Watanzania waliosoma Havard

Watanzania waliosoma Havard

mie nimesoma UDSM......B.Com. in Banking and Financial Services....

Sidhani kama yanihusu kivile..ila nimejikuta niko interested nayo
Ohooo kumbe udsm tena udbs alumni mwenzangu weye muke ya muzungu..masterz twende Havard mpnz
 
Rwegasira yuko wapi now?

Kikwete ni mtu wa kupita
sisi kama taifa tunaweza weka utaratibu wa kutambua 'vichwa' ili siku moja
tukipata serikali ya kweli,vitumike

Delphin Rwegasira sasa ni Profesa wa Kigoda (kipya) cha Mwalimu Nyerere cha masuala ya Maendeleo ya Uchumi pale UDSM
 
Mpaka September 2012, record inaonesha kuna alumni 85 kutoka nchi ya Tanzania🙁 (http://www.worldwide.harvard.edu/iws/pdf/International_Alumni_Breakdown_by_Country_2011.pdf)

Kenya wapo 183 na Uganda 47!

Inaweza kuwa kazi ngumu kupata majina yao.

Shukrani sana mkuu, nilikuwa sijaiona hii, imenisaidia kujibu maswali mengi niliyokuwa nayo kichwani - uchambuzi wangu mfupi huu hapo chini:

Watanzania:

Harvard Law School (HLS) = 22
Harvard School of Public Health (HSPH) = 21
Harvard Business School (HBS) = 17
Harvard College (COL) = 10
Harvard Graduate School of Education (HGSE) = 3
Graduate School of Arts and Sciences (GSAS) = 2
Graduate School of Design (GSD) = 0
Harvard Medical School (HMS) = 0

Tumesomesha wanasheria wengi zaidi na kwa kiasi kikubwa uwakili uko vizuri Tanzania, tatizo ni mifumo ya kisheria na wale majaji waliotajwa na mheshimiwa fulani.

Pengine kutokana na kuwepo kwa miradi ya afya ya Harvard nchini Tanzania ndio maana wamepokea wanafunzi wetu wengi (rejea posti yangu inayofuatia), na kwa sasa kuna miradi mingi ya afya ya jamii Tanzania, natumai inatusaidia.

Kundi la tatu lenye watu wengi ni waliosomea shule ya biashara ambapo kwa kawaida watu wanaenda hapo kusoma MBA, pengine ndio maana siku hizi uwekezaji, ujasiriamali na sekta ya mabenki inakua japo sina uhakika kama hawa wanatusaidia sana kama taifa.

Hiyo COL ndiyo inayotoa shahada ya kwanza, kwa kweli hapo vijana wetu ni wachache sana ukilinganisha na wa Nigeria, Kenya n.k.

Da, hapo kwenye elimu panajieleza penyewe ila kama HakiElimu imesaidia sekta hiyo nchini basi tukumbuke mwanzilishi wake ni mhitimu wa Harvard pia (nasikia na Mungai naye ni zao la chuo hiki).

Nashangaa hatuna hata msanifu majengo wale mtaalamu wa mipango miji aliyepitia GSD, ila hapo wana profesa huyu aliyetafiti Dar es Salaam katika tasnifu yake ya uzamivu: Harvard Graduate School of Design - Homepage

Pia nashangaa hatuna watu HMS japo tunao wengi HSPH, pamoja na hayo madaktari wetu kina Ulimboka wako vizuri tatizo ni vitendea kazi na mishahara/marupurupu.
 
Harvard ni jina kubwa tu kama Range Rover, Mercedes Benz, BMW, Porsche, Lexus au Cadillac. Mwisho wa siku, yote ni magari tu. Hata Toyota/KIA/Hyundai itakufikisha from point A to point B, and in most cases even more dependable ukilinganisha na magari yenye majina makubwa ambayo starting prices ni $100,000 kwenda juu.
 
Hata ukifanikiwa kupata elimu ya associate degree from one or another community college na ukafaulu vizuri, elimu hiyo should be able to get you a decent job kutegemea na fani uliyobobea: haijalishi kama ulisomea nursing assistant, software programming au commercial pilot. That's the whole point: getting from point A to point B.
 
