nosspass
JF-Expert Member
- Mar 7, 2013
- 5,798
- 4,752
Wandugu
Hili janga ni kubwa sana kwangu, nimekuwa na kawaida ya kununua mahitaji yote ya nyumbani kama baba na kiongozi wa familia kuna kipindi kulitokea mtafaruku kisa kikiwa shemeji zangu wamejaa kwangu, nikatangaza la mgambo sitaki cha shemeji wa wala wifi kwangu......wote wakatawanyika.
Bi mkubwa ilimuuma sana hakuwa na jinsi, kwani kama ni msaada niliwapa ikiwa ni kusoma na mambo mengine ya kuwasaidia, but aliwadekeza bila kujali kuwa niliyemuoa ni yeye pekee wamekaa kwangu kwa muda mrefu tuu.
Kwa hasira akawapangishia chumba, hata sijui ni wapi.
Bi mkubwa ana kazi yake nzuri tuu, but hachangiii chochote ndani ya nyumba, na wala kwangu sio tatizo kabisa, namshukuru Mola wanetu 2 wana afya njema sana na wana furaha.
Tatizo linalonisukuma kutaka ushauri hapa ni hii tabia aliyoanzisha bi mkubwa, anabeba vyakula ndani mwetu anapeleka kwa wadogo zake, niligundua kipindi fulani nikamkanya, akataharuki kwanza nimejuaje, akahamishia ugomvi kwa dada na kaka (wasaidizi wetu pale home), mpaka kaka aka resign.
Safari ikaendelea hakuacha hiyo tabia, tena imeota mizizi. Kila j3 hua anakuja na mdogo wake mmoja, anamfungashia furushi la mchele, sukari, mafuta ya kula, matunda na kila aina ya kitu apendacho.
Nikaweka mtego, kijana wangu mmoja ndo jasusi langu pale home, nimelifundisha likakomaa, kama zoba hivi, so bi mkubwa wala hana hofu nae ya kunitonya mie.
Siku ya siku nikajipanga na kijana wa kova, coz yule anaetoka na furushi kwangu namshuku ni mwizi, ile ametoka kwa gate, nilimwambia kijana afunge fasta ili bi mkubwa asijue nini kimetokea nje, ilikuwa mida ya saa nne usiku. Kabaaang, kanaswa binti, polisi fasta chini ya ulinzi, mie huyo nikaingia ndani kama sijui kunani.
Muda si mrefu akapigiwa simu aende kituoni, huko binti keshanaswa vitasa vya haja kasema kila kitu, aliogopa kuniomba nimsindikize, so akaenda na kaka, ile kafika na yeye chini ya ulinzi, walilala selo jana.
Asubuhi nikapitia, pale wakawa weshamumbia mie ndo niliwapa taarifa ya mchezo mzima, nikaomba waendelee kukaa pale, mchana kakayake akaenda kumtoa.
Ndugu zangu huyu mwanamke kalivuruga, kwa maelezo ya mdogo wake wameiba vitu vingi sana, hasa vya watoto, coz ana mdogo wake ana mtoto analingana na wa kwetu wa 1.
Kubwa nafikiria ni watoto wetu, najua wanaraha hata wakiwa na mimi, ila mama yao ni muhimu katika makuzi.
Hebu nipeni ushauri kidogo kabla sijaamua wa kwangu.
Hii kesi niipeleke mahakamani?
Kweli ni mdokozi, tena anakwiba vyakula vya wanawe, nitengane nae?
Anakazi yake nzuri, nikamshtaki kwa bosi wake?
Ongezeeni yatakayo nitoa hapa nilipo.
Karibuni
Hili janga ni kubwa sana kwangu, nimekuwa na kawaida ya kununua mahitaji yote ya nyumbani kama baba na kiongozi wa familia kuna kipindi kulitokea mtafaruku kisa kikiwa shemeji zangu wamejaa kwangu, nikatangaza la mgambo sitaki cha shemeji wa wala wifi kwangu......wote wakatawanyika.
Bi mkubwa ilimuuma sana hakuwa na jinsi, kwani kama ni msaada niliwapa ikiwa ni kusoma na mambo mengine ya kuwasaidia, but aliwadekeza bila kujali kuwa niliyemuoa ni yeye pekee wamekaa kwangu kwa muda mrefu tuu.
Kwa hasira akawapangishia chumba, hata sijui ni wapi.
Bi mkubwa ana kazi yake nzuri tuu, but hachangiii chochote ndani ya nyumba, na wala kwangu sio tatizo kabisa, namshukuru Mola wanetu 2 wana afya njema sana na wana furaha.
Tatizo linalonisukuma kutaka ushauri hapa ni hii tabia aliyoanzisha bi mkubwa, anabeba vyakula ndani mwetu anapeleka kwa wadogo zake, niligundua kipindi fulani nikamkanya, akataharuki kwanza nimejuaje, akahamishia ugomvi kwa dada na kaka (wasaidizi wetu pale home), mpaka kaka aka resign.
Safari ikaendelea hakuacha hiyo tabia, tena imeota mizizi. Kila j3 hua anakuja na mdogo wake mmoja, anamfungashia furushi la mchele, sukari, mafuta ya kula, matunda na kila aina ya kitu apendacho.
Nikaweka mtego, kijana wangu mmoja ndo jasusi langu pale home, nimelifundisha likakomaa, kama zoba hivi, so bi mkubwa wala hana hofu nae ya kunitonya mie.
Siku ya siku nikajipanga na kijana wa kova, coz yule anaetoka na furushi kwangu namshuku ni mwizi, ile ametoka kwa gate, nilimwambia kijana afunge fasta ili bi mkubwa asijue nini kimetokea nje, ilikuwa mida ya saa nne usiku. Kabaaang, kanaswa binti, polisi fasta chini ya ulinzi, mie huyo nikaingia ndani kama sijui kunani.
Muda si mrefu akapigiwa simu aende kituoni, huko binti keshanaswa vitasa vya haja kasema kila kitu, aliogopa kuniomba nimsindikize, so akaenda na kaka, ile kafika na yeye chini ya ulinzi, walilala selo jana.
Asubuhi nikapitia, pale wakawa weshamumbia mie ndo niliwapa taarifa ya mchezo mzima, nikaomba waendelee kukaa pale, mchana kakayake akaenda kumtoa.
Ndugu zangu huyu mwanamke kalivuruga, kwa maelezo ya mdogo wake wameiba vitu vingi sana, hasa vya watoto, coz ana mdogo wake ana mtoto analingana na wa kwetu wa 1.
Kubwa nafikiria ni watoto wetu, najua wanaraha hata wakiwa na mimi, ila mama yao ni muhimu katika makuzi.
Hebu nipeni ushauri kidogo kabla sijaamua wa kwangu.
Hii kesi niipeleke mahakamani?
Kweli ni mdokozi, tena anakwiba vyakula vya wanawe, nitengane nae?
Anakazi yake nzuri, nikamshtaki kwa bosi wake?
Ongezeeni yatakayo nitoa hapa nilipo.
Karibuni