Wangapi wanamkumbuka Umsolopagaas?

Wangapi wanamkumbuka Umsolopagaas?

Abunuwasi
Abunuwasi na Abdul wale watu walikuwa kiboko wale full vituko but wanafundisha kuna kisa kimoja masikini kaenda kumshukuru tajiri jirani yake kuwa amekula chakula kwa harufu ya mboga toka kwa tajiri yaani alikuwa ana lumangia tajiri akaenda kushtaki alipwe harufu yake ya mchuzi masikini akawa ana haha kesi imemkalia vibaya mara Abunuwasi anapita kumuuliza akamuhadithia mpaka mwisho Abunuwasi akasema nitakusaidia kisha kaanza kutangaza kuwa pana sherehe nyumbani pake akanunua mahitaji yote wageni wamefika lakini cha ajabu mchele upo kule moto upo huku nyama kule wageni wakachachamaa wakiongozwa na tajiri hii haiwezekani hiki chakula kitaiva vipi bila kufanya hivi? Abunuwasi ndipo alipoamka na kusema bwana tajiri kisa hiki ni sawa na ulivyo mshtaki masikini kesi ya harufu ya mchuzi wako.
 
Tujiepushe tu kutaja kitabu cha mfalme juha
1474564762632.jpg
 
Tehtehtehteh...nimecheka sana, inaelekea vijana wa zamani mnakumbuka Enzi zenu....Hivi hebu niambie lile kabila la Wagagagigikoko lilikuwa linasimuliwa katika kitabu gani vile??
kwenye umsolopagaz kulikuwa kuna kabila la wazuvendi
 
ninasikitika mtu niliye mfanyia hisani kwa kumwazima vitabu vifuatavyo

hekaya za abunuwasi
mashimo ya mfalme sulemani
malaika wa shetani
tutarudi na roho zetu?
Alfu lela ulela
simu ya kifo
mnuko wa damu
n.k

HAKUJUA THAMANI YAKE ALIVIPOTEZA NA HAKUWA NA MAJIBU YA WAPI VILIPO.

those days.... wapendwa mmenikumbusha mbali.
 
Dah mkuu mshana jr umenikumbusha masimulizi ya hivi vitabu vya Sir Haggard,Naweza sema huyu mzulu Msolopagazi ni moja kati ya binadamu wa Riwayani wenye mikwala ya hatari .....moja kati ya majigambo yake alipokutana na wajivuni "Mimi msolopogaas,mwana wa inkosikazi,mjukuu wa makumazan,nyanya wa khumabakoz, wa damu ya Chaka, wa kabila la Wazulu, mkuu wa jeshi la Nkomabakosi, kama wengi wengine walivyofanya; nawe utajiinamisha mbele ya Inkosikazi kama walivyofanya wengi wengine. Ndiyo, cheka, cheka! Usiku wa kesho
fisi watakuwa wanacheka na huku wanavunja na kuzitafuna mbavu zako
."...Huyu mtu hataree sana mkuu,asante kwa hizi kumbukumbu kiongozi.
 
Dah mkuu mshana jr umenikumbusha masimulizi ya hivi vitabu vya Sir Haggard,Naweza sema huyu mzulu Msolopagazi ni moja kati ya binadamu wa Riwayani wenye mikwala ya hatari .....moja kati ya majigambo yake alipokutana na wajivuni "Mimi msolopogaas,mwana wa inkosikazi,mjukuu wa makumazan,nyanya wa khumabakoz, wa damu ya Chaka, wa kabila la Wazulu, mkuu wa jeshi la Nkomabakosi, kama wengi wengine walivyofanya; nawe utajiinamisha mbele ya Inkosikazi kama walivyofanya wengi wengine. Ndiyo, cheka, cheka! Usiku wa kesho
fisi watakuwa wanacheka na huku wanavunja na kuzitafuna mbavu zako
."...Huyu mtu hataree sana mkuu,asante kwa hizi kumbukumbu kiongozi.
Bonge la mkwara
 
Abunuwasi na Abdul wale watu walikuwa kiboko wale full vituko but wanafundisha kuna kisa kimoja masikini kaenda kumshukuru tajiri jirani yake kuwa amekula chakula kwa harufu ya mboga toka kwa tajiri yaani alikuwa ana lumangia tajiri akaenda kushtaki alipwe harufu yake ya mchuzi masikini akawa ana haha kesi imemkalia vibaya mara Abunuwasi anapita kumuuliza akamuhadithia mpaka mwisho Abunuwasi akasema nitakusaidia kisha kaanza kutangaza kuwa pana sherehe nyumbani pake akanunua mahitaji yote wageni wamefika lakini cha ajabu mchele upo kule moto upo huku nyama kule wageni wakachachamaa wakiongozwa na tajiri hii haiwezekani hiki chakula kitaiva vipi bila kufanya hivi? Abunuwasi ndipo alipoamka na kusema bwana tajiri kisa hiki ni sawa na ulivyo mshtaki masikini kesi ya harufu ya mchuzi wako.
Hiki kitabu kinaitwaje?
 
Hiki kitabu sijui kama kinapatikana, baadhi ya vitabu vya kale vinapatikana kwa urahisi mfano Adili na nduguze, Alfulela ulela n.k ila hiki sijawahi kukiona japo huwa nasikia story zake kwa wingi
Mkuu kinapatikana ingawa kwa shida kiasi kwa maana ya kwamba si rahisi kukikuta kwenye bookshop nyingi ,mimi nilikisoma zamani kidogo kwenye maktaba kuu ya Tabora,na Natumai hata pale Tanganyika Library kinaweza kuwepo pia.
 
Mkuu kinapatikana ingawa kwa shida kiasi kwa maana ya kwamba si rahisi kukikuta kwenye bookshop nyingi ,mimi nilikisoma zamani kidogo kwenye maktaba kuu ya Tabora,na Natumai hata pale Tanganyika Library kinaweza kuwepo pia.
Ngoja nijaribu kukitafuta
 
Back
Top Bottom