Candid Scope
JF-Expert Member
- Nov 8, 2010
- 11,897
- 6,933
Mkuu,
Mie siwahukumu hao jamaa na wala sijasoma makala nzima maana naona Kidhungudhungu leo.
Point yangu ilikuwa ni kwamba, Wakatoliki ni kama watu wengine. Kwenye kundi la Kondoo, na Chui wamo. Na kwenye kundi la Chui, na Kondoo pia wamo. Wewe maelezo yako yanawapa hawa jamaa 100% kuwa ni watakatifu na unaweka sheria na mistari kibao kuwa HAWAWEZI.
Narudia tena, mie siwahukumu na hakuna sehemu nimesema kuwa JAMAA WANA MAKOSA. Ila kama Papa mwenyewe alikuwa akishirikiana na Hitler, itakuwa hao wengine? Point yangu ni moja, LOLOTE LILIWEZA KUTOKEA. Wanaweza kuwa ni MAFIA kweli au WAMESINGIZIWA.
Usalama wa Taifa upi unaoongelea? Na mwanasheria mwenyewe ndiyo huyo WEREMA kila siku anapewa shule na Tundu Lissu. Vyombo vyote vya usalama wa Taifa, maboss wake wameteuliwa na yule mwenye jina gani sijui? Ngoja nimuulize John Mnyika........
Kama ungesoma mabandiko yangu hapa utakuja kuelewa kwamba sijajenga utetezi wo wote, ila nimesimama kwenye ukweli kwamba kwa tuhuma na maelezo ya makala ya gazeti, hali kadhalika walio karibu na shirika hilo na kujua yanayojilia wameeleza bayana hapa kwamba:
Kuna mwanashirika mmoja mtajwa katika makala ile alikuwa anafanya mambo kwa siri katika mgodi huo na alipokuja gundulika na shirika na pia kugundulia ameliibia shirika pesa, alishtakiwa na kuwa rejected shirikani kwa kufukuzwa.
Aliposhtakiwa alifungwa, baada ya kutumikia kifungo cha ndani, sasa anatumikia kifungo cha nje. Kwa maana hiyo hawezi tena kurudi shirikani na hata mipango yake ya siri aliyokuwa anaifanya kwenye migodi ile imeshaota mbawa kwa vile alikuwa anafanya kwa kutumia kivuli cha shirika.
Inasemekana baada ya kumpata hayo aliapa kuliadabisha shirika lake kwa kulichafua kama kulipiza kisasi kwa kufukuzwa utawa, na ndicho alichokifanya.
Nimekua nashikilia msimano wangu tangu awali kutokana na uelewa wangu wa mashirika haya na taasisi zake katika kanisa hili, utaratibu unaosemwa katu hauwezi kufanywa na shirika kisheria kwa sababu mradi mkubwa kama ule huasisiwa na kukubaliwa na makao makuu na ndiyo yenye kuuendesha na kugharimia.
Mikataba katika shughuli za uchumi kama hizi haiwezi kufanya tu na kila mwanashirika, ila hufanywa na procurator wa shirika mwenye mamlaka katika mambo ya mikataba na mambo ya uchumi wa monasteri. Hata ingekuwa jimboni kuna procurator wa jimbo anayeshughulikia mambo ya mikataba na matumizi ya pesa, si kila mwanashirika au muumini, na hili walijua na linafahamika si katika mashirika ya dini tu hata taasisi ye yote.
Makala ya gazeti la Raia mwema halijaonyesha waliotia sahihi wadhifa wao, na kwa kuulizia wahusika sisi wengine tunaowafahamu hao wawili hawana nyadhifa za uprocurator wala ukubwa wa shirika, hivyo kwa hoja hiyo na kadiri ya sheria zao shirika halihusiki ila hao wawili personally ndio wanaotakiwa kubeba mzigo na shirika lilishamtema mmojawapo baada ya kugundua madudu aliyoyafanya.
Kwamba mipango ya kumwua Mwaikusa ilifanyika ndani ya Abatia ya Peramiho, hilo jambo zito, maana kama ni kweli Abasia ilifanya hayo dondoo za mikutano yao ya shirika itaonyesha lini na kwa namna gani walifanya kikao chao na theluthi mbili ya wajumbe wa mkutano kurithia kupanga na kutekeleza mauaji hayo. Je, hilo lawezekana?
Kwa taratibu zao za kishirika wana mikutano ifuatayo katika kutekeleza majukumu mazito katika shirika kama ifutatavyo:
- Senioratus (halmashauri kuu/kamati kuu ya shirika)
- Mkutano mkuu wa shirika unaowakutanisha wanashirka wote.
- Mikutano yote huwa na dondoo za mikutano na kumbukumbu za mikutano na mada zilizojadiliwa hutunzwa.
Mimi sijatetea hilo, ila kwa mapungufu kadhaa yaliyojitokeza katika gazeti hilo kwa ujumla inaonekana ni mtu fulani binafsi ambaye alikuwa mwanashirika amehusika na ndiye anayetakiwa kuwajibishwa, la sivyo kama ni shirika limehusika uchunguzi wa wazi ufanyike na hata gazeti litume mwandishi wake kwenda kupata ukweli, si kuandika kitu bila uthibitisho wa pande zote zinazohusika. Huu ndio msimamo wangu mdau Sikonge.