Wizara ya Afya yamtafuta mtaalamu aliyefumua jeraha la mgonjwa baada ya kushindwa kulipa hela

Bila kulipa hiyo hela, daktari angekatwa mshahara au posho yake, kinachoendelea kwenye vituo vya afya kuhusu ukusanyaji wa mapato, audits za fedha, dawa na huduma kimewafanya watumishi waone hakuna haja tena ya kuheshimu utu na kuwa na huruma wala busara maana ukifanya hivyo unaitwa mwizi wa dawa au fedha za umma, taratibu za kupata msamaha wa matibabu kwa mtu asiye na uwezo zimekuwa ngumu mno sawa na kusema tu misamaha hakuna maana mpaka unakamilisha kupata msamaha kama ni mgonjwa sana ndugu yako atakuwa mbele za haki, mtumishi akijaribu kupindisha taratibu akatoa msamaha haraka ataitwa mwizi na atalipa mwenyewe fedha hizo. Roho mbaya ya watumishi wa afya inayosemwa siyo ya kuzaliwa nayo, imetengenezwa na mfumo wenye negative attitude na watumishi wa afya nchini, hivyo system hiyohiyo inao uwezo wa kuiondoa kwa kubadili attitude hiyo, ni lini jambo zuri lililofanywa na watumishi wa afya limeongelewa? Wao hufanya mabaya kila siku? Ukiyatukana Maji kwenye glass yakikukwama usilalamike, hii ni nature, ndivyo ilivyo, inakupa unachotia. Kusema haya sio kwamba naunga mkono tendo baya alilofanya huyo ndugu au matendo mengine maovu, hapana, najaribu kuonesha wapi tulipojikwaa badala ya kulaumu tulikoangukia.
Mkuu umetufumbua Sana kumbe ndio Hali halisi ilivyo huko kwenye sekta ya afya

Nadhan mwamba amefanya vile Kama kufikisha meseji huenda ashawah kukatwa fefha kwa wema wake huko nyuma

HAKIKA USILOLIJUA N SAWA NA USIKU WA GIZA

Sent from my TECNO F1 using JamiiForums mobile app
 
Nimemsikiliza huyo kiongozi kaongea kwa utu na busara sana kwamba huyo mama kupata hio ajali ni dharura,je kuna mtu huwa anajiandaa na ajali au dharura?

Hivi huyo daktari unawezaje kufanya unyama kama huu?

Na alivyo na roho Chafu,Huyu hata akipewa dili la kuiba vitovu vya watoto hapo kituoni anafanya huyu
 
Nimemsikiliza huyo kiongozi kaongea kwa utu na busara sana kwamba huyo mama kupata hio ajali ni dharura,je kuna mtu huwa anajiandaa na ajali au dharura?

Hivi huyo daktari unawezaje kufanya unyama kama huu?

Na alivyo na roho Chafu,Huyu hata akipewa dili la kuiba vitovu vya watoto hapo kituoni anafanya huyu
Hata mabandama atanyofoa.
 
Sasa kule kufumua ndio hatadaiwa pesa?!

Au nyuzi na dawa alizotumia zinaweza

kutumika tena?!

Angezuia hata simu basi..
 
Wizara ya Afya imepokea kwa masikitiko makubwa taarifa hii inayozunguka mitandaoni kuwa, mtaalamu wa Afya katika kituo ambacho bado hakijatambuliwa amemshona mgonjwa jeraha kisha akalifumua kwa madai kuwa mgonjwa huyo hakuweza kulipia gharama. Ikiwa hili limetokea nchini Tanzania, basi ni ukiukwaji mkubwa wa huduma za kitabibu. Hivyo, wizara inaomba wenye taarifa za wapi huku au kituo gani wawasilishe mara moja kwa namba ya huduma kea mteja 199 ya wizara ya afya au watume ujumbe mfupi kwenye namba ya waziri wa Afya ya 0734124191.

View attachment 1923425
Aisee
 
Bila kulipa hiyo hela, daktari angekatwa mshahara au posho yake, kinachoendelea kwenye vituo vya afya kuhusu ukusanyaji wa mapato, audits za fedha, dawa na huduma kimewafanya watumishi waone hakuna haja tena ya kuheshimu utu na kuwa na huruma wala busara maana ukifanya hivyo unaitwa mwizi wa dawa au fedha za umma, taratibu za kupata msamaha wa matibabu kwa mtu asiye na uwezo zimekuwa ngumu mno sawa na kusema tu misamaha hakuna maana mpaka unakamilisha kupata msamaha kama ni mgonjwa sana ndugu yako atakuwa mbele za haki, mtumishi akijaribu kupindisha taratibu akatoa msamaha haraka ataitwa mwizi na atalipa mwenyewe fedha hizo. Roho mbaya ya watumishi wa afya inayosemwa siyo ya kuzaliwa nayo, imetengenezwa na mfumo wenye negative attitude na watumishi wa afya nchini, hivyo system hiyohiyo inao uwezo wa kuiondoa kwa kubadili attitude hiyo, ni lini jambo zuri lililofanywa na watumishi wa afya limeongelewa? Wao hufanya mabaya kila siku? Ukiyatukana Maji kwenye glass yakikukwama usilalamike, hii ni nature, ndivyo ilivyo, inakupa unachotia. Kusema haya sio kwamba naunga mkono tendo baya alilofanya huyo ndugu au matendo mengine maovu, hapana, najaribu kuonesha wapi tulipojikwaa badala ya kulaumu tulikoangukia.
Umeongea vizuri sana hatuna budi kujiuliza pia,huenda kuna shida huko kwenye hayo maeneo ya kutoa huduma za afya. Pasi na shaka yanayozungumzwa huku kwetu wananchi ni tofauti na maelekezo wanayokutana nayo watendaji katika maeneo yao ya kazi. Nalaani kwa nguvu zote hilo tukio lililokosa utu na uungwana lakini Wizara na wadau wote tujitafakari kwanini limetokea tukio la namna hiyo!?
 
Si ndio hapo et leo wanajifanya sio..'money oriented'..kifupi hospitalini hakuna utu
Kama huna pesa unafia kitandani wanakupita kama vile hawakuoni kabisa. Kwa sasa hali hii imetamalaki katika sehemu nyingi hapa nchini. Je umepata kusikia wajawazito wakifanyiwa Caesar hata pasipo kuwa na tatizo linalohitaji operation hiyo? Ukishangaa ya Musa utayaona ya Firauni.
 
huyu jamaa ana akili ndogo sana,
hata uwezo wa kujieleza unaonesha alivyo mpumbavu
 
Waziri yuko busy kutest mitambo, sema hii Nchi kwa sinema tuko vizuri sana

20210904_202035.jpg
 
Back
Top Bottom