Uzima Tele
JF-Expert Member
- Jan 20, 2023
- 1,532
- 3,535
Tundu Lissu Mwenyekiti wa CHADEMA ameamua kujitoa mwenyewe sadaka/dhabihu ya mateso kwa ajili ya ukombozi na wokovu wa Watanganyika wote
Angekuwa ni mtu anayefanya haya kwa faida binafsi (personal benefits) ili apate vitu vya dunia hii kama fedha, vyeo, majumba, ardhi nk vitokanavyo na dhuluma na damu za Watanganyika, basi bila shaka Tundu Lissu angeshakuwa tajiri na anaishi maisha ya anasa sana
Ameshapitia majaribu ya kupewa fedha, vyeo na fahari zingine ili akane misimamo yake, ili auze utu na heshima yake kama Nabii Balaamu au Yuda Iskariote. Lakini ameshinda yote. Bado tuna mashaka na nia ya mtu huyu?
HAPANA.!
Ndani ya mtu huyu mimi naliona kusudi la Mungu mwenyewe kwa ajili ya Tanganyika/Tanzania. Mungu kaliweka kusudi lake ndani ya Tundu Lissu. Mungu ameweka Utume Mtakatifu kwa ajili ya ukombozi na wokovu wa taifa hili zuri la Tanganyika kupitia mtu huyu. Huyu ni mtengeneza njia, ni sauti ya mtu aliaye nyikani kutengeneza njia ya Rais mwema ajaye wa nchi hii
Kusudi la Mungu aliye hai huwa halishindwi, litatimia kwa wakati sahihi uliopangwa. Wengine hatuwezi kupitia njia ya mateso anayopitia ndugu yetu, mteule wa Mungu huyu
Wengine hatuwezi kuubeba ujasiri alionao hadharani akijua kuwa kwa ujasiri wake huo, anaweza kukutana na kifo. Hata hivyo, Tundu Lissu HATAKUFA KAMWE hadi Mungu ametimiza kusudi lake ktk yeye
Waliobeba kusudi la Mungu hupewa uwezo wa kimungu, roho ya ujasiri, ulinzi mtakatifu. Ndio maana TL hajali lolote lililo mbele yake. Anaingalia Tanganyika na pengine Tanzania zaidi kuliko kujiona yeye binafsi na maslahi yake
Ndugu zangu waungwana wote, natoa wito kwa sisi wengine wote tusioweza kushiriki kwenye harakati hizi za ukombozi zenye maumivu ya moja kwa moja, basi tushiriki kwa njia zingine kama;
1. Kupiga magoti kila siku kuomba Mungu kwa ajili ya Tundu Lissu na CHADEMA hii mpya
2. Kutoa michango na misaada ya kifedha, mali na chochote ulichonacho kwa ajili ya CHADEMA na hususani familia ya Tundu Lissu ili iishi na kupata mahitaji yake muhimu ya kila siku wakati baba yao akiwa gerezani
3. Moral & Emotional support. Hebu wapenda haki wote tusikubali kukatishwa tamaa na shetani wafuasi wake binadamu ambao wanaunga mkono udhalimu na uonevu huu unaoendelea sasa nchini mwetu. Tutiane moyo na kwa umoja wetu tukabiliane na yeyote aliye kinyume cha HAKI
4. Tututumie platforms zilizopo kama vile social medias, YouTube channels nk kusukuma agenda za kudai HAKI, UHURU na UWAZI na ukombozi wa nchi na taifa letu toka mikononi mwa hayawani
Angekuwa ni mtu anayefanya haya kwa faida binafsi (personal benefits) ili apate vitu vya dunia hii kama fedha, vyeo, majumba, ardhi nk vitokanavyo na dhuluma na damu za Watanganyika, basi bila shaka Tundu Lissu angeshakuwa tajiri na anaishi maisha ya anasa sana
Ameshapitia majaribu ya kupewa fedha, vyeo na fahari zingine ili akane misimamo yake, ili auze utu na heshima yake kama Nabii Balaamu au Yuda Iskariote. Lakini ameshinda yote. Bado tuna mashaka na nia ya mtu huyu?
HAPANA.!
Ndani ya mtu huyu mimi naliona kusudi la Mungu mwenyewe kwa ajili ya Tanganyika/Tanzania. Mungu kaliweka kusudi lake ndani ya Tundu Lissu. Mungu ameweka Utume Mtakatifu kwa ajili ya ukombozi na wokovu wa taifa hili zuri la Tanganyika kupitia mtu huyu. Huyu ni mtengeneza njia, ni sauti ya mtu aliaye nyikani kutengeneza njia ya Rais mwema ajaye wa nchi hii
Kusudi la Mungu aliye hai huwa halishindwi, litatimia kwa wakati sahihi uliopangwa. Wengine hatuwezi kupitia njia ya mateso anayopitia ndugu yetu, mteule wa Mungu huyu
Wengine hatuwezi kuubeba ujasiri alionao hadharani akijua kuwa kwa ujasiri wake huo, anaweza kukutana na kifo. Hata hivyo, Tundu Lissu HATAKUFA KAMWE hadi Mungu ametimiza kusudi lake ktk yeye
Waliobeba kusudi la Mungu hupewa uwezo wa kimungu, roho ya ujasiri, ulinzi mtakatifu. Ndio maana TL hajali lolote lililo mbele yake. Anaingalia Tanganyika na pengine Tanzania zaidi kuliko kujiona yeye binafsi na maslahi yake
Ndugu zangu waungwana wote, natoa wito kwa sisi wengine wote tusioweza kushiriki kwenye harakati hizi za ukombozi zenye maumivu ya moja kwa moja, basi tushiriki kwa njia zingine kama;
1. Kupiga magoti kila siku kuomba Mungu kwa ajili ya Tundu Lissu na CHADEMA hii mpya
2. Kutoa michango na misaada ya kifedha, mali na chochote ulichonacho kwa ajili ya CHADEMA na hususani familia ya Tundu Lissu ili iishi na kupata mahitaji yake muhimu ya kila siku wakati baba yao akiwa gerezani
3. Moral & Emotional support. Hebu wapenda haki wote tusikubali kukatishwa tamaa na shetani wafuasi wake binadamu ambao wanaunga mkono udhalimu na uonevu huu unaoendelea sasa nchini mwetu. Tutiane moyo na kwa umoja wetu tukabiliane na yeyote aliye kinyume cha HAKI
4. Tututumie platforms zilizopo kama vile social medias, YouTube channels nk kusukuma agenda za kudai HAKI, UHURU na UWAZI na ukombozi wa nchi na taifa letu toka mikononi mwa hayawani
Mungu wa mbinguni katika Yesu Kristo awabariki nyote🙏🏻🙏🏻