Wanawake Wana Akili Kuliko Wanaume? Hata kwenye Siasa na Uongozi, Wanawake Wameonyesha Uwezo Kuliko Wanaume

Pascal Mayalla

Platinum Member
Sep 22, 2008
50,504
113,618
Wanabodi,
Huku nikiisubiri kesho kwa hamu kushuhudia akili za wanawake kwenye kilele siku ya wanawake duniani hapo Machi 8, huku nikitafakari mwelekeo na mustakabali wa siasa zetu za hapa nyumbani Tanzania, nimekuja kujiridhisha kiukweli kabisa ukubali, ukatae, kumbe wanawake wana akili sana kutushinda sisi wanaume!, ila wengi walikuwa hawalijui hili kwasababu siku zote sisi wanaume tumekuwa tunawabania, tunawazibia na kuwakandamiza!.

Na hata huyu Mwanamke Numero Uno Tanzania, kiukweli alibaniwa sana na kama sio Mwenyeenzi Mungu kuingilia kati na kumuibua, kamwe tusingeutambua uwezo wake na akili zake!.

Hata kwenye medani za siasa na uongozi, kiukweli kabisa wanawake wameonyesha uwezo na kuwa na akili nyingi zaidi ya nanaume!, na akili kubwa kuliko wanaume ambao ni akili ndogo!.

Kesho tutashuhudia kundi fulani la wanawake 19 wenye akili kubwa, likiibuka kidedea dhidi ya kundi fulani kuubwa na watu fulani ambao huwa wanataniwa jina fulani la Utani!.

Hata wale wanyama Nyumbu, kwenye Serengeti migration, ,je ulijua kumbe mnyama ambaye huwa anaongoza kuvuka mto ni jike?. Kama ulikuwa hujui sasa ndio ujue na usubirie kesho na kushuhudia wanawake wenye akili kubwa wakifanya vitu vikubwa!.

Nahitimisha hili swali, ni wangapi humu walikuwa wanajua wanawake wana akili na uwezo kuliko mwanaume?. Yaani hata Eva, kumbe alikuwa na akili kuliko Adamu na kiukweli ndio maana wakiamua kitu ni wameamua!. Na usikute sisi ambao ni dhaifu kwa jinsia ile ndio maana tunapelekwa pelekwa, kwa kifupi tunapelekeshwa!.

Tena sio tuu wanawake wana akili kuliko wanaume bali hata uwezo!, Kuelekea Siku ya Wanawake Duniani: Je Wajua Kuna Wanawake Wana Uwezo Mkubwa Kuliko Wanaume ila Wamekuwa Wanabaniwa!. Hata Huyo Kuonyesha Uwezo na ...

Hata kwenye kazi Je, kuna kazi za kike na za kiume? Fupa hili lililowashinda wanaume wanne, mwanamke mmoja ataliweza?

Baada ya kuujua ukweli huu, sasa ni mwendo wa heshima na adabu kwa wanawake wote. Siku ya wanawake duniani, hongera wanawake wote duniani.
Mungu ibariki Tanzania
Paskali.
 
Wanabodi,
Huku nikiisubiri kesho kwa hamu kushuhudia akili za wanawake kwenye kilele siku ya wanawake duniani hapo Machi 8, huku nikitafakari mwelekeo na mustakabali wa siasa zetu za hapa nyumbani Tanzania, nimekuja kujiridhisha kiukweli kabisa ukubali, ukatae, kumbe wanawake wana akili ssna kutushinda sisi wanaume!, ila wengi walikuwa hawakijui hili kwasababu siku zote wanawake tunakuwa tunawabania!.
P najua toka dk 1 uliwapiga debe mno na kuombea chama kubwa lifarakane na kisambaratike,ila huenda akili kubwa zaidi zilizuia hilo .Hivyo akili kubwa ya chama imeshinda.🤔
 
Baada ya kuujua ukweli huu, sasa ni mwendo wa heshima na adabu kwa wanawake wote. Siku ya wanawake duniani, hongera wanawake wote duniani.
Mungu ibariki Tanzania
Paskali.
Anza kampeni wanaume tupumzike wao waongoze familia, kwa maneno mengine tupokezane majukumu wao wachukue yetu nasi tubebe yao.

