Peramiho yetu
JF-Expert Member
- May 25, 2018
- 5,304
- 14,913
Mkuu umetufumbua Sana kumbe ndio Hali halisi ilivyo huko kwenye sekta ya afyaBila kulipa hiyo hela, daktari angekatwa mshahara au posho yake, kinachoendelea kwenye vituo vya afya kuhusu ukusanyaji wa mapato, audits za fedha, dawa na huduma kimewafanya watumishi waone hakuna haja tena ya kuheshimu utu na kuwa na huruma wala busara maana ukifanya hivyo unaitwa mwizi wa dawa au fedha za umma, taratibu za kupata msamaha wa matibabu kwa mtu asiye na uwezo zimekuwa ngumu mno sawa na kusema tu misamaha hakuna maana mpaka unakamilisha kupata msamaha kama ni mgonjwa sana ndugu yako atakuwa mbele za haki, mtumishi akijaribu kupindisha taratibu akatoa msamaha haraka ataitwa mwizi na atalipa mwenyewe fedha hizo. Roho mbaya ya watumishi wa afya inayosemwa siyo ya kuzaliwa nayo, imetengenezwa na mfumo wenye negative attitude na watumishi wa afya nchini, hivyo system hiyohiyo inao uwezo wa kuiondoa kwa kubadili attitude hiyo, ni lini jambo zuri lililofanywa na watumishi wa afya limeongelewa? Wao hufanya mabaya kila siku? Ukiyatukana Maji kwenye glass yakikukwama usilalamike, hii ni nature, ndivyo ilivyo, inakupa unachotia. Kusema haya sio kwamba naunga mkono tendo baya alilofanya huyo ndugu au matendo mengine maovu, hapana, najaribu kuonesha wapi tulipojikwaa badala ya kulaumu tulikoangukia.
Nadhan mwamba amefanya vile Kama kufikisha meseji huenda ashawah kukatwa fefha kwa wema wake huko nyuma
HAKIKA USILOLIJUA N SAWA NA USIKU WA GIZA
Sent from my TECNO F1 using JamiiForums mobile app