Katika hali isiyo ya kawaida, Mwanadada anayejulikana katika Mitandao ya Kijamii, Mange Kimambi, amewachana January Makamba na Mwamvita katika Instagram page yake kwa kuweka sauti zilizorekodiwa wakipanga deal na mfanyabiashara wa kiitaliano ambaye amelizwa dola milion 100 ili apewe deal la kujenga port Bagamaoyo.
Jaribu kupitia..
(Mazungumzo ya Sauti yameambatanishwa)
WAONAVYO ACT Wazalendo KUHUSU SAKATA LA JANUARI MAKAMBA...............................
Tusiingie kwenye ugomvi usiotuhusu.
January alikuwa mwana mkakati wa Chama cha Mapinduzi kuhakikisha Magufuli anashinda Urais.
Vivyo hivyo walikuwepo wana mkakati wa Edward Lowassa kuhakikisha Lowassa anashinda uchaguzi...
January anatuhumiwa kusababisha wanamkakati wa Lowassa waliokuwa wamejifungia hotelini kukamatwa kwa tuhuma za makosa ya Mtandao(kwamba walikuwa wana hack Mtandao wa tume Nec na kuhariri matokeo yaliyotumwa toka majimboni)
January akaaminika kuwa ndiye aliemnyima ushindi Lowassa baada ya kuwachomekea .
Vita ikaatangazwa rasmi,hakuna jema lolote litakalofanywa na January likakubaliwa au kupongezwa na wafuasi wa Lowassa, wakafanya kila liwezekanalo ili na January aukose uwaziri kama walivyoukosa Urais
Rais Magufuli akamteua January kwa kuzingatia vigezo alivyoona vinamfaa,sasa Wanamkakati wa Lowassa wanaendeleza vita kuhakikisha January anapotea kisiasa ili kulipiza kisasi.
Tanzania ya visasi itaua vipaji vya vijana wanaochipukia kusiasa,siungi mkono siasa na visasi bali mimi ni muumini wa siasa za kusamehe na kushughulikia maswala.
Magufuli hakosoleki mpaka mkose mtaji wa kiasa? Mbona watoto bado wanakaa chini shuleni? Mbona umeme unakatika kila siku tena bila taarifa? Mbona wananchi wengi wanazidi kuwa maskini pamoja na kuwa tunaambiwa makusanyo ni zaidi tril 1.7 kwa mwezi?
Mbona bei ya mafuta imeshuka lkn nauli usafuri wa magari ipo palepale?
Yapo maswala mengi na makubwa yakufanywa kuwa ajenda kuliko kupoteza muda kujadili Mapenzi ya Mwavita na Muitalia wake au January na shemeji yake.
Let base on issues rather than parsonality.