa sasa na Bunge hilo Maalum likatoa pendekezo kwamba; “Mtu yeyote mwenye asili au nasaba ya Tanzania na ambaye ameacha kuwa raia wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kupata uraia wa nchi nyingine atakapokuwa katika Jamhuri ya Muungano atakuwa na hadhi maalum kama itakavyoainishwa katika sheria za nchi.”

Nukuu hii imebainishwa katika Sura ya 6, Ibara ya 72 ya Katiba Inayopendekezwa ya Oktoba, 2014.

2. Suala la Mgombea Binafsi halipo kwa mujibu wa katiba na sheria zetu. Hoja hii lilipendekezwa kwenye mjadala wa katiba mpya ambayo bado haijakamilika. Hivyo hatuwezi kusema ni lini serikali itaruhusu, labda mpaka pale tutakapokuwa na sheria hiyo.

3. Katiba Mpya ni ajenda ya kitaifa. Ni dhahiri taifa letu linahitaji katiba mpya itakayoakisi mahitaji yetu ya sasa na baadae.

Kwa kulitambua hilo, kama itakumbukwa, mchakato wa Katiba Mpya ulifikia pazuri ambapo serikali kwa nia njema iliitisha bunge maalum la katiba likihusisha wadau wanaowakilisha makundi mbalimbali.

Kwa bahati mbaya, baadhi ya makundi muhimu yanayowakilisha wananchi yaligoma kuendelea kuhudhuria bunge hilo wakati mchakato wa kupatikana katiba mpya ukiendelea, hivyo kukwamisha zoezi zima na serikali kulazimika kusitisha.

Vipaumbele vya Serikali kwa sasa, kama ilivyotangazwa na Mheshimiwa Rais John Pombe Magufuli mara kadhaa, ni kushughulikia kero zinazogusa wananchi moja kwa moja na kuboresha utoaji huduma bora ikiwemo kuweka miradi ya kimkakati itakayokuza uchumi wa taifa letu.

Ajenda ya Katiba Mpya itafikiwa tena pale itakapofika wakati wake kwani Katiba ni hitaji la nyakati.

4. Wizara hairidhishwi na uvunjifu wowote wa sheria unaofanywa na askari au mtumishi yeyote kwani sheria ziko wazi. Makosa ya jinai yote yanashughulikiwa na mahakama zetu kwa mujibu wa sheria bila kuangalia mtendaji ni nani.

Asante.
'mapanya wengi hawachimbi shimo likaenda' idadi ya wajumbe wa bunge la katiba ilikuwa kubwa mno kufanikisha lolote la maana. Muda mwingi ukatumika kutunga kanuni.
 
Hakuna wajanja kama wanasheria. Wamejivua majukumu yote na kulipa sheri. Hakimu anahukumu vibaya kwa kupokea rushwa, akishinda rufaa, anaambiwa hakimu wa mwanzo aliongozwa vibaya na sheria(s/he was mislead by the law!)
Hata baada ya kuonekana imem-mislead hakimu, bado sheria hiyo inayomislead mahakimu haibadirishwi..!!
 
Swali zuri.

Sheria hii ilizingatia kwamba aliye na taaluma anayo nafasi kubwa ya kuajiriwa tena kutokana na taaluma yake, hivyo bado akawa anaendelea kujazia akiba yake hadi atakapostaafu, tofauti na asiye na taaluma.

Hizi asilimia 33 ni za kumpa unafuu wa kujikimu wakati akifuatilia kazi nyingine.

Asante.

Kwanza asanteni kwa kuanzisha huu uzi hapa ni jambo jema.

Majibu yenu kwa mdau ( man dunga ) yanaleta maswali mengi zaidi kuhusu sheria ya mafao. Kwanza, Je ni kweli Selikari na wizara haina taarifa kuwa kuna tatizo kubwa la ajira Tanzania? Mifano ni mingi sana na mojawapo ni zile nafasi za ajira zilizotangazwa na TRA mwaka jana nafasi ni moja wanaomba watu zaidi ya 1000 au zaidi, sasa kama kuna tatizo la ajira na ni kubwa kwanini mseme mwenye taaluma ana nafasi kubwa ya kuajiriwa, hao waliopo mtaani na wakakosa ajira hawana taaluma?

