Waziri Masha na Kashfa ya Vitambulisho

Waziri Masha na Kashfa ya Vitambulisho

Kamati ya Bunge imeshindwa kujua la kufanya na Spika ameamuru kuwa watulie na hakuna kufanya lolote hadi j3, hizi ni taarifa za ndani.
 
Kamati ya Bunge imeshindwa kujua la kufanya na Spika ameamuru kuwa watulie na hakuna kufanya lolote hadi j3, hizi ni taarifa za ndani.

Huyu Spika ni mbabe sana hawajui la kufanya......this is very low I can not take it.....
 
Nadhani hapa katibu mkuu wa Waziri alikosa, huwezi kumzunguka boss wako. Kitendo cha Katibu mkuu wa waziri Masha kupata maelekezo kutoka kwa Katibu Mkuu kiongozi bila ya Masha kujua, ni sawa na kumzunguka.

Huyo Katibu Mkuu wa Waziri Masha anatakiwa ajieleze inakuwaje anawasiliana na Katibu Mkuu Kiongozi pasipo Waziri kuhusishwa? Na inakuwaje Katibu Mkuu Kiongozi amsikilize Katibu Mkuu wa Wizara bila kuhoji kama Waziri husika alikuwa awareness.

Something is wrong somewhere.

Thank you! Thank you!

So far naona kweli unastahili kujiita "special relativity."

Sikia Mkuu. Hiki kitu "Katibu ndio Mtendaji Mkuu" kinachanganya wengi, wengi sana. Ndio maana mwenyekiti mpya wa Umoja wa Wanawake anadiriki kusema "niko napanga jinsi ya kumsaidia Katibu kuendesha chama chetu."

Noooooo! Mwenyekiti/Waziri au Mkuu yeyote wa Idara hauwezi kusema utendaji ukuu ni wa Katibu Mkuu basi uweke miguu juu usiongoze wala usisimamie kazi wizara/chama/idara. No way Jose! Sehemu ya Waziri au Mwenyekiti kusimamia na kuongoza idara/chama chechote kile ni kujua what is happening under his nose at any given second!

Masha akimuuliza Katibu, hapa nini kinaendelea katika suala X, Y, Z katibu Mkuu hawezi kumwambia Masha "mimi bosi wangu yuko Ikulu...haya wewe hayakuhusu." Atakuwa amekataa "kufunikwa," kama alivyosema Fundi Mchundo, lakini mfumo huu utakuwa vurugu!
Na Luhanjo nae, kama ulivyosema Uwiano, hatakiwi ku get in between the Principal sectretary and his Minister! That's another flaw there.

Ndio maana Masha amekataa huu upuuzi, kwamba mambo ya wizara yake yaingiliwe na wakubwa wengine wa Ikulu wakati yamewekwa chini ya wizara yake. Kaona huu mradi ukiwa screw up wananchi hawatakuwa na muda wa kusoma Government Procurement Act kutafuta mchawi. Mambo ya wizara ya Mambo ya Ndani mwisho wa siku anaulizwa Masha!

Kama kweli habari alizoleta huyu Kinvaba ni za kweli, basi aidha Luhanjo ndio anaoneka alitaka kuingilia hapa, maana na yeye hatakiwi kuwemo katika mchakato. Au nawezekana Masha alitaka kufanya ufisadi, ndio, lakini naona mfumo wenyewe ovyo. Hata mimi nisingekubali upuuzi wa kupewa mzigo, sifa na lawama za uwaziri halafu wajuba wengine ndio wanaamua mambo ya wizara.
 
Last edited:
]
Wakuu hapa kazi ipo, mimi nimeona matatizo yafuatayo:-

1) uandishi wa barua siyo makini kabisa. Mhe. ni msomi (Masters holder) tena mwanasheria aliyebobea, inakuwaje aandike barua shallow hivyo! 60% ya barua ni malalamiko kutoka sagem, nilitegemea kuona kiambatanisho A, kiwe malalamiko ya sagem.

Huyo ndo waziri kijana na msomi.
Hata mwanafunzi wa kidato cha 6 hawezi akaaandika namna hii.
 
Mkuu Invisible
Many thanks. Naona nitakuwa very busy this wkend!! duh..!!
 
Msije mkashangaa mjomba bado anamuacha tuu katika hicho kiti na aendelaa kuboronga na kumuaibisha....mjomba anaangalia sana maslahi ya masela wake
 
Msije mkashangaa mjomba bado anamuacha tuu katika hicho kiti na aendelaa kuboronga na kumuaibisha....mjomba anaangalia sana maslahi ya masela wake

Masha hapa kosa lake nini? hebu tuambizane kwa mapana jamani. Katika hiyo barua, Masha kafanya nini kinachoonyesha kuwa yuko guilty? After all bado details zinahitajika hapa, hao Sagem walijuaje kama wameenguliwa kwenye mchakato? Nani anajua hili?

