JanguKamaJangu
JF-Expert Member
- Feb 7, 2022
- 2,308
- 5,460
Akitoa taarifa kwa waandishi wa habari Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mjini magharibi Unguja Kamishna Msaidizi wa Polisi ACP Abubakar Khamis Ally amesema kufuatia video iliyosambaa mitandaoni ikiwaonesha baadhi ya watu katika eneo la viwanja vya mnazi mmoja Zanzibar wakila hadharani wakati wa mchana wa Ramadhani, Jeshi hilo lilifanya msako na kuwakamata watu wapatao kumi na mbili wakiwa na vielelezo ambapo amesema wanaendelea na taratibu nyengine ili kuwafikisha Mahakamani.
Aidha ameyataja makosa mengine ni pamoja na unyang’anyi, Madawa ya kulevya na makosa mengine ambapo watuhumiwa wanashikiliwa na Polisi na wengine tayari wameshahukumiwa Mahakamani.
Pia soma:
- Yanayoendelea Zanzibar tusubiri majibu ya Wahanga na kuzaa gharika
- Kamishna Mkuu wa Jeshi la Polisi Zanzibar: Tulikamata wavuta bangi sio wanaokula mchana
- Zanzibar: Akutana na kipigo baada ya kuonekana akila mchana!
- Zanzibar: Serikali yalaani vitendo vya unyanyasaji wa kidini vinavyoendelea visiwani
- PEMBA: Achapwa Mikwaju Kula Mchana Mwezi mtukufu wa Ramadhan