Watanzania hii ndio sababu ya kwanini tuliandika katiba mpya, mnamchosha rais na kero zenu kwenye misafara yake

MK254

JF-Expert Member
May 11, 2013
31,649
48,411
Enzi za katiba ya zamani hapa kwetu ilikua hivi hivi kama tunavyoshuhudia kwa Watanzania, kwamba maskini wanyonge wanalaghaiwa na kunyanyaswa bila msaada wowote, hata wakifika kwa wakuu wa mikoa taswira inabaki ile ile, mpaka siku msafara wa rais utapita, kisha umpigie rais makelele hadi akuskie halafu unapewa mic uongee tatizo lako, hapo sasa ndio unakua umefika mwisho wa mateso yako maana ataamrisha suluhu.

Huwa natazama video za rais Magufuli, kweli ana nia ya dhati ya kutatua matatizo ya watu wake, lakini naona mzee wa watu ameanza kuchoka, siku za mwanzo mwanzo kwwenye hii misafara alikua anaskliza kesi za namna hii, lakini sasa hivi naona ameanza kuzichunia na inabidi mtu apige makelele sana ya kichizi kwenye hii mikutano ya kampeni ndio usklizwe.

Kwa hali ya hivi, maelfu na maelfu ya kero haziwezi kutatuliwa, lazima mtegemee katiba na sio kukaa mkisubiri misafara ya rais, mtamchosha sana.

 
share,

Waafrika tuache uzembe kwamba kila mmoja analala usiku, kunao tunapiga mzigo wa kazi usiku wote. Hili bara litaendelea kuwa maskini kwa ajili ya huu uzembe, lazima watu mchangamke na kuwa tayari kufanya kazi masaa 24/7
 
Waafrika tuache uzembe kwamba kila mmoja analala usiku, kunao tunapiga mzigo wa kazi usiku wote. Hili bara litaendelea kuwa maskini kwa ajili ya huu uzembe, lazima watu mchangamke na kuwa tayari kufanya kazi masaa 24/7

Curfew imeisha?!
 
  • Thanks
Reactions: Oii
Waafrika tuache uzembe kwamba kila mmoja analala usiku, kunao tunapiga mzigo wa kazi usiku wote. Hili bara litaendelea kuwa maskini kwa ajili ya huu uzembe, lazima watu mchangamke na kuwa tayari kufanya kazi masaa 24/7
Broh unamiliki bilioni ngapi?
 
Broh unamiliki bilioni ngapi?

Sihitaji mabilioni wala sizitaki (au unazungumza kuhusu bilioni za Kitz maana hizo ni rahisi kwa mtu kuzimiliki), cha msingi ni kupiga kazi ili tujitoe kwenye huu ukata uliotamalaki Afrika.

Taifa ndogo kama Sweden lenye watu wachache mno, milioni kumi ila lina uchumi unaoweza kuinunua EAC yote na iongeze humo Ethiopia, Somalia, Sudan zote mbili, DRC na bado ibaki na chenji.
 
Waafrika tuache uzembe kwamba kila mmoja analala usiku, kunao tunapiga mzigo wa kazi usiku wote. Hili bara litaendelea kuwa maskini kwa ajili ya huu uzembe, lazima watu mchangamke na kuwa tayari kufanya kazi masaa 24/7

Hujaelewa hoja. Ni lugha ya picha. Maana yake ni afadhali ungelala tu upumzishe akili sababu ulichoandika ni upupu.
 
Sihitaji mabilioni wala sizitaki (au unazungumza kuhusu bilioni za Kitz maana hizo ni rahisi kwa mtu kuzimiliki), cha msingi ni kupiga kazi ili tujitoe kwenye huu ukata uliotamalaki Afrika.

