Shida ipo.
Hutoweza kucommunicate na taifa lolote duniani or should I say nje ya africa
Well kama ni hivyo basi leo kungekuwa hakuna tatizo la watu wazima ambao ni graduates kushindwa kumudu English sababu hata wao wamejifunza ukubwani for 6 years ukiondoa miaka ya chuo kikuu.
Na hao watu waliojifunza kichina ukubwani ni wangapi au ni asilimia ngapi ya graduates wote?
Hautoweza kusoma vitu vilivyoandikwa nje ya lugha yako kwa kutumia lugha yako kama hata kutumia hiyo lugha yako ni tatizo na hauwezi.
Tanzania kuna lugha zaidi ya 100 na asilimia 10 tu ya watanzania ndio wanatumia Kiswahili kama main language na 90% wanatumia kama second language.
Sasa hapo hata ukikitumia Kiswahili shuleni effect itakuwa ndogo vilevile na kutakuwa hakuna tofauti na kutumia English at all.
Considering mpaka leo hii tumeshindwa kubadirisha kutoka kiingereza kwenda Kiswahili.
Unadhani tutaweza kutumia Kiswahili wakati hata kubadirisha kwenda Kiswahili tumeshindwa?
Even kutumia lugha yenyewe ya hayo masomo tumeshindwa.
China na India wana lugha nyingi lakini lakini wanaoutimia main languages ni zaid ya asilimia 10.
Hivyo hata wakitumia lugha zao effect itakuwepo.
So kujifananisha nao ni kama kumpa tembo maji anayokunywa mbuzi.
Na kama kufundisha kwa lugha mama kutaleta wavumbuzi.
Kwanini primary Level wanafundisha Kiswahili masomo yote ukiondoa English na hakuna wabunifu au wavumbuzi wadogo?
Usiniambie hakuna wabunifu au wavumbuzi wadogo duniani.
Na mkuu unataka kusema kwamba hizi shule za kata zinafundisha masomo ya English kama inavyotakiwa?
Hapana bali wanatumia English na Kiswahili kwa asilimia kubwa na wanafunzi bado hawaelewi na still hakuna wavumbuzi wala wabunifu labda wapo lakini wapo wapi?.
Kingine ni kwamba wahindi na wachina sio kwamba hawajui kiingereza kabisa hapana wanajua.
Sababu wanajua umuhimu wa kiingereza kwenye kasi ya maendeleo duniani na kushirikiana na mataifa mengine so kiingereza ndio main key kwa kuwasiliana.
Sababu kiingereza kina umuhimu wake duniani au huo umbuzi na ubunifu wetu hautofika popote considering taifa bado masikini na wala hakuna watu wanaojua umuhimu wa ubunifu na uvumbuzi.
Kwani sasa hivi hakuna wabunifu au wavumbuzi watu wazima wa kiafrika?
Hapana wapo lakini huwezi kuwaona wala kuwasikia sababu hata waijitangaza hakuna mwafrika atawaikiliza maybe angetumia English kujitangaza angesaidiwa na watu wanaojua umuhimu wa ubunifu na uvumbuzi.
Na ndio sababu nikasema tatizo lipo.
Sababu hata ukiwa na uvumbuzi kama huwezi kucommunicate na watu wanaojua umuhimu wa uvumbuzi na ubunifu basi utakufa na uvumbuzi wako hapahapa.
Mkuu kiingereza ni essential kwenye ulimwengu wa leo.
Umesema vitu vingi. Lakini nadhani unachokosa ni picha pana tu ya umuhimu wa kujifunza kwa lugha yako.
Utamaduni ukipanuka uhitaji wa bidhaa za kiswahili unakuwa... Mfano kupanuka kwa kiingereza kumefanya watanzania na dunia kufurahia Filamu za kiingereza ..maana wanaelewa.
Sasa Ukisema hatuwezi nakushangaa maana kiswahili chenyewe its hardly 150 years.. ukisema ni safari ndefu nitakubali ila kusema haiwezekani nitashangaa...
Wanaojifunza lugha ukubwani ni wengi.. hakuna mtu aliyesoma kichina toka akiwa mdogo nchi hii ni leo tuna wakalimani lukuki wa lugha ya kichina.. simply kwa sababu ya uhitaji.. wapo Watu wanazungumza kiarabu na mie nimejifunza kihehe na kisukuma ukubwani. Hiyo sio kazi ni interests .
Tutawezaje:
Kwa kufasiri.. lazima kufasiri maarifa sio vitabu. Elimu often hakusaidii kama haiwezi kufasiriwa katika mtazamo wa mazingira yako.
Baada ya kujua Taifa liko wapi, na linapaswa liende wapi, Kwanza tunajiwekea
nini kifundishwe, kisha
Kwa nini,
Lini kifundishwe ,halafu
kwa namna gani kifundishwe
Mfano unanifunza geografia ya Central Amerika for what!? Au Kakao (Ghana) Hii inanisaidia nini!? Lazima ujue kwanini unataka Watu wajifunze kile Unachotaka wajifunze.
Swala la communication ni swala la kuhitajika. Kama huna unachoweza kunivutia niwasiliane na wewe, then tusiwasiliane... Ila ukiwa na chochote kitakachofanya tuhitajiane naamini tutawasiliana.. bila kuwa na sababu ya kuwasiliana kujua lugha hiyo ya kizungu ni umbea tu. Maana hakufanikishi lolote.
Fundisha.kiswahili Watu waweze kuyajua maeneo yao vizuri ili waweze kuyatawala... Hiyo ndio Intelligence... Unapenda kijijini unaambiwa wakati wa upepo usipite njia ya chini maana utawashwa.. wamejifunza upepo huvumisha upupu..wameyatawala Mazingira yao.. kiakili.
Uvumbuzi sio kujenga meli pekee... Hata aliyegundua uyoga huu unaliwa na huu hauliwi... Aliyegundua Michembe ni njia bora.ya kutunza viazi.. na maparage ni equivalent ya conflackes wote walivumbua... Ni Mainjinia wetu waliokariri ndio wanaowatisha wananchi wavumbuzi namna bora ya kuboresha teknolojia zao.
Tukiwa tunasoma kulikuwa na vijana toka vijijini kabisa kwenye Umitashumta walikuwa wanafanya vumbuzi kubwa mno.na za maana zenye tija kama zitaendelezwa... shinda ni management of talents...
Kuongea kiingereza hakukufanyi miraculously smart.. na wala hakukufanyi uwe mvumbuzi... Wavumbuzi wako wengi na kwa taifa letu ukiondoa dharau wavumbuzi wengi wako vijijini na mashambani... True innovation.