Unakumbuka enzi zile sadamu hussein alivyokuwa anapigwa na bush lakini alikuwa bado anazidi kujigamba kuwa 'tutapigana hadi muiraki wa mwisho'
Mi naona jibu ni kama ulivyoliweka, ni kwamba tunahofia ile hali ya kuonekana 'unajigalagaza mbele ya mkeo', yaani ni kama vile unaonyesha udhaifu wako ktk kuongoza! Kiongozi mwoga mwoga hafai, inzi jasiri hufia kidondani. Yaani kama wewe rais unakuwa mdogo kama pilitoni, sisi wananchi unatuongoza tutakuonaje? Kwahiyo it's just a notion ambayo kuibadilisha inahitaji muda na patience
Nimeongea mengi, nasubiri maswali sasa
Kwakweli..
Nauliza swali moja hapa,kwa wanawake wanaokiri makosa na kuomba msamaha je inakuwa imetoka moyoni au atakuwa makini usimkamate tena??
Wanaume wengi hatuombi msamaha katika mazingira hayo kwa sababu wanawake wengi ni waongo. Unawezaje kumuomba msamaha mtu ambaye unaamini kuwa ni mwongo?Hivi kwanini wenzetu nyie si wepesi hata kidogo wa kukiri makosa yenu na kuomba msamaha? Kwanini mara nyingi huwa mnatafuta means ya kujusfty makosa kuliko kuomba msamaha? je ni ubabe ama ni aibu ama mnahisi kufanya hivyo ni kujishusha hadhi yani kutoka kuwa mwanaume na kuwa mtu mwingine?
je na kwa wale mnaokiri na kuwaangukia wake zenu kwa samahani, je wake zenu wamewahi kubadili heshima yenu ama hata kukudharau?
leo akina mama tukae tuwatupie maswali kwa kila hoja watakazo leta hadi tujue nini ni nini.
nawasilisha.
afadhali kungwi wetu umerudi
hoja yako nzuri sana dada hilo jambo hata mimi nakutana nalo mara kwa mara ila tatizo lililopo ni kwamba kama una hoja iliyokamilika kwamaana ya ushahidi usiotia shaka kwa mwanaume mstaraabu atakiri kosa na kuomba radhi ila kama unakuja na maneno ya kuambiwa au ulisikia huna uthibitisho wa unachokisema siwezi kukubali lazima nithibitishe kuwa sivyo hivyo unavyodhani au kufikiria. kufanya hivyo ndio tunaonekana wabishi, ila wapo wengine wakiona ukweli uko wazi wanatumia ubabe sasa hapo inakuwa siyo ustarabu. wengine wanaona itakuwa aibu kukiri na kuomba radhi au akikubali na wewe unaweza kulipiza fikra ni nyingi lakini inategemea zimetua kichwa gani na wakati gani. muangalie pia sehemu za kutubananisha iwe faragha siyo vikao vya wazee au mawifi sijui shangazi itakuwa ngumu kukiri.
Itoke moyoni wapi bwana, mara nyingi inakuwa ni kutaka kukuridhisha tu ili mjadala uisheNauliza swali moja hapa,kwa wanawake wanaokiri makosa na kuomba msamaha je inakuwa imetoka moyoni au atakuwa makini usimkamate tena??
dada kiukweli sipokwenye mahusiano lakini hapo ni ukatili sana na uonevu