Who is John Tendwa?

Tarehe 27/4/2001, Raisi Benjamin William Mkapa alimteua Bwana John Tendwa kuwa Msajili mpya wa Vyama vya Siasa akichukua nafasi ya George Christopher Liundi ambaye muda wake ulimalizika.

Kabla ya hapo John Tendwa alikuwa wapi na alikuwa anafanya nini - wana JF mpo? - msaada unatakiwa kwani giza lililotanda kuhusu historia yake linaleta wasi wasi.

Je ni Mtanzania? Alizaliwa wapi? Alisomea wapi?

Good question, i mean thread imechelewa lakini si sana,kama tungefanya hivyo kwa Balali ambaye alikuwa maybe raia wa marekani, maybe tungesave ufisadi mwingi sana...

Hatuna utaratibu wa vetting kwenye nafasi muhimu zinazohusisha demokrasia ya kweli, zenye kuhusisha kuwatumikia wananchi wote kama watanzania na si wana ccm,chadema ama CCJ, nafasi zenye ku deal na usalama wa Taifa ie mkurugenzi wake, waziri wa mabo ya ndani nk,jeshi nk...

Ni muhimu bunge liwe linawapitisha watu kama hawa, naona siasa za vyama vingi ni maneno tu lakini mazingira hayaruhusu ama yana ukiritimba!

Ni kama CCM wanavyopractice ufisadi wa kibepari na wakati itikadi zao ni za kijamaa...Tufumbue macho!
 
Tatizo Tanzania wateule wa rais hawapitishwi na Bunge ndiyo maana wengine hata u-research hautagundua chochote kuhusu CV zao na ni kwanini wamechaguliwa kuongoza kitengo au ofisi husika.

Ilitakiwa rasi akifanya uteuzi mzito kama hii ya msajili wa vyama vya siasa basi jina lipelekwe Bungeni na rais mwenyewe au kupitia waliopo chini yake wa-make case ya kwa nini rais kamchagua mtu fulani kwa ajili ya nafasi fulani. Raisi akishatoa maelezo yake (preferably kwa maandishi) kamati husika ijadili uwezo wa mtu huyo kupewa nafasi hiyo. Baada ya hapo mteuliwa mwenyewe apewe nafasi ya kujieleza mbele ya kamati ya Bunge au Bunge lenyewe ni kwa sababu gani anaona ana uwezo wa kuongoza ofisi husika. Kinacho fuata hapo ni mteuliwa kupigiwa kura na Bunge.

Tukifuata utaratibu wa wateule mbali mbali kupitishwa na Bunge basi hatutakuwa na shida ya kuchunguza bila mafanikio mtu katokea wapi. Kupitia utaratibu wa mtu kupitishwa na Bunge, kupitia yeye mwenyewe na aliyemteua wataelezea wasifu wake na kwa nini anafaa. Tusipofanya hivi watu watashika nafasi mbalimbali muhimu bila hata kujua wanatokea wapi.

Kama wanasiasa wanajieleza kwa wananchi ni kwa nini wanafaa (iwe wanadanganya au la) kwa nini na viongozi wengine muhimu wa kuteuliwa wasipitie process hiyo hiyo?

Kuna vitu vingi vidogovidogo tunaweza kufanya ambavyo vitasaidia kuepuka maswali madogo madogo ambayo wala hayakutakiwa kuwa tatizo. Majawabu rahisi yapo kwa matatizo ambayo tunayaona makubwa. Tunahitaji tu kufikiri kidogo na kutunga sheria practical badala ya sheria zisizo na faida zozote kwa taifa.
 
Tatizo Tanzania wateule wa rais hawapitishwi na Bunge ndiyo maana wengine hata u-research hautagundua chochote kuhusu CV zao na ni kwanini wamechaguliwa kuongoza kitengo au ofisi husika.

