Mr Rocky mimi bado najiuliza kwanini swala la nisamehe miongoni mwa walio wengi ni gumu? hao wanaofanya hayo ni ubabe ama ujinga?gfsonwin sio wote kwa maneno yako ambao huwa hawaombi samahani
Kuna mazingira ambayo kabisa unajiona umeenda mchomo na hukupaswa kusema au kutenda na unaomba msamaha kwa mwenzako
yaweza isiwe ni yale maneno ya moja kwa moja kuwa samahani dear nimefanya kosa ila vitendo vingine vinaashiria kumuomba samahani
Sio kwamba dhana ya ubabe au kuwa mwanaume ndio ikifanye uwe na roho ngumu kung'ang'ania kitu ambacho kabis unajua ni kosa
Hivi kwanini wenzetu nyie si wepesi hata kidogo wa kukiri makosa yenu na kuomba msamaha? Kwanini mara nyingi huwa mnatafuta means ya kujusfty makosa kuliko kuomba msamaha? je ni ubabe ama ni aibu ama mnahisi kufanya hivyo ni kujishusha hadhi yani kutoka kuwa mwanaume na kuwa mtu mwingine?
je na kwa wale mnaokiri na kuwaangukia wake zenu kwa samahani, je wake zenu wamewahi kubadili heshima yenu ama hata kukudharau?
leo akina mama tukae tuwatupie maswali kwa kila hoja watakazo leta hadi tujue nini ni nini.
nawasilisha.
PetCash so kwa wababa yapendeza wakiambiliwa sirini eeh! ila je mbona sisi hamtufanyii hivyo? haya tumeelewa kwamba nia leadership ego lkn a lida has to be model and not mbabe kwanini nyie wenzetu mnaweka ubabe?Mkuu gfsonwin na Wakuu wanawake wote naomba kutoa hoja;
Its a matter of leadership ego...we all have it presidents, ward secretaries, fathers, mothers and even brothers and sisters.
Aliye mkubwa kumuomba msamaha mdogo ni kama anaona credibility inashuka! Ndo maana hata madaktari na walimu wagomeje-viongozi hawawezi kuadmit their mistakes(which are many by the way), watatafuta tu kujisafisha kwa justification.
Mimi naamini justification ni mbaya sana ndo maana hata kwenye bible(my fav book.) watu wote walioambiwa dhambi zao wakaanza kujijustify Mungu aliwakataa kabisa! (Ref.. our father Adam, Cain, Saul)
Na waliotubu aliwapenda sana tu hadi kuwatajataja over the generations hata kama dhambi zao zilikua kubwa kiasi gani
Ref David (He comitted adultery, killed the womans husband and married her). Yet akasamehewa.
Inaudhi sana ukimwambia mtu kosa lake anaanza kufanya hivyo...Ila you are our wives so help saving us from the men we have become.
Pai kinadada na wake zetu mnakosea the way mnavyotuaproach na kutuambia makosa yetu. Kama ukimwambia mkiwa wawili chumbani kwa upole ni wachache sana watakaokuwa hivyo (Ambao kwa niaba ya wanaume wote naomba kuwaita mafisadi wa mahusiano.)
Nawasilisha
mgeni 10, hapa sijiongelei mimi, ila nimejaribu kuleta mada ambayo wengi wanapitia huko. kwa bahati wa kwangu huwa anakiri na kuomba samahani ila tu malipizi yake unakoma na wewe ujitahd usiwe mkosa.................Pole kwa hayo yaliyokukutaSi wanaume wote wako hivyo, Ni huyo Wako Tu PengineMuombee Sana ili awe vile upendavyo maana kwa Mungu yote yanawezekana
Nahisi wanaume kama mimi tumeonewa tu, mie hukiri makosa... hata nikiwa mlevi, mbushi, au nimekamatwa live nina "ndogo" huwa nakiri kosa ili nisamehewe na kupigania baby come back
kungwi kanionea sana
Haya ngoja nirudi pub maana maisha ya useja yalishanishinda
na kama moshi unavyoumiza macho ndani ya chumba cha jiko ndivyo ilivyo kuish na mwanaume mkorofi ndani ya nyumba.
Blaine we aare neva weak ma dia bro. women are very strong ila tu wababa nyie hamtaki kulikubali hilo. kama huamini mwambiemkeo asafiri ubaki home wewe na watoto ndipo utakapojua what i mean.(according to malezi) udhaifu sio sifa ya uanaume so hatutakiwi kuwa nayo. kuhusu mwanamke udhaifu inakubalika maana wao wapo chini yetu (according to malezi)
Kwani kuna undugu mzuri kuliko ule? Ushawahi angalia vizuri jinsi mambo yanavyokuwa? We acha tu! Kumbe tuko pamoja kama mpaka sehemu muhimu hatutofautiani
PetCash so kwa wababa yapendeza wakiambiliwa sirini eeh! ila je mbona sisi hamtufanyii hivyo? haya tumeelewa kwamba nia leadership ego lkn a lida has to be model and not mbabe kwanini nyie wenzetu mnaweka ubabe?
jamani uzuri wanawake wote humu jamvini tu wasikivu sana na hata Asprin na Mr Rocky wanajua hilo mkitumabia mnataka tunapowaambia makosa yenu tuwaambie mkiwaje basi sisi tutatii tu.
pia kuna kitu kimoja huwa kinanishangaza sana, wanaume walio wengi hasa kwenye ndoa siku mkewe akimwambia umekosea basi yeye moyoni husema leo atanitambua kitandani, basi akifika kwa bed yaaani utafikir sijui ndo nini ana kudo kama anakomoa na mkimaliza anasema kabisa tumeshafanya hivi ugomvi hakuna je hii ni halali? eti Bishanga wewe waona ni vyema kufanya hivi kwa mtazamo wako?