Wizara ya Afya yamtafuta mtaalamu aliyefumua jeraha la mgonjwa baada ya kushindwa kulipa hela

Analogia Malenga

JF-Expert Member
Feb 24, 2012
5,000
9,862
Wizara ya Afya imepokea kwa masikitiko makubwa taarifa hii inayozunguka mitandaoni kuwa, mtaalamu wa Afya katika kituo ambacho bado hakijatambuliwa amemshona mgonjwa jeraha kisha akalifumua kwa madai kuwa mgonjwa huyo hakuweza kulipia gharama. Ikiwa hili limetokea nchini Tanzania, basi ni ukiukwaji mkubwa wa huduma za kitabibu. Hivyo, wizara inaomba wenye taarifa za wapi huku au kituo gani wawasilishe mara moja kwa namba ya huduma kea mteja 199 ya wizara ya afya au watume ujumbe mfupi kwenye namba ya waziri wa Afya ya 0734124191.

 
Hapa chini ni video ya mzozo kati ya muuguzi wa hospitali na diwani baada ya muuguzi husika kufumua mshono wa mgonjwa aliepata ajali kwa madai ya kutolipa hela.

Diwani amemlaumu muuguzi huyo kwa kuchukua maamuzi bila kumshirikisha au kuwashirikisha ngazi ya kijiji akidai angeweza kumlipia kama angemtaarifu kwani ndio mdau wake ikizingatiwa ilikuwa ajali hivyo ni dharula ambayo hakuwa ameandaa pesa yake.

Muuguzi akijitetea, amesema alimwambia atafute uwezekano kabla ya kufikia uamuzi huo.

Wizara ya afya imeshtushwa na kusikitishwa na video hiyo huku ikiomba taarifa za mahali na kituo cha afya ulipofanyika ukiukwaji wa huduma za kitabibu
 
Wafanyakazi kama hawa ni wakutimua, Nchi ina vijana wengi ambao hawana ajira
 
video ipo kweny page ya michuzi na wizara ya afya
instagram
 
Back
Top Bottom