umenishangaza kuwa hukiri kosa ni kuonyesha udhaifu. kwa upande wangu nadhani kukiri kosa ni kuonyesha ushujaa, umetambua kosa lako na unataka kujirekebisha. mara nyingi kitu unachokiri kukikosea na ukaomba msamaha huwa hutarajii kurudia tena. na hapo ndo tunapopishana sisi ni wakaka.
mara nyingi mtu ambaye hataki kukiri kosa ni kwamba hayupo tayari kuacha kitu alichofanya, na hii ni hatari sana hasa katika mahusiano. Nampenda sana mume wangu, ukigundua kafanya kitu na wewe unadhani kuwa ni kosa, ukimwambia tu na kama kweli kafanya ataomba msamaha. Unajua wakati mwingine huwa tunafanya vitu ambavyo sisi wenyewe hatudhani kama ni kosa, lakini mwenzio akaona kuwa ni kosa. akikuambia, na kama kweli ulifanya, ni vizuri kukiri na kuomba msamaha. Mimi huwa ni msameheji mzuri sana, lakini kabla sijasamehe napenda nijue exactly nasamehe nini, nikiwa na stori robo ya kitu ulichonifanyia napenda muhusika aniambie stori kamili, yaani nijue kwa uhakika kabisa ni vitu gani vilitokea, wapi, na kwa wakati gani. unajua sometimes unaweza ukafanya mwenzako akakukosea, kwa hiyo nikijua details, huwa inanisaidia mimi siku nyingine nisimsababishe mwenzangu akarudia kosa ambalo alifanya.