Taifa ndogo kama Sweden lenye watu wachache mno, milioni kumi ila lina uchumi unaoweza kuinunua EAC yote na iongeze humo Ethiopia, Somalia, Sudan zote mbili, DRC na bado ibaki na chenji.
Kama hauna mabilioni we nae kilaza tu et m nafanya kazi hadi usiku 🤣🤣🤣 takataka!! We sema ulishindwa kulala vile upo kwenye banda ya bati hapo Mathare. Jotooo
 
Sihitaji mabilioni wala sizitaki (au unazungumza kuhusu bilioni za Kitz maana hizo ni rahisi kwa mtu kuzimiliki), cha msingi ni kupiga kazi ili tujitoe kwenye huu ukata uliotamalaki Afrika.

Taifa ndogo kama Sweden lenye watu wachache mno, milioni kumi ila lina uchumi unaoweza kuinunua EAC yote na iongeze humo Ethiopia, Somalia, Sudan zote mbili, DRC na bado ibaki na chenji.

Hivi kuna nchi yenye uchumi wa kuinunua nchi nyingine?

Ilishatokea wapi nchi ikanunua nchi? Na akili zako zilivyo finyu unaweza kua unaongea hivi kwa kumaanisha GDP ya Sweden ni kubwa kuliko za hayo mataifa uliyoyataja bila kujua resources zilizopo kwenye hayo mataifa zina thamani mara trillion ya hicho kiGDP cha hiyo Sweden.
 
Ni kweli mkuu! Katiba mpya yenye mifumo imara ya kujitegemea ndio dira nzuri ya maendeleo.
Bahati mbaya sana viongozi kwa maksudi hawataki katiba mpya na wananchi walio wengi hawajui umuhimu wa katiba bora.
Do you mean there's no land grabbing in Kenya? Absolutely no Kenyan should point a finger against anybody coz we all know venye vitu viko Kwa grao uko mashinani.
 
We kweli zumbukukuHivi kuna nchi yenye uchumi wa kuinunua nchi nyingine?

Ilishatokea wapi nchi ikanunua nchi? Na akili zako zilivyo finyu unaweza kua unaongea hivi kwa kumaanisha GDP ya Sweden ni kubwa kuliko za hayo mataifa uliyoyataja bila kujua resources zilizopo kwenye hayo mataifa zina thamani mara trillion ya hicho kiGDP cha hiyo Sweden.
Wewe ndio umechemsha zaidi. Wewe sio mchumi sijui kwa nini unajifanya kuwa unafahamu haya mambo kiasi cha kumtusi MK254? Wewe ni mjinga kwa kulinganisha resources zilizo chini ya ardhi hapa Afrika Mashariki na Gdp ya Sweden. Kamwe huwezi linganisha resources ambazo hazijachimbwa na resources ambazo zimechimbwa na kutumika kuunda uchumi. Gdp ndio kigezo cha msingi kwenye kulinganisha utajiri wa nchi mbali mbali.

Kulingana na akili yako finyu, DR Congo ambayo ina madini aina karibu zote ni tajiri kushinda UK ambayo haina madini mengi? UK ni tajiri kwa sababu wananunua madini kutoka nchi za kiafrika ingawa wao hawana madini ardhini. Kuwa na dhahabu ardhini bila ya kuwa na ujuzi wa kuyachimba na kuyarefine ni ujinga tu. Wao wana industries ya kurefine dhahabu, mafuta, steel, aluminium na kadhalika. Ilhali sisi Waafrika hatuna hizi industries.

Kuwa na resources ardhini bila ya kuwa na akili ya kuyachimba na kuyarefine ni ujinga. Waafrika sisi ni wajinga kwa sababu tunaringa na madini yaliyo ardhini ambayo hatuna uwezo wa kuyachimba. Makampuni kutoka nje ndio yanakuja kuyachimba na kuyapeleka kwao. Usiwahi linganisha Gdp ambayo ni kigezo cha utajiri wa nchi na madini yaliyo ardhini ambayo bado hayajachimbwa.
 
Rais yupo kwajili ya wananchi hayupo kwaajili ya mabwenyenye wazungu kama huko kwenu sasa tamaduni za kwenu usilete huku. Kwanza vipi umeacha habari ya korona au ndio maji ya shingo maana kila kukicha ulikuwa unajisifia kupima sasa hivi imeishia wapi ile Pima pima pima pimaaa
 
Back
Top Bottom