Mokaze
JF-Expert Member
- Aug 3, 2018
- 14,370
- 14,945
Kwa bahati mbaya sana, vijana wa sasa hapa Tz sio tu wanashindwa kuzungumza au kuandika Kiingereza:- Hata Kiswahili wanachoandika au kukiongea mara nyingi sana kina makosa. Ukitaka kujua tatizo ni lugha (iwe Kiswahili au Kiingereza), pitia tu mambo watu wanayoandika wanapochangia mada kwenye mitandao.
a) WENGI SANA hawawezi kutofautisha kati ya herufi L na R. Unamsikia mtu anasema "nilipokuwa nachumbia mahari ambapo mahali ilipelekwa ni kwa mjomba"
b) Ni Watanzania wengi (hata baadhi ya viongozi wanasiasa) wanasema:- "Tangia sasa...." wakimaanisha kuanzia sasa. Hawajui wangepaswa kusema "Tangu sasa", au "kuanzia sasa"
c) Wapo pia watu wengi ambao hawajui the difference between a subject and a predicate (samahani kwa kuchanganya kimombo ndani maana hata mimi yapo maneno ya Kiswahili siyajui - kwa mfano subject and predicate). Nilitaka kusema kwamba watu wengi "wanachanganya mambo" wakati wanazumgumzia mambo mawili tofuati.
Kwa mfano mtangazaji wa habari anasema:- 'Lile gari lilimgonga mtu na kufa" Maana ya mstari huu ni kwamba gari ndio lilikufa. Angetaka kusema mtu ndie kafa angesema "lori lilimgonga mtu akafa"
d) Makosa yapo mengi tu kwenye Kiswahili kinachozungumwa na baadhi ya wasomi wa Tanzania. Kosa lingine ni pale mtoa habari anaposema:- "Alipigwa risasi akaweza kufa" badala ya kusema alipigwa risasi akafa. Unaposema mtu ameweza kitu fulani una maana hicho ni kitu ambacho alikuwa anataka akipate na akajitahidi mpaka akakipata. Hivyo sio sawa kusema mtu aliyepigwa risasi aliweza kufa maana hakuwa anajitahidi kufa.
So, my question to your dear readers is this:- If we can make SO MANYA MISTAKES in Kiswahili which is our mother tongue, do you expect us to be proficient, and efficient in making utterences in a foreign language? No way ! CIAO !
hata mimi yapo maneno ya Kiswahili siyajui - kwa mfano subject and predicate)
Subject ni kiima na predicate ni kiarifu.
Kwa mfano mtangazaji wa habari anasema:- 'Lile gari lilimgonga mtu na kufa"
Hiyo sentensi ipo sahihi na inaeleweka, hiyo inaitwa "sentensi tata" na hata katika lugha zingine sentensi za aina hiyo zipo (Ambiguous sentences).
