Wife wangu ananiibia, ushauri unahitajika

Wife wangu ananiibia, ushauri unahitajika

Mkeo elimu dunia haijamkomboa ila ukifilisika tutajua tabia nyingi za mkeo.

sio mpaka afilisike, Afanye tu mama ndie ahudumu mwezi mmoja kwa mahitaji ya nyumbani yote kama kuna bili zote za maji umeme na king'amuI ili iwe sababu ya msamaha kwa matendo aliyoyafanya, itaona reaction yake manake wao kutoa vyao inauma sana kuliko vya kutolewa na wanaume zao.
 
Potezea mkuu. Ila ili wasikuibie, usiwe unanunua vitu in bulky... Anza kununua robo kilo sukari, mchele kilo kilo mpaka wtanyooka tu. Kuna ndugu hawapendi kujishughulisha na kazi yao ni kula vya wenzao tu...
 
we jamaa mchoyo...ingawa pia mke wako ana makosa

Inawezekana kabisa tabia hiyo aliyonayo umemjengea wewe
 
Thank you all, hii issue ni ya 2014 september, zaidi ya mwaka na nusu.
Kila mtu kasema aliloweza kusema wengine wametukana na kukashifu, ila kila mmoja ana mtazamo wake ktk hili, but hapa kuna wenye ndoa na wasio na ndoa,,, kama huna umechangia hujielewi, kwa yule aliyechangia na ana ndoa atakuwa na mtazamo wake. Kwa kifupi tulitengana, hakutaka kurudi na yeye ndie aliepeleka madai ya TALAKA mahakamani, kwani baada ya kuhamia kwa kakake, THEN KWENYE NYUMBA YAKE, hakutaka mawasiliano na mimi, tuliwasiliana kupitia mwanasheria wake, she got money as I said early, but kwangu sio tatizo am well enough to run anything appear. Watoto ninao na wanaendelea vema, she come to visit them kama atakavyo. Sihitaji kujipendekeza hata kidogo, nakubaliana na yeye... what i believe now ulikuwa ni mpango wa muda mrefu sana ukishirikisha wadogo zake. TATIZO NI UBINAFSI, TENA ULIOPITILIZA, mengi niliyabeba but imefika TAMATI. Now anakimbizana na talaka, thanks GOD sehemu kubwa ya mali niliandikisha watoto, na yeye ndo kajitoa.......NDOA NI YA WATU WAWILI, WAKISHINDWA KUAFIKIANA HAKUNA NDOA TENA.

ASANTENI SANA.
 
pole sana kwa maswaibu yaliyokukuta. Suala lako ni zito ila umelilea sana mwenyewe. Cha kufanya mkeo akitoka aite watu wakubwa wa kwao mkae kikao ili kwanza msuluishe hayo matatizo yaliyofikia kupelekana polisi. Baada ya hapo weka taratibu na sheria za nyumba yako mfano kaeni chini pigeni hesabu ya matumizi ya nyumbani kwako kwa mwezi na ukishayapata muwe mnachangia nusu kwa nusu na hizo hela mpe yeye wewe baki na gharama za umeme maji na TV pia kama mkeo ana gari akikisha anaweka mafuta mwenyewe. Masuala mengine kama ujenzi nk unakomaa nayo wewe pia na ada za watoto ila vitu vidogo kama kwenda sokoni na kununua vitu vya ndani mwache afanye yeye ila under control
 
Mkeo ni tatizo ila wewe ni tatizo zaidi, hakukua na sababu ya kuwafukuza hao ndugu zake, ungekaa nae chini na kumwambia awe anachangia mahitaji ya hapo nyumbani.
 
