Wanawake wengi hawawataki wanaume maskini

Wanawake wengi hawawataki wanaume maskini

Unaendaje kupigwa kende kwa 10000?
Hiyo si hela ya maji tu.
Nureen muhindi huyu mara ya mwisho ndo nilimpa 35000.
Na akanirudishia zote asubuhi na kusema niende kwao nikamuoe.
Sijawai kuhonga senti 10 tokea miaka 25 sasa.
Hawa na mwenzie nilikula buure kabisa.
Wanapishana tu chumbani .
 
63B8D243-CEE4-447C-93B5-99A4BF51588F.jpeg

Harmful na dosho12 mbona hamchangii mada😂 wapi shemeji Castle_Lite
 
Hii hoja huwa inanishangaza sana. Kwamba mkiingia kwenye mahusiano maisha yenu yanaganda kumsubiri mwanaume?

Ndio maana sometimes huwa nawaza women empowerment ni poor utilization of fund and resources. What is a meaning of empowering a girl child if she will grow up and expect a man to solve all of her living responsibilities.
Women gani unazungumzia mkuu?
I mean kizazi kipi?
 
Unaendaje kupigwa kende kwa 10000?
Hiyo si hela ya maji tu.
Nureen muhindi huyu mara ya mwisho ndo nilimpa 35000.
Na akanirudishia zote asubuhi na kusema niende kwao nikamuoe.
Sijawai kuhonga senti 10 tokea miaka 25 sasa.
Hawa na mwenzie nilikula buure kabisa.
Wanapishana tu chumbani .
Hii nayo ni shida, mtu anaweza toa upendo wewe. Unahesabia umepewa bure
 
Tuanze chini , tukijipata anaanzq kuongeza michepuko pesa inaenda nje , ndani unaanzq kuhangaika pesa yote nje
Ya nn yote hayo?
Kwa hiyo unaona ni heri uolewe na mwanaume mwenye mapesa yake tayari hili kusudi hata akiwa anazitumia kwa michepuko kwako wewe haitakuuma sana si ndio maana yake?

Maana mnavyokomaa na hii hoja yenu, utafikiri hao wanaume mnaowakuta wameshajipata ndio huwa hawachepuki.
 
Hapo sasa utajua we mwenyewe mkuu! Hujui tu uvumilivu wa kuanza na mtu chini ntajichosha kukuelezea.. magumu anayopitia mtu kumvumilia mwenzie vishawishi anavyovuka mpaka wafikie lengo! Jinsi mtu unavyojikana ili mwende sambamba na huyo masikini… Halafu anajipata anajiona matawi; hivi nilikutanaje kutanaje na hili limwanamke!! Hapa hatuongelei tamaa ya pesa tunaongelea kuanza na mtu chini, kama huwezi kutuliza fahamu vzr unakimbilia tamaa ni ww sasa! Sio kila jambo ni kuhusu tamaa na sio kila mtu ana tamaa..
Kwa hiyo kumbe hofu yako wewe ya kuanza na maskini mwenzio from the scratch ni ila akianza kuchepuka na kutumia pesa ambazo mmezitafuta wote kwa wanawake michepuko yake si ndio?

Swali, sasa je, hao wanaume ambao mnawakuta tayari wameshajipata ndio huwa hawachepuki?

Au hao wanaume ambao tayari mnawakuta wameshajijenga hata wakichepuka haiwaumii chochote kwa sababu tu hamkushirikiana kutafuta pesa wanazohonga kwa michepuko yao?
 
Kwa hiyo unaona ni heri uolewe na mwanaume mwenye mapesa yake tayari hili kusudi hata akiwa anazitumia kwa michepuko kwako wewe haitakuuma sana si ndio maana yake?

Maana mnavyokomaa na hii hoja yenu, utafikiri hao wanaume mnaowakuta wameshajipata ndio huwa hawachepuki.
Huwezi kuelewa , sisi ambao ni wahanga ndo tunaelewa!

Na hii kwenye jamii ni issue iliyoharibu familia nyingi sn na inaendelea kuharibu, more than 60 percent....fuatilia sio kusema tunakomaa na hoja ndo hali halisi...

Kwanza mi personally siwezi ku handle cheating sina huo moyo ...tusije gawana msjengo bure...


wakikutwa na pesa wAtajua wenyewe pesa katafuta mwenyewe aonge anavyotaka hiyo michepuko ....ila sio uhangaike na mkeo instead of ku focus kujenga familia atafute mwingine ale mwingine...
 
Wanawake wengi wamejikuta wameingia kwenye ndoa za majuto kwa tamaa ya pesa, kumbe amani yao ilikuwa kwa mwanaume masikini aliyemdhania. Ni woga tu, maisha mazuri ya ndoa ni wote muanzie kwenye zero point
Kwa vile wengi wao upeo ni mdogo sana hawawezi kukuelewa hapa.