Swali lingine, Je kila mwenye taaluma anihitaji kufanya kazi hadi uzeeni (hili pia limeulizwa na DeepPond )? ni lini mlifanya utafiti mkagundua kuwa watanzania wanahitaji kufanya kazi mpaka wawe wazee ndio muwalipe mafao yao?

Kingine hamuoni kuwa huu ubaguzi unapunguza uwezekano wa kufunguliwa kwa biashara endelevu, maana kama utampatia mtu mwenye taaluma mafao yake angali bado ana nguvu za kufikiria na hali ya kufanya kazi (akiwa kijana) uwezekano wa yeye kuwekeza kwa kuanzisha biashara ni mkubwa hivyo kuongeza nafasi za jira na mapato katika nchi na kuleta ukuaji wa uchumi. Sasa kwa sheria hii ni wangapi wanashindwa kufanya hivyo na badala yake mmewafanya wawe watu wa kutegemea ajira?
 
Swali: kwanini faini za barabarani ni sawa kwa vyombo vyote vya usafiri? mfano pikipiki ni elfu 30 sawa na 113 scania, kwanini faini isiwe kulingana na ukubwa wa gari? hii kitu inachochea rushwa sababu bodaboda atatoa wapi fedha za kulipa faini na badala yake ana amua kutoa rushwa
 

Ndugu wana JamiiForums,

Tunashukuru kwa maoni yenu na mijadala inayoendelea hapa kila siku kuhusu masuala ya Katiba na Sheria za nchi yetu. Aidha kuhusu haki za binadamu, rushwa, utawala wa sheria na mengineyo.

Kupitia thread hii maalum; tutapokea maoni, ushauri na hata malalamiko yenu. Tunawahakikishia kuwa tutachukua hatua stahiki kwa haraka zaidi.

Unaweza kututumia pia Private Message (PM) na utajibiwa kwa haraka sana.

Fuatilia ukurasa rasmi wa Wizara ya Katiba na Sheria hapa JamiiForums kupata taarifa mbalimbali kuhusu utoaji wa huduma za Katiba na Sheria nchini Tanzania.

Tufuatilie pia kwenye mitandao yetu ya:

Instagram: @katibasheria_
Twitter: @sheria_katiba
Facebook: Wizara ya Katiba na Sheria

ANUANI ZETU NI:
Wizara ya Katiba na Sheria
Mji wa Serikali, Mtumba
S.L.P. 315,
Dodoma.

Masijala: barua@sheria.go.tz
Simu: +255 26 2310021
Nukushi: 255 26 2321679
Barua pepe: km@sheria.go.tz
Tovuti: www.sheria.go.tz
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, imemhukumu, mmiliki wa kampuni ya kufua umeme ya IPTL, Harbinder Seth kulipa fidia ya Sh26.9 bilioni baada ya kupatikana na hatia ya kujipatia Sh309 bilioni kwa njia ya udanganyifu.

YAANI KAJIPATIA BIL309 ISIVYO HALALI FAINI BIL29
 
Mimi nataka kufahamu inakuwaje kuna adhabu zinazotoka kwa mujibu wa sheria lakini ukizitathimini unaona kabisa sheria inamapungufu lakini wizara ipo na haijali kabisa.

Mfano:
Mtu kakwapua mabilioni ya serikali halafu adhabu inakuja aende jela miaka mitatu au alipe faini ya milioni 50, sasa mtu kaiba bilioni faini milioni ndio nini sasa?
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, imemhukumu, mmiliki wa kampuni ya kufua umeme ya IPTL, Harbinder Seth kulipa fidia ya Sh26.9 bilioni baada ya kupatikana na hatia ya kujipatia Sh309 bilioni kwa njia ya udanganyifu.
 
26 Reactions
Reply
Back
Top Bottom