Kuna nini kimefichwa kati ya Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani na Katibu Mkuu Kiongozi? Kwa nini wanafanya mambo bila kumjulisha Waziri wa Mambo ya ndani? Wamemwona, mtoto sana hivyo hawezi kuwaelekeza wazee wenye uzoefu au wanataka kumwangusha Masha kisiasa?

Hao makatibu wote wawili wamemdharau waziri Masha na wanapaswa kuwajibika/shwa regardless Masha ni Fisadi, mtoto au hawezi kazi!
 
Last edited by a moderator:
Wakuu hoja ipo kwenye kamati ya ubunge mambo ya nje,ulinzi na usalama, kinachotakiwa kama waziri mkuu alivyosema DR.slaa angesubiri mchakato umalizike hapo pangekuwa patamu na ingekuwa kazi rahisi kumuhukumu muhusika halisi.

na kama Mh.DR.Slaa anataka skata la ID Lishughulikiwa basi Mh.Spika alipendekeza alipeleka hoja Binafsi ndani ya ubunge na taratibu za bunge zifuztavyo kushughulikia suala hili na atakaye patikana na hatia atajulikana ,hatua zaidi za kimaadili kama kanuni za bunge zinvyoelekeza zitafuatwa na muhusika akiona vipi basi mapema anasimama na kufanya ya akina msabaha na karamagi.

napenda kusisitiza nchi yetu inafuata na kutekeleza kwa umakini mkubwa utawala wa sheria,naamini serikali ya awamu ya nne iko makini na hujumu zozote zitakazotabanaishwa kwenye mchakato wa tenda ya National ID BASI wahusika wote sheria itachukuwa mkondo wake bila kujali rangi,cheo ubabe ulionao n.k
 
..............hiyo barua kaandikiwa na SAGEM....au kaandika under BIG influence ya SAGEM........no....doubt about it.....

Inaelekea Kuna mtu ndani ya kamati...........for some reasons alivujisha siri za kikao.......akitegemea ataisaidia SAGEM....

...Masha hakuwa na sababu ya kulalamika........baada ya kupata malalamiko toka SAGEM alitakiwa awashauri...wapeleke malalamiko yao kufuata taratibu zinazohusika........period.......

....kuhusu CS kumuandikia barua PS.....ni jambo la kawaida......afterall......at the end of the day ni waziri ndie atakayeiwakilisha hiyo cabinet paper...........kwa hiyo hakuna kuzungukwa hapo.......

NOW the CONCLUSION..........

....Lawrence MASHA HAS TO GO
 
Mbona wengine kwetu haifunguki? wee mtu usiyeonekana lete hicho kitu kwa njia nyingine basi

...pole sana! mtumie nauli mapema ili apande "ndege ya ATCL" na "Kitambulisho" cha uraia ili aweze kupita mpakani bila usumbufu akiwa na mfuko wake wa rambo kukuletea makabrasha haya kabla kibanda chake hakijakatiwa umeme wa "Richmond" na "Kiwira" kutokana na kutizama sana "GTV" inayoonesha mchelemchele tu kwa sasahivi!
 
Masha hapa kosa lake nini? hebu tuambizane kwa mapana jamani. Katika hiyo barua, Masha kafanya nini kinachoonyesha kuwa yuko guilty? After all bado details zinahitajika hapa, hao Sagem walijuaje kama wameenguliwa kwenye mchakato? Nani anajua hili?

Kuna nini kimefichwa kati ya Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani na Waziri Mkuu Kiongozi? Kwa nini wanafanya mambo bila kujulisha Waziri wa Mambo ya ndani? Wamemwona, mtoto sana hivyo hawezi kuwaelekeza wazee wenye uzoefu au wanataka kumwangusha Masha kisiasa.

Hao makatibu wote wawili wamemdharau waziri Masha na wanapaswa kuwajibika/shwa regardless Masha ni Fisadi, mtoto au hawezi kazi!

....why single out SAGEM.......angefanya research ya makampuni mengine yaliyoondolewa pia, ............na kuona sababu ni zipi ili kujua pia kama ilikuwa ni fair treated au lah..........otherwise ame-fall into trap ya SAGEM kumlalamikia yeye.........no doubt ile barua sehemu kubwa imeandikiwa na SAGEM...........

......kwa kumbukumbu zangu za haraka document ya Joint Venture Paper pekee........kama haipo.....inatosha kabisa kufanya Bid document yako kuwa Non Responsive........hakuna mjadala hapo...........

...hivi kweli wewe umeisoma hiyo barua......je umeona ile sehemu Waziri alipo-acknowledge mawasiliano kati ya CS na PS.......hakuna tatizo......
 