Kwenye uhandisi kinachotisha sasa ni Caltech - rejea:
Caltech Named World's Top University in Times Higher Education Global Ranking | Caltech

"Caltech is a highly focused science and engineering research and education institution located in Pasadena, CA. It is home to approximately 2,300 students and 300 faculty, and boasts 31 Nobel laureates among its past and current faculty and alumni. Caltech manages the Jet Propulsion Laboratory (JPL) for NASA, and owns and operates a global network of astronomical observatories and research facilities" - California Institute of Technology - World University Rankings - 2013-14 - Times Higher Education

Mkuu Udadisi

MIT bado chuo bora duniani kwa sasa,soma hapa!
Best Undergraduate Engineering Programs | Rankings | US News

Au kwa nn usisomwe hapa chini?Kwa vyuo vyote duniani bado MIT ina shika namba moja duniani
http://www.topuniversities.com/univ...-subject-rankings/2013/engineering-mechanical
 
Mkuu Udadisi

MIT bado chuo bora duniani kwa sasa,soma hapa!
Best Undergraduate Engineering Programs | Rankings | US News

Au kwa nn usisomwe hapa chini?Kwa vyuo vyote duniani bado MIT ina shika namba moja duniani
QS World University Rankings by Subject 2013 - Engineering - Mechanical, Aeronautical & Manufacturing | Top Universities

Hivi kwenye kulinganisha/kupima vitu:

Redet na Synovate nani zaidi? Gallup na Pew nani zaidi? US News na Times Higher Education nani zaidi?
 
Thanks, jaribu mkuu u never now nawe unaweza kuwa kwenye bracket hiyo, sijui kwa Africa unaweza kufanya test kivipi? Ukimaliza test yao wanakueleza mambo mengi - kuanzia analytical mind yako inavyofanya kazi, Temperament yako, huko kwenye kundi gani la binadamu wenzako walio hai na walio tangulia mbele ya haki nk. Jaribu kama kuna uwezekano mkuu ujitambue.
 
Kwa mtazamo wangu hawa watu wamekwenda kusoma Havard au Stanford kwa manufaa yao binafsi isipokuwa kama walipelekwa na Serikali. Hivyo ni jukumu la serikali kutambua umuhimu wao na kuwashirikisha kwenye maswala yanayohusiana na nyanja zao.

Hivyo kutokujulikana au kutokutambulika kwao kunaonyesha jinsi gani serikali yetu ya Tanzania na watumishi wake walivyokuwa wabinafsi na wasio thamini michango ya wasomi katika kufikia maamuzi mbalimbali ya taifa hili.

Na ninaamini kabisa watumishi wa serikali wanatambua kabisa kuwa kwenye maamuzi fulani fulani ingekuwa vizuri kuwashikirikisha wasomi ilikupata mawazo huru yasiyo kuwa na ushawishi wa pande yoyote ile ili kuliletea taifa hili maendeleo.

Mwisho ningependa kusema pia, siyo wote wanaosoma Havard ni vichwa kuna wengine wanalipia kwa gharama yoyote ile ili wapate CHETI cha Havard. Maana kuna tofauti kati ya kuwa na cheti cha Havard na kuendeleza kipawa na ufahamu wa kitu ndani ya Havard.

Huu ni mfumo mbaya wa hichi chama cha ccm ulijijengea kuwa ambao siyo wana siasa awawezi shirikishwa kwenye kuijenga nchi yao matokeo yake wanakwenda kuwapa kazi watu kama akina chikawe, hawa ghasi, na mkuchika,na lukuvi
 
Waliosoma ktk vyuo vya ivy league waje nyumbani tupige mzigo ! ! kusomea huko cyo dili sana hutashindwa kujikomboa wewe na jamii inayokuzunguka! ! ! kusomea ktk ivy league na maendeleo ni different entities! Kwani mengi alisoma harvard? ?
 
Kuna Prof. Pastor Ntake Mtanzania mwenye uraia wa Canada kwa sasa hivi.
 
Waliosoma ktk vyuo vya ivy league waje nyumbani tupige mzigo ! ! kusomea huko cyo dili sana hutashindwa kujikomboa wewe na jamii inayokuzunguka! ! ! kusomea ktk ivy league na maendeleo ni different entities! Kwani mengi alisoma harvard? ?

Kuna jamaa kagraduate na MSc in Aerospace Engineering na anapiga box pale Lokheed Martin. Unamwambia arudi bongo wapi bongo ataitumia skills zake na nani atamatch $$$$$$$$ anazolipwa na Lokheed Martin?
 
Sumaye degree yake ni 'magumashi'
kuwa kwake PM ndio sababu kubwa alipata admission...
sidhani kama ange qualify kama angekuwa fresh from high school...

Hahahahahaha! Ana case studies nyingi wakati wa DISCUSSION🙂 Kwa hili sikubishii Mkuu....
 
So far nawajua wawili tu
Andrew Chenge, na Arnold Kileo...

kuna mtu anaweza ku list wengine ambao wamesoma chuo hiko maarufu
na wengi wanasema ndio the best in the world?
Mkuu The Boss, vipi unafukuzia admission Harvard? Sema ili kama kuna wenye madesa ya Harvard wakutumie🙂
 
Back
Top Bottom