Thank you all, hii issue ni ya 2014 september, zaidi ya mwaka na nusu.
Kila mtu kasema aliloweza kusema wengine wametukana na kukashifu, ila kila mmoja ana mtazamo wake ktk hili, but hapa kuna wenye ndoa na wasio na ndoa,,, kama huna umechangia hujielewi, kwa yule aliyechangia na ana ndoa atakuwa na mtazamo wake. Kwa kifupi tulitengana, hakutaka kurudi na yeye ndie aliepeleka madai ya TALAKA mahakamani, kwani baada ya kuhamia kwa kakake, THEN KWENYE NYUMBA YAKE, hakutaka mawasiliano na mimi, tuliwasiliana kupitia mwanasheria wake, she got money as I said early, but kwangu sio tatizo am well enough to run anything appear. Watoto ninao na wanaendelea vema, she come to visit them kama atakavyo. Sihitaji kujipendekeza hata kidogo, nakubaliana na yeye... what i believe now ulikuwa ni mpango wa muda mrefu sana ukishirikisha wadogo zake. TATIZO NI UBINAFSI, TENA ULIOPITILIZA, mengi niliyabeba but imefika TAMATI. Now anakimbizana na talaka, thanks GOD sehemu kubwa ya mali niliandikisha watoto, na yeye ndo kajitoa.......NDOA NI YA WATU WAWILI, WAKISHINDWA KUAFIKIANA HAKUNA NDOA TENA.

ASANTENI SANA.
pole na hongera mkuu
 
HUYO ANAKURUDISHA NYUMA ...SASA MAISHA HAYA..PESA KWA MFUKO..AKILI KU MKICHWA ...
 
Mm cijaelewa kabisa, anakaz yake nzur tu na huwa hachangii kitu, inaamana uwezo wa kuwatunza ndugu zake anao au umemtafutia sababu.
 
Wandugu

Hili janga ni kubwa sana kwangu, nimekuwa na kawaida ya kununua mahitaji yote ya nyumbani kama baba na kiongozi wa familia kuna kipindi kulitokea mtafaruku kisa kikiwa shemeji zangu wamejaa kwangu, nikatangaza la mgambo sitaki cha shemeji wa wala wifi kwangu......wote wakatawanyika.

Bi mkubwa ilimuuma sana hakuwa na jinsi, kwani kama ni msaada niliwapa ikiwa ni kusoma na mambo mengine ya kuwasaidia, but aliwadekeza bila kujali kuwa niliyemuoa ni yeye pekee wamekaa kwangu kwa muda mrefu tuu.

Kwa hasira akawapangishia chumba, hata sijui ni wapi.

Bi mkubwa ana kazi yake nzuri tuu, but hachangiii chochote ndani ya nyumba, na wala kwangu sio tatizo kabisa, namshukuru Mola wanetu 2 wana afya njema sana na wana furaha.

Tatizo linalonisukuma kutaka ushauri hapa ni hii tabia aliyoanzisha bi mkubwa, anabeba vyakula ndani mwetu anapeleka kwa wadogo zake, niligundua kipindi fulani nikamkanya, akataharuki kwanza nimejuaje, akahamishia ugomvi kwa dada na kaka (wasaidizi wetu pale home), mpaka kaka aka resign.

Safari ikaendelea hakuacha hiyo tabia, tena imeota mizizi. Kila j3 hua anakuja na mdogo wake mmoja, anamfungashia furushi la mchele, sukari, mafuta ya kula, matunda na kila aina ya kitu apendacho.

Nikaweka mtego, kijana wangu mmoja ndo jasusi langu pale home, nimelifundisha likakomaa, kama zoba hivi, so bi mkubwa wala hana hofu nae ya kunitonya mie.

Siku ya siku nikajipanga na kijana wa kova, coz yule anaetoka na furushi kwangu namshuku ni mwizi, ile ametoka kwa gate, nilimwambia kijana afunge fasta ili bi mkubwa asijue nini kimetokea nje, ilikuwa mida ya saa nne usiku. Kabaaang, kanaswa binti, polisi fasta chini ya ulinzi, mie huyo nikaingia ndani kama sijui kunani.

Muda si mrefu akapigiwa simu aende kituoni, huko binti keshanaswa vitasa vya haja kasema kila kitu, aliogopa kuniomba nimsindikize, so akaenda na kaka, ile kafika na yeye chini ya ulinzi, walilala selo jana.

Asubuhi nikapitia, pale wakawa weshamumbia mie ndo niliwapa taarifa ya mchezo mzima, nikaomba waendelee kukaa pale, mchana kakayake akaenda kumtoa.

Ndugu zangu huyu mwanamke kalivuruga, kwa maelezo ya mdogo wake wameiba vitu vingi sana, hasa vya watoto, coz ana mdogo wake ana mtoto analingana na wa kwetu wa 1.

