Habari za weekend mkuu, thanks kwa mchango wako.
Naona kuna ideology mbalimbali ulizonazo kuhusiana na Evolution. Inakuwa ni ngumu sana kuweza kuendana nawe pamoja katika mjadala.
Katika maisha yangu sijawahi kufundishwa uhusiana kati ya Evolution na Big Bang au Cosmic Evolution. Maana nimesoma evolution as Evolution katika core yake.
PIa theory ya evolution haina mahusuano na dating ila inatumia dating kufanya comparisons sometimes. Datings hiyo ni part nyingine kabisa na errors zake sio errors za Evolution. Hizo errors zinaweza kutokea, ndio maana kuna absolute na relative datings.
Pia evolution haina uhusiano na Kuelezea origin of life. Evolution sio theory ya origin of life, bali ni theory inayoelezea origin of species. Nampa sana points Darwin kwa kuita kazi yake "Origin of Species" lakini wapinzani ndio wanaosema amezungumzia origin of life na kuanza kumpinga bila kusoma kazi yake.
Ninaomba kama tutajadiliana tujadiliane bila Mythologies Na conspiracies. Tujadili kama wasomi na nina imani una uelewa mzuri sana na utanisaidia.
Tuanze mwanzo ili kuondoa elimu isiyokwepo na tuelimishane vyema.
What is the theory of evolution.
Ni paradigm inayotazama historia ya viumbe katika dunia kutoka katika mageuzi yanayofanyika taratibu na kupelekea kutokea kwa aina nyingine ya kiumbe.
(Nimetumia kitabu cha Johnson M, 1999: Archaeological Theory: An Inteoduction. Oxford.)
Mpaka hapo katika simple definition, unakubali kuwa kuna mageuzi yanayofanyika taratibu katika viumbe?