Nimesoma comments za wawili hapo wanajitetea eti hawako tayari kuolewa na mwanaume maskini kwa sababu wanaogopa hao wanaume maskini watakuja kuwasaliti huko mbeleni wakishajipata...

...sasa, swali langu ni hivi kwao je, hao wanaume ambao tayari wameshajipata ndio huwa hawachepuki?... maana walivyoweka hoja yao utafikiri kwamba hao wanaume matajiri wanaowakimbilia kuolewa nao ndio huwa hawachepuki wala hawahongi michepuko.

Wasichokijua, hakuna mwanaume mwenye kiburi na anayedharau wanawake kama mwanaume ambaye tayari ameshajijenga kiuchumi na hasa akishajua wewe mwanamke umeolewa na yeye kwa sababu ya pesa tu.

Hawa wanajitengenezeaga matatizo bila kujua.
 
Siyo kweli, uzuri wa mwanamke ni sura na makalio, siyo hali yake ya kiuchumi wala mazingira na endapo atakuwa hana elimu kubwa sana huyo ndiye anafaa kwa familia bora maana anakuwa hana makuu.
Hawa wanawake wa kisasa wana upuuzi mwingi sana waliokaririshwa kwenye semina zao za usawa.

Yaan mpaka wanaamini vigezo walivyojiwekea wao kwenye uchaguzi wa mwanaume kama vile kipato,umri mkubwa na urefu basi ndio hata wanaume nao tumejiwekea vigezo hivyo hivyo kwenye kuchagua mwanamke.

Wasichokijua wanaume tulio wengi vitu kama financial status ya mwanamke huwa hatuangalii kabisa, kikubwa hasa tunachoangalia ni physical attractiveness na haiba ya kike(feminity).

Leo hii mwanamke kama "Sanchworld" ana thamani kubwa sana kwenye soko la mahusiano kuliko mdada mwenye muonekano wa kawaida ambaye ana PHD kutoka Cambridge university na Boss wa NHIF na anakunja mshaara wa 35m kwa mwezi.

Yaani we mwanamke hata uwe na pesa kiasi gani, ila kama ni mbaya hauna mvuto wowote, hakuna mwanaume atakayekuwa na shobo na wewe sana sana wewe ndio utaishia kutongoza na kuhonga wanaume. Wakati huo kuna Khadija matako wa uswahilini ambaye hana pesa wala elimu ila ndio hivyo tena wanaume wanamtafuta kwa hudi na uvumba.

Sasa huyo anayesema eti hata sisi wanaume hatupendi kuwa na mwanamke maskini, anachekesha sana.
 
Hawa wanawake wa kisasa wana upuuzi mwingi sana waliokaririshwa kwenye semina zao za usawa.

Yaan mpaka wanaamini vigezo walivyojiwekea wao kwenye uchaguzi wa mwanaume kama vile kipato,umri mkubwa na urefu basi ndio hata wanaume nao tumejiwekea vigezo hivyo hivyo kwenye kuchagua mwanamke.

Wasichokijua wanaume tulio wengi vitu kama financial status ya mwanamke huwa hatuangalii kabisa, kikubwa hasa tunachoangalia ni physical attractiveness na haiba ya kike(feminity).

Leo hii mwanamke kama "Sanchworld" ana thamani kubwa sana kwenye soko la mahusiano kuliko mdada mwenye muonekano wa kawaida ambaye ana PHD kutoka Cambridge university na Boss wa NHIF na anakunja mshaara wa 35m kwa mwezi.

Yaani we mwanamke hata uwe na pesa kiasi gani, ila kama ni mbaya hauna mvuto wowote, hakuna mwanaume atakayekuwa na shobo na wewe sana sana wewe ndio utaishia kutongoza na kuhonga wanaume. Wakati huo kuna Khadija matako wa uswahilini ambaye hana pesa wala elimu ila ndio hivyo tena wanaume wanamtafuta kwa hudi na uvumba.

Sasa huyo anayesema eti hata sisi wanaume hatupendi kuwa na mwanamke maskini, anachekesha sana.
Feminism imewauzia wanawake illusion mbaya sana. Katika list ya makundi ambayo nayadharau wakitoka mashoga wanafuata feminists
 
Huwezi kuelewa ,

wakikutwa na pesa wAtajua wenyewe pesa katafuta mwenyewe aonge anavyotaka hiyo michepuko ....ila sio uhangaike na mkeo instead of ku focus kujenga familia atafute mwingine ale mwingine...
Sasa kisichoeleweka nini hapo sasa?

Mbona umeruka ruka wee halafu mwisho wa siku umekuja kwenye ile ile nadharia yangu? ambayo ndio ukweli wenyewe.