Lakini kumbuka tulionywa tuishi nao kwa akili
 
P najua toka dk 1 uliwapiga debe mno na kuombea chama kubwa lifarakane na kisambaratike,ila huenda akili kubwa zaidi zilizuia hilo .Hivyo akili kubwa ya chama imeshinda.🤔
Umegonga penyewe huyu jamaa nilikuwa namjibu kila alipokuwa anapotosha humu JF kwa kujifanya anajua administrative law vizuri kwa kuleta notes za darasani akidhani mahakama inafanya kazi hivyo, wakati theories mahakamani ni sehemu ndogo sana zinafanya kazi, na ndipo nikamshauri kama anahisi CHADEMA hawakufuata taratibu aende akaungane na mawakili wa hao malaya 19 kupambana na akina Kibatala.

Hata hivyo, hakufanya hivyo, so what does it imply? Ni kwamba hana uwezo mahakamani tofauti na notes zake kuwadanganya wajinga wasiojua sheria, na hao wajinga hujikuta wanamwamini, wakati ni empty.

Labda tu nimwambie kitu asichokijua, japo sikutaka kumwambia, ni kwamba nyaraka za hao kina Mdee, kwa maana ya affidavits supporting their chamber summons, hakuna sehemu yoyote waliposema waliteuliwa na CHADEMA, so hiyo pekee ni issue meritorious kwa CHADEMA, ambayo tunajua sheria inaenda kuwagonga hao malaya kwenye miguu ya judge, bila wao kujua.

Japo humu JF, wakati maswali hayo yanaulizwa, walikuwa wanayaona hayana maana, na kuhusu kutokusikilizwa, karibu wote waliohojiwa walisema walipata taarifa kwa njia ya WhatsApp, ambayo kwa lugha nyingine tunasema TEHAMA, ambapo katiba ya CHADEMA inatambua matumizi ya TEHAMA. Hapa napo mbumbumbu hawawezi kujua umuhimu wa swali hili na mengine mengi. Hivyo basi, namalizia kwa kusema kuwa hao malaya 19 wanapigwa kweupe, na siku ya hukumu nitakuja hapa kutoa ushuhuda kama moja ya legal minds mkongwe hapa nchini.

NB: Sio kila mtu humu anapojibu upuuzi wa wale wajinga wa Lumumba kulingana na comments zao. Basi ni mpuuzi. No, wale wapuuzi wa Lumumba huwa tunawajibu kulingana na ujinga wao.
 
Wanabodi,
Huku nikiisubiri kesho kwa hamu kushuhudia akili za wanawake kwenye kilele siku ya wanawake duniani hapo Machi 8, huku nikitafakari mwelekeo na mustakabali wa siasa zetu za hapa nyumbani Tanzania, nimekuja kujiridhisha kiukweli kabisa ukubali, ukatae, kumbe wanawake wana akili sana kutushinda sisi wanaume!, ila wengi walikuwa hawalijui hili kwasababu siku zote sisi wanaume tumekuwa tunawabania, tunawazibia na kuwakandamiza!.
Biblia imetuongoza kwa kusema: Wanaume ishini na wake zenu kwa akili.. 1 Petro 3:7 (NEN)
... wanaume wamepewa nguvu, akili wamepewa wanawake.. ndio maana ukisoma biblia vizuri utakugundua mfalme suleiman alikuwa na wake wengi si kwasababu ya sex tu bali pia ni kutumia akili zao.. katika kukamilisha mambo yake ya ufalme.. kazi nyingi za kijasusi duniani zinafanywa na wanawake zaidi wanaume wanakuja kumalizia zile sehemu zinazohitaji nguvu (special force).. mimi binafsi nikitaka taarifa za mtu yeyote nayemtaka nampelekea mwanamke tu kazi yangu inakuwa imeisha
 
Wanabodi,
Huku nikiisubiri kesho kwa hamu kushuhudia akili za wanawake kwenye kilele siku ya wanawake duniani hapo Machi 8, huku nikitafakari mwelekeo na mustakabali wa siasa zetu za hapa nyumbani Tanzania, nimekuja kujiridhisha kiukweli kabisa ukubali, ukatae, kumbe wanawake wana akili sana kutushinda sisi wanaume!, ila wengi walikuwa hawalijui hili kwasababu siku zote sisi wanaume tumekuwa tunawabania, tunawazibia na kuwakandamiza!.
Kawawa funika kikombe
 
Back
Top Bottom