Kiraka
JF-Expert Member
- Feb 1, 2010
- 4,630
- 4,687
Mangi usiombee,,, ni vitu vidogo sana but, y udokoe,,, tena vya wanao.....wapime mafuta tuu ruwa mangi....
Mzee pole sana na huu mkasa. Naomba unijibu maswali yafuatayo kiukweli ili inisaidie katika kukupa ushauri
1. Je mahusiano ya mkeo na familia yako yakoje (Ndugu wa upande wako, wazazi na wengine)
2. Wewe uhusiano wako na ndugu wa upande wa mkeo , kabla ya tukio la kuwaondoa hapo kwako ilikuwaje?
3. Hapo kwako kuna ndugu zako wengine wanaishi? Au wewe unasaidia ndugu zako kwa kiasi gani? uki compare na mkeo?
4. Ki elimu wewe na mkeo mna level sawa? kama si sawa nani kamzidi mwenzie.
5. Ki mapato nani kamzidi mwenzie?
6. Familia zenu kimapato ipi iko juu na kwa kiasi gani?
7. Je mkeo kwao ndio mtoto mwenye mafanikio pekee? na je wewe kwenu ndio mtoto mwenye mafanikio pekee?
Asante naomba jibu bila kupotosha ili nijaribu kukupa ushauri kwani mzee waweza haribu ndoa na future ya wanao kwenye hili tukio.