Wangapi wanamkumbuka Umsolopagaas?

Wangapi wanamkumbuka Umsolopagaas?

Angelikuwa hapa bongo ungekuta keshamlamba bj inkosikazi kwa haya anayofanya, huyu utingo angeshughulikiwa na wale kaa, angepelekwa bonde la czambaz!
 
Tehtehtehteh...nimecheka sana, inaelekea vijana wa zamani mnakumbuka Enzi zenu....Hivi hebu niambie lile kabila la Wagagagigikoko lilikuwa linasimuliwa katika kitabu gani vile??

Bulicheka!
 
Nakufa,nakufa,wapo wapi wale wakuu waliotangulia mbele??siwaoni,wewe upo makumazahn??au umekwisha nitangulia sehemu ya mbele nisiyoijua mimi?,mahali panapozungukazunguka??Nasikia harufu ya damu,Naitwaaa!Ndipo alipoiinua inkosikazi yake,akaizungusha ,Ikawa kama inayotoa nuru ya dhahabu,,
 
lakini kiliwai kupigwa marufuku hicho kitabu...... ilionekana kama kinafundisha ujasili flani ambao watawala waliona kama ungeleta madhara kwa vijana...wengi waliosoma hicho kitabu kwa hisia wanatembea na vishoka kiunoni mpataka leo hii...
 
Mshana, jitolee kutuwekea walau mhitasari wa story za huyo jamaa. Ninakumbuka lakini sio kivile ... ulikuwa ukikisoma unajihisi kama vile unaona kinachoendelea namna walivyokuwa wakitumia miti / matawi kukatiza mbugani ...
 
Kuna baadhi ya vitu huwakutanisha watu kiroho hii post ni kimojawapo! najiona mimi wa wakati huo nikisoma hivi vitabu mstari kwa mstari

Ohoo,ushaanza sasa mambo yako!acha mambo ya kijinga bhana!
 
Huyu jamaa ndo alikua nauwezo wa kuvuka maji ya shingo bila pu.mbu hazigusi maji
 
TU
Moja ya vitabu vizuri vilivyowahi kuburudisha na kuchangamsha akili wakati ule ni vile vya bwana Msa (Mohamed Said Abdullah). Kuna mtu anakumbuka SIRI YA SIFURI? Au niko mwenyewe?
tuko wote
 
Back
Top Bottom