Hiyo kauli yako ya "watajua wenyewe pesa katafuta mwenyewe, aonge anavyotaka hiyo michepuko".... inaonesha kwamba kama mumeo umemkuta tayari ana hela zake hauna shida kabisa hata akizimalizia zote kwa michepuko, kwa sababu tu haukuwepo wakati anazitafuta.

Hivyo basi, nyie mko tayari kuvumilia umalaya wa mwanaume ambaye mmemkuta tayari ana fedha zake, ila sio mwanaume ambaye mmeanza naye chini.

Na huu ndio ukweli wa hii hoja yenu ambao mnanajing'ata ng'ata kuukubali.
 
Kwa hiyo kumbe hofu yako wewe ya kuanza na maskini mwenzio from the scratch ni ila akianza kuchepuka na kutumia pesa ambazo mmezitafuta wote kwa wanawake michepuko yake si ndio?

Swali, sasa je, hao wanaume ambao mnawakuta tayari wameshajipata ndio huwa hawachepuki?

Au hao wanaume ambao tayari mnawakuta wameshajijenga hata wakichepuka haiwaumii chochote kwa sababu tu hamkushirikiana kutafuta pesa wanazohonga kwa michepuko yao?
Ndio
 
Sasa kisichoeleweka nini hapo sasa?

Mbona umeruka ruka wee halafu mwisho wa siku umekuja kwenye ile ile nadharia yangu? ambayo ndio ukweli wenyewe.

Hiyo kauli yako ya "watajua wenyewe pesa katafuta mwenyewe, aonge anavyotaka hiyo michepuko".... inaonesha kwamba kama mumeo umemkuta tayari ana hela zake hauna shida kabisa hata akizimalizia zote kwa michepuko, kwa sababu tu haukuwepo wakati anazitafuta.

Hivyo basi, nyie mko tayari kuvumilia umalaya wa mwanaume ambaye mmemkuta tayari ana fedha zake, ila sio mwanaume ambaye mmeanza naye chini.

Na huu ndio ukweli wa hii hoja yenu ambao mnanajing'ata ng'ata kuukubali.
Nisome tena
Wapi nimerukaruka
Mi nimekujibu ulichoandika!

Na nimesema personally siwezi ku handle hayo mambo...sina huo moyo kabisa...

Nimekujibu ni bora ahonge hizo pesa zake sio atafute mke ale mchepuko...sio fair..
Sijasema kuwa watu wawe tayari kuvumilia umalaya wa waume zao...

Ndo maana divorce rate ni kubwa, na zinaombwa na wanawake
 
Feminism imewauzia wanawake illusion mbaya sana. Katika list ya makundi ambayo nayadharau wakitoka mashoga wanafuata feminists
Feminism ni silaha anayoitumia shetani kuwaangamiza wanawake kwa kuwapotosha vitu vingi kuhusu maisha.

Baada ya wanawake kuona equality wanayoitaka wao haiwezekaniki, sasa hivi feminists wanawasisitiza kuji isolate na wanaume na kisha kutafuta pesa kwa hudi na uvumba wakiamini eti kuwa pesa itamreplace mwanaume na kuwafanya wawe na maisha ya furaha zaidi.

Ngoja tuone mwisho wao.
 
Feminism ni silaha anayoitumia shetani kuwaangamiza wanawake kwa kuwapotosha vitu vingi kuhusu maisha.

Baada ya wanawake kuona equality wanayoitaka wao haiwezekaniki, sasa hivi feminists wanawasisitiza kuji isolate na wanaume na kisha kutafuta pesa kwa hudi na uvumba wakiamini eti kuwa pesa itamreplace mwanaume na kuwafanya wawe na maisha ya furaha zaidi.

Ngoja tuone mwisho wao.
Nani alikwambia hiyo ndio maana ya feminism?😂 yaani mpaka mambo ya kishenzi sikuhiz yanajumuishwa kwenye feminism kumbe!
 
Nisome tena
Wapi nimerukaruka
Mi nimekujibu ulichoandika!

Na nimesema personally siwezi ku handle hayo mambo...sina huo moyo kabisa...

Nimekujibu ni bora ahonge hizo pesa zake sio atafute mke ale mchepuko...sio fair..
Sijasema kuwa watu wawe tayari kuvumilia umalaya wa waume zao...

Ndo maana divorce rate ni kubwa, na zinaombwa na wanawake
Sijui hata unachokataa ni nini wewe mwanamke, wakati comments zote unakubaliana na nadharia yangu.

Angalia comment yako ya kwanza hii halafu tuichambue kimantiki sawa.

"Tuanze chini , tukijipata anaanzq kuongeza michepuko pesa inaenda nje , ndani unaanzq kuhangaika pesa yote nje
Ya nn yote hayo?"


Katika muktadha wa ndoa kwenye comment yako hii unamaanisha kwanza sisi wanaume tukianza kushika pesa lazima tuwe na michepuko na lazima tuhonge hiyo michepuko.