Kubwa nafikiria ni watoto wetu, najua wanaraha hata wakiwa na mimi, ila mama yao ni muhimu katika makuzi.

Hebu nipeni ushauri kidogo kabla sijaamua wa kwangu.

Hii kesi niipeleke mahakamani?
Kweli ni mdokozi, tena anakwiba vyakula vya wanawe, nitengane nae?
Anakazi yake nzuri, nikamshtaki kwa bosi wake?


Ongezeeni yatakayo nitoa hapa nilipo.

Karibuni
Mungu akusaidie na kizazi chako maana unatiha huruma Sana ujitambui tu
 
Wandugu

Hili janga ni kubwa sana kwangu, nimekuwa na kawaida ya kununua mahitaji yote ya nyumbani kama baba na kiongozi wa familia kuna kipindi kulitokea mtafaruku kisa kikiwa shemeji zangu wamejaa kwangu, nikatangaza la mgambo sitaki cha shemeji wa wala wifi kwangu......wote wakatawanyika.

Bi mkubwa ilimuuma sana hakuwa na jinsi, kwani kama ni msaada niliwapa ikiwa ni kusoma na mambo mengine ya kuwasaidia, but aliwadekeza bila kujali kuwa niliyemuoa ni yeye pekee wamekaa kwangu kwa muda mrefu tuu.

Kwa hasira akawapangishia chumba, hata sijui ni wapi.

Bi mkubwa ana kazi yake nzuri tuu, but hachangiii chochote ndani ya nyumba, na wala kwangu sio tatizo kabisa, namshukuru Mola wanetu 2 wana afya njema sana na wana furaha.

Tatizo linalonisukuma kutaka ushauri hapa ni hii tabia aliyoanzisha bi mkubwa, anabeba vyakula ndani mwetu anapeleka kwa wadogo zake, niligundua kipindi fulani nikamkanya, akataharuki kwanza nimejuaje, akahamishia ugomvi kwa dada na kaka (wasaidizi wetu pale home), mpaka kaka aka resign.

Safari ikaendelea hakuacha hiyo tabia, tena imeota mizizi. Kila j3 hua anakuja na mdogo wake mmoja, anamfungashia furushi la mchele, sukari, mafuta ya kula, matunda na kila aina ya kitu apendacho.

Nikaweka mtego, kijana wangu mmoja ndo jasusi langu pale home, nimelifundisha likakomaa, kama zoba hivi, so bi mkubwa wala hana hofu nae ya kunitonya mie.

Siku ya siku nikajipanga na kijana wa kova, coz yule anaetoka na furushi kwangu namshuku ni mwizi, ile ametoka kwa gate, nilimwambia kijana afunge fasta ili bi mkubwa asijue nini kimetokea nje, ilikuwa mida ya saa nne usiku. Kabaaang, kanaswa binti, polisi fasta chini ya ulinzi, mie huyo nikaingia ndani kama sijui kunani.

Muda si mrefu akapigiwa simu aende kituoni, huko binti keshanaswa vitasa vya haja kasema kila kitu, aliogopa kuniomba nimsindikize, so akaenda na kaka, ile kafika na yeye chini ya ulinzi, walilala selo jana.

Asubuhi nikapitia, pale wakawa weshamumbia mie ndo niliwapa taarifa ya mchezo mzima, nikaomba waendelee kukaa pale, mchana kakayake akaenda kumtoa.

Ndugu zangu huyu mwanamke kalivuruga, kwa maelezo ya mdogo wake wameiba vitu vingi sana, hasa vya watoto, coz ana mdogo wake ana mtoto analingana na wa kwetu wa 1.

Kubwa nafikiria ni watoto wetu, najua wanaraha hata wakiwa na mimi, ila mama yao ni muhimu katika makuzi.

Hebu nipeni ushauri kidogo kabla sijaamua wa kwangu.

Hii kesi niipeleke mahakamani?
Kweli ni mdokozi, tena anakwiba vyakula vya wanawe, nitengane nae?
Anakazi yake nzuri, nikamshtaki kwa bosi wake?


Ongezeeni yatakayo nitoa hapa nilipo.

Karibuni
By the way ungelikuwa mwalimu mzr Ila kwakuwa ujitambui unatapika katika nchi huru poleeeeeeeeeee
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom