Wawasilisha Barua Ubalozi wa Ujerumani wakitaka walipwe fidia kutokana na Babu na Bibi zao kuteswa wakati wa Ukoloni.

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Apr 18, 2017
2,812
11,989

The United Kingdoms of Afrika (UKOA) kupitia kwa Dr. Moses Katega “Prince Katega II” Na Dr. Fadhili Emily Kabujanja “Mfalme Dr. Fadhili” wameandika barua na kuiwasilisha Ubalozi wa Ujerumani Nchini Tanzania wakidai kulipwa fidia kwa kilichotokea wakati wa Ukoloni.

Kupitia taarifa yao waliyoiwasilisha ‘public’ wameeleza kuwa wamechukua hatua hiyo kwa niaba ya Watanzania 700,000.

Barua yao kwenda kwa Shirikisho la Jamhuri ya Ujerumani, wamemtaarifu Balozi kuwa madhumuni yao ni kutaka kwenda katika Vyombo vya Kisheria kwa makosa uliyoyatenda wakati wa ukoloni, hivyo wanataka kufungua mashtaka ya kudai fidia.

Wameeleza kuwa Barua hiyo ni Notisi ya kutaka kufungua mashtaka ya kudai fidia kwa makosa ya mauaji ya halaiki ya watu wenye asili ya Kabila la Wamatumbi, Wapogoro, Wazaramo, Wangindo, Wanguni, Wangarambe na Makabila mengine katika Vita ya Majimaji (1905- 1907).

Soma barua kamili chini...

RAIS WA UJERUMANI ALICHOSEMA OKTOBA 2023
Oktoba 2023, Rais wa Shirikisho la Ujerumani, Dkt. Frank Walter Steinmeier alifanya ziara Nchini ikiwemo kukutana na mwenyeji wake, Rais Samia Sululu Hassan katika Ikulu Jijini Dar es Salaam na kuzungumzia kuhusu kumbukumbu ya Vita ya Majimaji iliyotokea Mwaka 1905 – 1907.

Kiongozi huyo alisema, “Ziara hii nimeiweka katika kuangalia yale yaliyotokea wakati wa Ukoloni na pia kuonana na waathiriwa wa Vita ya Majimaji, kuzungumza na wahanga wa vita hiyo, najua walipitia kipindi kigumu ambacho si cha kupendeza, nitakayozungumza nayo nitayafikisha Ujerumani na ikiwezekana kuangalia namna ya kurusisha mabaki ya watu waliopigana vita.”

1_4_page-0001.jpg

1_4_page-0002.jpg

1_4_page-0003.jpg

1_4_page-0004.jpg

1_4_page-0005.jpg

Tafsiri ya Barua hiyo upande wa Lugha ya Kingereza

M1_5_page-0001.jpg

M1_5_page-0002.jpg

M1_5_page-0003.jpg

M1_5_page-0004.jpg

M1_5_page-0005.jpg
 
hawa wako sawa, nawaunga mkono kabisa katika hili..

Serikali inapaswa pia kuifungulia mashitaka serikali ya ujerumani kwakututawala na kutuharibia mifumo yetu ya maisha ambayo tulikuwa nayo na kama tungeachwa basi leo hii tungekuwa mbali sana kiuchumi, kifikra nk.

Serikali inapaswa kuwafungulia mashitaka Waingereza pia kwa kututawala na kutusababishia madhira makubwa ikiwemo kuua watu wetu, kutesa watu wetu, kuharibu utamaduni wetu nk.

Tunapaswa pia kuwafungulia mashitaka waarabu wa Oman kwa kuuza ndugu zetu kama watumwa na kuharibu utu wetu, kuua watu wetu na kuharibu utamaduni wetu.

Fidia itakayopatikana ijenge vyuo vya ufundi na shule za kisasa maeneo yaliyoathirika sana na ukoloni pamoja na biashara ta utumwa.
Serikali husika zitoe scholarship za elimu ya juu kwa watu wetu kwenda kusoma kila mwaka, wasipungue wanafunzi 300 kila mwaka kwenye nchi husika.
 
Nzuri, ila inauwaje watu wenye PhD wanaandika L sehemu ya R? na Kiswahili kingine kidhaifu hivi?

Sina wasiwasi na Content.

Hivi wale Nama na Waherero wa Namibia wenyewe fidia yao ililipwa? nafikiri wao walianza hizi harakati zamani kidogo.
 
Nzuri, ila inauwaje watu wenye PhD wanaandika L sehemu ya R? na Kiswahili kingine kidhaifu hivi?

Sina wasiwasi na Content.

Hivi wale Nama na Waherero wa Namibia wenyewe fidia yao ililipwa? nafikiri wao walianza hizi harakati zamani kidogo.
Mkuu hata mm kuna baadhi ya maneno huwa nasahau niweke R au L
Japo ni maneno ambayo hayatumiki sana.

Hili tatizo kubwa sana.
 
Hawa ni wapumbafu, mateso tunayopitishwa na CCM ni makubwa kuliko hata ya wakoloni, pia wameshindwa hata kuandika barua kwa kiingereza? shame on them
 
Nzuri, ila inauwaje watu wenye PhD wanaandika L sehemu ya R? na Kiswahili kingine kidhaifu hivi?

Sina wasiwasi na Content.

Hivi wale Nama na Waherero wa Namibia wenyewe fidia yao ililipwa? nafikiri wao walianza hizi harakati zamani kidogo.
Yaani ni aibu sn haswa wanaCCM R&L zinawatesa sn
 
hawa wako sawa, nawaunga mkono kabisa katika hili..

Serikali inapaswa pia kuifungulia mashitaka serikali ya ujerumani kwakututawala na kutuharibia mifumo yetu ya maisha ambayo tulikuwa nayo na kama tungeachwa basi leo hii tungekuwa mbali sana kiuchumi, kifikra nk.

Serikali inapaswa kuwafungulia mashitaka Waingereza pia kwa kututawala na kutusababishia madhira makubwa ikiwemo kuua watu wetu, kutesa watu wetu, kuharibu utamaduni wetu nk.

Tunapaswa pia kuwafungulia mashitaka waarabu wa Oman kwa kuuza ndugu zetu kama watumwa na kuharibu utu wetu, kuua watu wetu na kuharibu utamaduni wetu.

Fidia itakayopatikana ijenge vyuo vya ufundi na shule za kisasa maeneo yaliyoathirika sana na ukoloni pamoja na biashara ta utumwa.
Serikali husika zitoe scholarship za elimu ya juu kwa watu wetu kwenda kusoma kila mwaka, wasipungue wanafunzi 300 kila mwaka kwenye nchi husika.
Tumeachwa miaka 62 nchi ni fukara, bora wajerumani wangeendelea kututawala mpka sasa tungekuwa mbali sn
 
Back
Top Bottom