Masuala ya Tender Evaluation ni Strictly Confidential. Sasa hawa walipataje inside info za Evaluation Report kuwa wameenguliwa??? Kuna utata hapa!!! Ni lazima kijana aende na Maji. Hivyo ni kufanya mambo kienyeji. Awajibishwe au ajiwajibishe.
 
Kwa lipi? hebu wekeni maneno sawa......nataka nijue

Watu bwana, yaani kwa vile kuna thread nyingi hapa zinasema Masha fisadi, basi na hapa wameng'ang'ana Masha has to go bila kuwa na sababu which is clearly stated.

Hiyo barua haimweki Masha kwenye hatia, na kama kuna hatia basi kuna mawili, either Masha has to Go or hao Makatibu wakuu wawili. What if Katibu Mkuu ndio ali-leak-isha info kwa Sagem? if not what prevailed had Sagem wakalalamika? hili hakuna mtu anayetaka kuliongelea.

....kuhusu CS kumuandikia barua PS.....ni jambo la kawaida......afterall......at the end of the day ni waziri ndie atakayeiwakilisha hiyo cabinet paper...........kwa hiyo hakuna kuzungukwa hapo.......

NOW the CONCLUSION..........

....Lawrence MASHA HAS TO GO

Kwa hiyo Masha angesubiri tu taarifa akaisome bungeni, hajui background; then akiulizwa maswali ajibu nini? If that is the system it is more than rotten, bogus and no wonder mambo yanakwenda ndivyo sivyo kila leo.

Kama hamtakubali kubadili hilo lisystem lenu la uongozi, mtaendelea kulia sana...na endeleeni kuendesha nchi kwa mazoea na sio kufuata taratibu.

Hapa hypothesis nyingine inakuwa derived kuwa huko kwenye system kuna cold war between wazee waliozoea kuendesha nchi kwa uzoefu na vijana 'labda' wanaotaka kuendesha nchi kwa kufuata organisational ranks na taratibu.

Sielewi bado bwana Ogah, inakuwaje Katibu Mkuu apeleke taarifa kwa Katibu Mkuu Kiongozi, na Katibu Mkuu Kiongozi atoe rulling on the way forward bila kushauriana na Waziri husika?


Sikatai kwamba Masha has to go, but there is a need to know he has to go on which grounds.
 
Last edited by a moderator:
Masha hapa kosa lake nini? hebu tuambizane kwa mapana jamani. Katika hiyo barua, Masha kafanya nini kinachoonyesha kuwa yuko guilty? After all bado details zinahitajika hapa, hao Sagem walijuaje kama wameenguliwa kwenye mchakato? Nani anajua hili?
Don't tell me hujaona kosa? Mkuu hivi kosa unataka liweje? Masha anataka makampuni yaliyoondolewa kwa kukosa kukidhi vigezo yarudishwe! Wakati huo huo anakiri kuwa hana uwezo wa kuiingilia Bodi ya zabuni. Pia anasema KM wake ameridhika na uamuzi wa Bodi ila yeye hakubali. Ndo maana Katibu Mkuu Kiongozi aliagiza iandikwe taarifa ili Masha awasilishe cabinet.

Maybe bado huta ona kosa, ila ikweli ndo huo.

Kuna nini kimefichwa kati ya Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani na Katibu Mkuu Kiongozi? Kwa nini wanafanya mambo bila kumjulisha Waziri wa Mambo ya ndani? Wamemwona, mtoto sana hivyo hawezi kuwaelekeza wazee wenye uzoefu au wanataka kumwangusha Masha kisiasa?
Hakuna kinachofichwa, Katibu Mkuu Kiongozi alimwangiza Katibu Mkuu mambo ya ndani aandike cabinet paper ambayo Waziri ataiwasilisha. Sasa kuzungukwa gani unakosema? CS ana mamlaka ya kuwaagiza PS wote, na hilo Masha amelikiri katika barua yake kwa PM. Ulitaka CS amwagize Waziri? thats impossible. CS alitaka kuleta suluhusho kati ya maamuzi ya bodi na Masha. Kumbuka bodi ilistick katika uamuzi wake na Waziri Masha naye alistick kwenye maamuzi yake. Namna ya kuondoa hiyo deadlock ilikuwa ni cabinet paper!

Hao makatibu wote wawili wamemdharau waziri Masha na wanapaswa kuwajibika/shwa regardless Masha ni Fisadi, mtoto au hawezi kazi!
Wamemdharau kivipi? PS wa mambo ya ndani alitekeleza maagizo ya Masha kwa kuiandikia bodi. Alipopata majibu ya bodi alimjulisha Waziri, pia akamweleza kuwa yeye ameridhika na maamuzi ya bodi. Wakati huo huo Masha akaendelea na msimamo wake. Hivyo PS akalazimika kumweleza Bossi wake yaani CS. CS akamwagiza aandike cabinet paper, ampe Masha ili aiwasilishe cabinet. sasa dharau ipi?
 
Back
Top Bottom