Ilitakiwa rasi akifanya uteuzi mzito kama hii ya msajili wa vyama vya siasa basi jina lipelekwe Bungeni na rais mwenyewe au kupitia waliopo chini yake wa-make case ya kwa nini rais kamchagua mtu fulani kwa ajili ya nafasi fulani. Raisi akishatoa maelezo yake (preferably kwa maandishi) kamati husika ijadili uwezo wa mtu huyo kupewa nafasi hiyo. Baada ya hapo mteuliwa mwenyewe apewe nafasi ya kujieleza mbele ya kamati ya Bunge au Bunge lenyewe ni kwa sababu gani anaona ana uwezo wa kuongoza ofisi husika. Kinacho fuata hapo ni mteuliwa kupigiwa kura na Bunge.

Tukifuata utaratibu wa wateule mbali mbali kupitishwa na Bunge basi hatutakuwa na shida ya kuchunguza bila mafanikio mtu katokea wapi. Kupitia utaratibu wa mtu kupitishwa na Bunge, kupitia yeye mwenyewe na aliyemteua wataelezea wasifu wake na kwa nini anafaa. Tusipofanya hivi watu watashika nafasi mbalimbali muhimu bila hata kujua wanatokea wapi.

Kama wanasiasa wanajieleza kwa wananchi ni kwa nini wanafaa (iwe wanadanganya au la) kwa nini na viongozi wengine muhimu wa kuteuliwa wasipitie process hiyo hiyo?

Kuna vitu vingi vidogovidogo tunaweza kufanya ambavyo vitasaidia kuepuka maswali madogo madogo ambayo wala hayakutakiwa kuwa tatizo. Majawabu rahisi yapo kwa matatizo ambayo tunayaona makubwa. Tunahitaji tu kufikiri kidogo na kutunga sheria practical badala ya sheria zisizo na faida zozote kwa taifa.
Again tunarudi kule kule, ndio maana tulimwambia MKJJ kuhusiana na upinzani bungeni kujengwa, hilo litawezesha kubadili taratibu nyingi za ki kiritimba....

Kuing'oa ccm kwanza then all is possible, ukpo MKJJ?
 
Again tunarudi kule kule, ndio maana tulimwambia MKJJ kuhusiana na upinzani bungeni kujengwa, hilo litawezesha kubadili taratibu nyingi za ki kiritimba....

Kuing'oa ccm kwanza then all is possible, ukpo MKJJ?

Lakini hili swala ni la Watanzania wote si MKJJ tu. MKJJ hawezi kuleta mabadiliko Bungeni na wala pekee hata kuwa factor ya kuing'oa CCM. This call should be to all Tanzanians.
 
Lakini hili swala ni la Watanzania wote si MKJJ tu. MKJJ hawezi kuleta mabadiliko Bungeni na wala pekee hata kuwa factor ya kuing'oa CCM. This call should be to all Tanzanians.

Change begins in one room,and matter of fact it begins wit mi n you, MKJJ and others, then spread by conveying it to the people, ninazungumzia kuwa ni lazima kuna-influential people ambao ni vital, sijam-single out MKJJ in vain, ila ana influence.... pengine more than me n you, na kwahiyo ni muhimu ku keep an eye on such people, if they use their influence in a good and productive ways then that's ok, but the opposite is a Big No!
 
inamaana hata alipochaguliwa nafasi magazeti hawakutuandikia huyu jamaa ni nani?
 
Pia alishafanya kazi mahakama ya kazi and gues what? ameacha kimada pale.

NI vizuri tumjue huyu mtu, Pamoja na kuwa mtu ambaye sikupenda hii sisijei (sikutaka tuendelee kugawanyika kipindi hiki) yeye hakupaswa kutofanya wajibu wake na amekuwa mkandamizaji sana. Yes inatakiwa tumjue mienendo yake na tabia zake ili tuweze kujua akili yake huwa inawaza vipi.
 
Labda tutafute baba yake au shangazi yake vinginevyo hakuna habari yake yoyote inayojulikana. Inaonekana hata Elimu yake haijulikani. hata magazeti yameanza kumuandika baada ya 2005.
 
Yes, hata mimi nataka nimfahamu huyu bwana. Kuna mtu aliniambia wakati alipodai kuwa hana muda wa kuhakiki wanachama wa CCJ kuwa J. Tendwa ni kigeugeu sana atageuza kauli yake! Muda si muda tukamsikia anahakiki wanachama hao. CCJ baada ya kubaini rafu dhidi ya wanachama wake walimwambia Tendwa asitishe zoezi akagoma! Leteni data za J. Tendwa jamani!
 