Sass basi wewe binafsi hauko tayari kuolewa na mwanaume kapuku, kwa sababu siku wewe na mwanaume huyu kapuku mkiaanza kupata pesa, mwanaume huyu kapuku ataanza kuwahonga michepuko kitu ambacho kitakuuma sana maana atakuwa anahonga pesa ambazo wewe na yeye mmeshirikiana kuzitafuta, yaan utaona ni kama vile jasho lako linaenda kuliwa na mwanamke mwingine... na ndio maana ukamaliza kwa kusema "ya nini yote hayo".

Katika muktadha huo huo wewe uko tayari kuolewa na mwanaume ambaye tayari ana pesa zake, na mwanaume huyu unaona ndio sahihi kwa mwanamke anayetaka kuolewa... kwa mwanaume huyu haujatilia maanani sana possibility ya yeye kuchepuka, kama ambavyo umetilia maanani possibility ya mwanaume yule kapuku kuchepuka akishapata pesa kwenye scenario ya kwanza.

Sasa swali, kichwani mwako unaamini sisi wanaume kuchepuka ni kasumba yetu, kwanini haujali kabisa suala la mwanaume huyu tajiri kuchepuka? Jibu liko wazi tu ni kwa sababu haukushiriki kuzitafuta pesa za huyu mwanaume wewe umezikuta tu ndio maana hata akichepuka huko na kuzihonga zote wewe hauumii kwa chochote kama ambavyo ungeumia endapo kma mngekuwa mmeshirikiana wote kuzitafuta.

Sijajua nini kinakufanya mpaka unakataa hii fact na wakati fikra zako zinaonesha huu ukweli ulio uchi... naona mwenzako hapo kakubali wazi kwa sababu kila mwenye akili timamu anaye reason properly ndio kitu anachokiona kwenye maandishi yako.

Hata kwenye hii comment yako unakubali, lakini bado unaiweka kinamna ya kukataa angalia "ni bora ahonge pesa alizotafuta mwenyewe, lakini sio zile alizotafuta mke.. sio fair... sasa hapa si unakubaliana na mimi?
 
Nani alikwambia hiyo ndio maana ya feminism?😂 yaani mpaka mambo ya kishenzi sikuhiz yanajumuishwa kwenye feminism kumbe!
It is deeper than you think my dear.

Najua wewe umekariri "equal rights for education, equal opportunites, equal rights for freedom, equal blah..blah.." si ndio?

Sasa sisi tunaiangalia zaidi ya hapo na hasa hii modern feminism imeleta upumbav mwingi sana kwenu nyie wanawake, ila hamjui kwa sababu social engineering mnayofanyiwa.
 
Nisome tena
Wapi nimerukaruka
Mi nimekujibu ulichoandika!

Na nimesema personally siwezi ku handle hayo mambo...sina huo moyo kabisa...

Nimekujibu ni bora ahonge hizo pesa zake sio atafute mke ale mchepuko...sio fair..
Sijasema kuwa watu wawe tayari kuvumilia umalaya wa waume zao...

Ndo maana divorce rate ni kubwa, na zinaombwa na wanawake
Halafu unavyosema eti personally hauwezi kuhandle cheating, wakati huo kichwani mwako unatembea na imani ya kwamba sisi wanaume ni wachepukaji siku tukijipata.

Hapo ni sawa na kusema "mimi sipendi kula nyama, ila napenda kula mchuzi wake ukiwekewa limao na pilipili".. yaan haupendi nyama ila unapenda kinachotokana na nyama.

Hivyo hivyo pia na wewe kwa kauli yako hii ni kwamba hauko tayari kuvumilia usaliti wa mwanaume kapuku mliyeanza naye chini, ila uko tayari kuvumilia usaliti wa mwanaume uliyemkuta na mihela yake.

Ungekuwa kweli wewe huwezi kuvumilia cheating, basi hata wazo la kuolewa haukupaswa kuwa nalo kabisa kwa sababu akilini mwako wanaume wote umeshatuweka kwenye group moja kuwa ni wachepukaji mara tu tupatapo hela.
 
It is deeper than you think my dear.

Najua wewe umekariri "equal rights for education, equal opportunites, equal rights for freedom, equal blah..blah.." si ndio?

Sasa sisi tunaiangalia zaidi ya hapo na hasa hii modern feminism imeleta upumbav mwingi sana kwenu nyie wanawake, ila hamjui kwa sababu social engineering mnayofanyiwa.
Ninaijua ndani nje na nimeisoma vzr mpk chuo kikuu.. hiyo modernization mnayotaka kuitumia haiapply hapa ila mnaforce tu! Mtu huko kaamka na imaginations zake za kutaka danga liwe na sifa za mume sjui mahari kilo 150 mnakuja kusema ni feminsm ..
 
Back
Top Bottom