Halafu unavyosema eti personally hauwezi kuhandle cheating, wakati huo kichwani mwako unatembea na imani ya kwamba sisi wanaume ni wachepukaji siku tukijipata.
Hapo ni sawa na kusema "mimi sipendi kula nyama, ila napenda kula mchuzi wake ukiwekewa limao na pilipili".. yaan haupendi nyama ila unapenda kinachotokana na nyama.
Hivyo hivyo pia na wewe kwa kauli yako hii ni kwamba hauko tayari kuvumilia usaliti wa mwanaume kapuku mliyeanza naye chini, ila uko tayari kuvumilia usaliti wa mwanaume uliyemkuta na mihela yake.
Ungekuwa kweli wewe huwezi kuvumilia cheating, basi hata wazo la kuolewa haukupaswa kuwa nalo kabisa kwa sababu akilini mwako wanaume wote umeshatuweka kwenye group moja kuwa ni wachepukaji mara tu tupatapo hela.