Kama kuna wadau wanaweza kunisaidia (naamini itawasaidia wengine) kuweza kumjua vema ni nani, ametoka wapi, na hapa alipo tutarajie wapi ataelekea... (I doubt anaweza kuingia kwenye siasa na akawa upande wa chama 'flani').


Dalili za kuingia kwenye chama flani mie nishaziona ..maongezi yake yanamtambulisha
 
Hivi kwanini habari za huyu John Billy Tendwa hazipatikaniki? Inakuwaje mtu mkubwa, muhimu kama yeye tunakosa historia na wasifu wake?

Yaani hata shule na vyuo alivyosoma hakuna?
 
John tendwa mi nimewahi kusikia ni mhehe,halafu nikasikia ni mngoni.......
Mkuu, kwa uhakika kabisa huyu Bwana ni mpare. Kuna mdogo wake wa kuzaliwa tumbo nafahamiana naye. Ni mpare wa kutokea Same. Ila CV yake kwa kweli sina, labda nijaribu kumdodosa huyu jamaa. Na kwa bahati mbaya huyu bwana mdogo na kaka yake hawaivi kabisa.
 
Inv,

Kabla ya kumuangalia Tendwa hebu tujiulize kiti alichokalia kina masharti/wasifu gani? Kama kweli ni mwanasheria kama anavyojigamba, kumbe elimu yetu ilishakufa siku nyingi, maana amejisahau.

Kama aliteuliwa na Mkapa bado nahitaji kuchunguza ila kama angekuwa chaguo la JK.... lol
 
Wakuu mnaonaje tusijadili kabila la mtu ila elimu na utendaji wake? Au kwa sababu ni sehemu ya CV?
 
Ni Jaji John Billy Tendwa... ni wakili vile vile.. mwanzoni alijaribu kuwa impartial lakini baada ya kufokewa kama mtoto mdogo na Mapuri kufuatia angalizo lake kwa CCM alinywea na kujikuta amerudishwa kwenye mstari. Kuanzia wakati huo kile CCM inataka CCM inapata..naam na ziada.
 
Hivi kweli kuna mliotegemea impartiality kutoka kwa mtu aliyeteuliwa na raisi wa CCM? Puhliiiiiiiz....hata SCOTUS haiko impartial....sembuse wateule wa raisi wa kutoka CCM?
 
Rekodi za maamuzi yake ya kijaji na pamoja na shughuli zake za kiwakili bado vipo?

Kuwa jaji peke yake ama kuwa wakili haina maana hakuwa corrupt, kwasababu sifa kuu Tanzania kwa viongozi ni how much of a better corrupt leader you are, especially kwenye positions za kulindana, ntashangazwa sana kama serikali inaongozwa kifisadi halafu eti wateuwe majaji waadilifu kwenye nafasi zinahusihsa na maslahi yao ya kuendelea kubaki madarakani...Thubutu!

Ni sawa kujifunga kitanzi mwenyewe kwasababu wanajuwa hawana uadilifu na lazima waweke "watu wao", MKJJ, huo mstari unaodai Tendwa alikuwepo mwanzoni ni upi? Ama ni alipokubali kufanya uhakiki? Hata hilo la kukubali kufanya uhakiki unadhani ma-handlers wake hawakujua outcome?
 
HApA NDIO UMUHIMU WA SAUTI YA UMEME, FMEs' aka MZEE WA NYETI UNAPOONEKANA, HII KITU INGESHUSHWA SASA HIVI, MKUU YUKO WAPI SIKU HIZI
 
HApA NDIO UMUHIMU WA SAUTI YA UMEME, FMEs' aka MZEE WA NYETI UNAPOONEKANA, HII KITU INGESHUSHWA SASA HIVI, MKUU YUKO WAPI SIKU HIZI

Labda aje na yeye aanzishe yenye kumhusu Mkurugenzi mkuu wa tume ya uchaguzi,bni muhimu tuanze sasa kabla hayajatukuta huko mbeleni.
 
Back
Top Bottom