Waziri Abdallah Ulega: Nilishindwa kupinga maamuzi ya Luhaga Mpina kupima samaki kwa rula kwenye migahawa

Chachu Ombara

JF-Expert Member
Dec 11, 2012
5,897
10,358
Naona Wabunge na Mawaziri kutoka chama cha mapinduzi bado wanapeleka moto kwa Luhaga Mpina baada ya kuonesha kuwa-challenge kwenye masuala mbalimbali.

Akichangia Bungeni, Waziri wa Mifugo na Uvuvi ametupa dongo kwa Boss wake wa zamani kwenye Wizara hiyo kuwa hakutumia busara kupima samaki ambao washapikwa.

---

Waziri wa Mifugo na Uvuvi Abdallah Ulega amesema alishindwa kupinga maamuzi ya aliyekuwa Boss wake Luhaga Mpina baada ya Viongozi wa Wizara hiyo kwenda kupima kwa rula samaki waliopikwa kwenye mgahawa wa Bunge.

Ulega amesema hayo wakati akijibu hoja ya Mpina aliyoiibua Bungeni wakati akichangia mjadala wa Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Mifugo na Uvuvi ambapo alimtaka Waziri aeleze kanuni iliyotumika kutekeleza zoezi hilo.

“Wakati mwingine tunakaa kimya maana kukaa kimya nayo ni busara, samaki akishapikwa anapoteza shape anapoteza size sayansi ya samaki haielekei huko , samaki yule aliyepimwa na Boss wangu wa zamani (Mpina) Mheshimiwa alikuwa amekaangwa kapita katika nyuzijoto nyingi sana alipoteza uhalisia sasa alitaka wakati ule nimwambie Mzee unakosea hapa”




Pia soma
 
Sayansi Ya Siasa Inaambatana Na Mambo Kadhaa Wa Kadhaa
Fitna , Husda, Ndumilakuwili, Kujipendekeza, Kijino Pembe, Chawa
Kuhakikisha Unalinda Mkate, Kitumbua Chako Kisiingie Mchanga Muda Mpaka Ufikie Tonge La Mwisho La Kukombea Mboga Zote Kwenye Bakuri Lako!!!!
 
Ulega muoga, na kwa mawazo yake hayo ni kama nae anamwambia naibu wake awe anakaa kimya bosi akifanya mambo yake, anaendeleza tabia za kikondoo kwa viongozi wa serikali, bila shaka hata akiona Samia anakosea bado atakaa kimya.
Hii jamii ya watanga huwa wanafiki sana,uswahili mwingi,kamfukuzisha kazi Mashimba Ndaki wakati yeye ni mweupe balaa
 
Hii jamii ya watanga huwa wanafiki sana,uswahili mwingi,kamfukuzisha kazi Mashimba Ndaki wakati yeye ni mweupe balaa
Nidhamu Ya Dhati
Nidhamu Ya Kujipendekeza
Nidhamu Ya Woga



Hapo Juu Ni Aina Tofauti Za Nidhamu
Ulega Awekwe Sehemu Yake
 
Kuna wakati unaweza fanya jambo fulani ili kuwashtua wengine. Huwa inasaidia pia.

Lakini samaki kama amevuliwa kwa viwango vile vile bado unaweza kujua kama alikuwa sawa au si sawa baada ya kuvuliwa.

Kwenye viwanja vya ndege huwa kuna watu wa TAWA kuhakikisha ngozi za wanyama kama simba waliowindwa walifikia umri wa kuwindwa. Japo ngozi imekauka ila askari ana uwezi wa kujua kama alikidhi vigezo vya kuwindwa kwa kuona hiyo ngozi.
 
Naona Wabunge na Mawaziri kutoka chama cha mapinduzi bado wanapeleka moto kwa Luhaga Mpina baada ya kuonesha kuwa-challenge kwenye masuala mbalimbali.

Akichangia Bungeni, Waziri wa Mifugo na Uvuvi ametupa dongo kwa Boss wake wa zamani kwenye Wizara hiyo kuwa hakutumia busara kupima samaki ambao washapikwa.

---

Waziri wa Mifugo na Uvuvi Abdallah Ulega amesema alishindwa kupinga maamuzi ya aliyekuwa Boss wake Luhaga Mpina baada ya Viongozi wa Wizara hiyo kwenda kupima kwa rula samaki waliopikwa kwenye mgahawa wa Bunge.

Ulega amesema hayo wakati akijibu hoja ya Mpina aliyoiibua Bungeni wakati akichangia mjadala wa Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Mifugo na Uvuvi ambapo alimtaka Waziri aeleze kanuni iliyotumika kutekeleza zoezi hilo.

“Wakati mwingine tunakaa kimya maana kukaa kimya nayo ni busara, samaki akishapikwa anapoteza shape anapoteza size sayansi ya samaki haielekei huko , samaki yule aliyepimwa na Boss wangu wa zamani (Mpina) Mheshimiwa alikuwa amekaangwa kapita katika nyuzijoto nyingi sana alipoteza uhalisia sasa alitaka wakati ule nimwambie Mzee unakosea hapa”


View attachment 2609416

Pia soma
Yaani samaki kapakuliwa kwenye sahani tayari kwa kuliwa eti anapimwa na rula. Kwa hili nchi ilitia aibu.
 
Kama alikuwa anaogopa kumwambia ukweli bosi wake basi hafai kuwa kiongozi kabisa.kwa nchi zinazojielewa angeachishwa hiyo nafasi.Hii ameonesha hata kwa sasa atakuwa hana maamuzi ktk wizara yake kwa kumhofia rais.
 
Na bado,yani mtageukana mpaka basi.MIE NATAMANI MPIGANE MAKONDE Kwanza hapo mjengoni ndio tujue nani ni mzdlendo.kwa sasa wananchi wa kawaida tumeshawajuwa viongozi wetu mna "ndimimbili"ktk kila mambo muhimu kwa mustakabali wa nchi yetu.ukitulia na ukawa na kumbukumbu za kauli za kichawachawa za viongozi walewale ambao ndio hawahawa '-rejea awamu ya 5 na ya sita-' utaelewa kuwa tanzania haijapata uongozi bora,ila tuna bora viongozi wafuata upepo kwa manufaa ya mavmbo yao na vizazi vyao wala si kwa ajili yetu wadanganyika.
 
Anahofia kutokuwepo hapo? Au anahofia kutofanya maamuzi sahihi na kushauri kwa manufaa ya nchi na watu wake?
Excuse ya kipumbavu sana, kwa hiyo aliogopa kutoa ushauri kwa waziri kuogopa kuondolewa........hapa ndo unaona namna gani nchi imejaa manafiki. Sasa kama naibu waziri huna ujasiri wa kumshauri waziri jambo sahihi la kufanya, mtu wa kawaida itakuwaje?​
 
Back
Top Bottom