Kuhani,
Kwa muda mrefu Makatibu wakuu wa Kiongozi wanajiona kuwa wao ni next baada ya rais. Hili sasa limekuwa ni kama tatizo la kurithishana. Mara nyingi Katibu Kiongozi hufanya maamuzi au kutoa maelekezo yaliyo nje ya kazi zake. Nakumbuka mzozo kati ya Waziri wa Mambo ya Ndani (Mrema) na CS (Rupia) juu ya kupatiwa hatia ya ukazi daraja 'A' kwa Chavda. CS Rupia ndiye aliyekuwa key player katika suala la kumbeba Chavda kupitia watendaji wa Wizara ya Mambo ya Ndani. Hali ilikwenda na kuwa mbaya kiasi cha Kumfanya Mrema aonekane kama Waziri boya huku mambo yakipita baina ya CS na PS wa mambo ya ndani. Nadiriki kusema kuwa Masha amejaribu walau kutumia wakati huu kubainisha mapungufu yaliyopo katika utendaji ndani serikali.
Katika hili CS ninahisi ndiyo key player kwani yeye ndiye mhimili mkubwa wa ajira za wale wote waliopo katika tender committe. Umafia ulikuwa unaendelea na huenda Masha alikwishaugundua na hakusita kuweka mambo katika macho ya watu. Sidhani sana kama katika hali hii Masha atapenda akubali kuendelea kuitwa waziri wa Mambo ya Ndani 'jina' asiyeweza kulinda na kutetea maslahi ya taifa na hasa akiwa ndiye Waziri Mwenye dhamana.
Pundamilia,
Kwa hiyo ndugu yangu unanambia hizi power grab kati ya Chief Secretary, the Minister, and Principal Secretary hazikuanza leo wala jana? Of course!
Utaratibu wa kazi ya Katibu Mkuu Kiongozi uko fuzzy. On the one hand kuna wachangiaji wengine wanasema siku zote makatibu wakuu walikuwa "wanafunikwa" na mawaziri waliozoea vibaya. On the other, you have this Masha situation ambapo Waziri ndio anakataa "kufunikwa," anaangalia kazi yake kama ni dhamana ya mwisho juu ya kazi zote za Wizara, anajaribu ku push back against this backdoor paper dealing between the secretaries at Ikulu and one right under his nose. Sasa sidhani kama tunaweza kusema kwa uhakika nani kamuingilia mwenzake, lakini suffice is to say that hii itifaki ina mushkeli na inachanganya wengi.
Katibu Mkuu Kiongozi, inadaiwa, ni mkuu, ni bosi, wa watumishi wa Umma. Definition za "mtumishi wa umma" zimetolewa nyingi humu. Moja imesema ni wote ambao sio "political appointees" au wabunge. Kwa nadharia hiyo, Mkuu wa Majeshi ya ulinzi, ambae sio mwanasiasa, sio Mbunge, na yeye bosi wake ni Chief Secretary! Au kuna exception kwamba mwanajeshi sio mtumishi wa umma? Na Mkuu wa TISS je? Au ma-spy nao wako exempted from this model? Jaji Mkuu nae anaripoti kwa Chief Secretary? Au the judiciary iko excepted? I mean, at some point you gonna have to say somebody come up with a newer definition of Mtumishi wa Umma, cause this just ain't working, it's got too many exceptions, don't ya think? Ungependa kusikia defition yangu ya "Mtumishi wa Umma"? Mtu yeyote anaepokea paycheck ya serikali ni mtumishi wa umma. Every last one of them! Which makes Chief Secretary the boss of everybody! Outta whack, ain't it? Ndo maana nasema Luhanjo si bosi wa mtu!
Nadhani Masha ameeleza vizuri sana role ya Chief Secretary:
"Ninatambua kwamba Katibu Mkuu Kiongozi anayo mamlaka na madaraka makubwa ya kuingilia maamuzi ndani ya Wizara yoyote pale anapoona maagizo ya Baraza la Mawaziri hayatekelezwi."
Kwangu mimi hapo maana yake huyu Chief Secretary anaweza kuingilia chochote kile kinachofanywa na yeyote yule, katika wakati wowote ule akifuatilia maagizo ya Barazala la Mawaziri. Including ya Waziri. Lakini hii haimaanishi ni bosi wa Waziri au Katibu Mkuu. Ila,
"...ingefaa Waziri ahusishwe kwa kuwa mwisho wa siku mimi ndiye nitakaewajibika kwa maamuzi yoyote ambayo yatafanyika Wizarani kwangu pasipokujali kwamba maamuzi hayo yalipata baraka za Katibu Mkuu Kiongozi au hapana."
Waziri anasema Katibu Mkuu Kiongozi hawezi akamvuta chemba Katibu wa Wizara. Wizara ni lazima iwe ukurasa mmoja katika kutekeleza maagizo ya kuingiliwa na Katibu Mkuu Kiongozi. Mkuu wa Utumishi wa Umma sio Mkuu wa watumishi wa umma. Tusichanganye.
Nadhani Waziri Masha hakukosea kukataa kufanywa second banana wa Katibu Mkuu Kiongozi, Luhanjo.