Wanaume wenye watoto tupeni uzoefu wenu. Mara ya kwanza unampelekea Mwanamke wako hospitali kujifungua, hiyo siku ilikuwaje?

Wanaume ambao mnawatoto embu tupeni uzoefu wenu kwa mara kwanza unampelekea Mwanamke wako hospitali kujifungua,hiyo siku ilikuwaje na kipi utoweza kusahau kabisa
Andaa chakula cha kutosha na kizuri kwa ajili ya mama na mtoto, uwe na nyumba nzuri, mtu wa kusaidia kupika na shughuli nyingine. Uwe na bunda la kutosha la hela kuanzia sasa na kuendelea manake hiyo sasa ni familia, hakuna tena mambo ya kula kwenye migahawa, nguo za kutosha na fedha za matibabu ziwe hapo. Hapo ndio maisha yanaanza mzee.
 
Siku ambayo sitakaa niisahau ni Ile alirudi klinik akasema hajahudumiwa mimba yake mpaka aende na mwenzie,wakati huo ina miezi mitatu.
Kidume nikatupia vest raba na jinsi nkamwambia utanikuta nje.
Msala ni pale nlivyofika clinik eti naambiwa lazima nipimwe ngoma maana mtoto hatakiwa apate vvu.Kumbuka mm ni wale walioapa kutopima ngoma mpaka mwisho Dunia ila sasa yamenikuta.
Unaambiwa nilivuja jasho kinoma wakati yule nesi anapima.Yaani anagusa gusa specimens halafu anatikisa kichwa Kwa masikitiko ilimradi tu mbwembwe.
Siku Ile nilipungua kilo sana siwezi sahau.
 
Picha limeanza saa tisa usiku,,baby mama uchungu umempata na kumbuka baby mama wangu hujifungua kwa operesheni

So mwelekeo ni muhimbili na ndio mtoto wangu wa kwanza,nipo makazi africana mbezi,,mungu mkubwa nje kuna nissan march kadogo kadogo hivi ndio nikakapiga start hao muhimbili,,yaan baby mama anaugulia maumivu mwamba namtaja Allah kwa sana na kumtukuza atufikishe salama

Dah ilikuwa experience ya kipekee sana
 
Uzazi wa pili Kipindi kile corona imepamba moto 2020 ingawa ilikua vyepesi sana lakini kidogo akili iliyumba.

Uzazi wa kwanza ndio sita sahau!
Kwanza kabisa hospitali ya jirani walisema uzazi wa kwanza lazima mwananyamala ama sinza.
Nikaomba sinza tukaelekezwa maana tulikuwa wa geni dar, hatuna mwenyeji hata mmoja.
tukaenda, kipimo tukaambiwa kurudi tarehe fulani, siku hio tulivyorudi nikaambia anabaki nirudi nikaandae chakula na vinginevyo, bahati nzuri tulipewa abc za kujifungua so vifaa alikuwa navyo.
Siku ya kwaza ikakata, siku ya pilli nayo ikakata!
Nikashauriwa na daktari kwamba njia imekataa kufunguka inatakiwa dawa fulani kama kumbukumbu ziko vizuri ni dinoproston, bei 50,000 kidonge kimoja! Nilizunguka mji wa dar es laam karibu kila famasia hio dawa hamna, siku inayofuata nikarudi pale namwambia ness nimekosa akanijibu ongea na watu vizuri dawa ipo hapa hapa lete hela nikuchulie!
Nusu saa nyingi dawa ikapatikana!
Akapewa dawa hata haikusaidia, siku ya nne ikaisha , siku ya tano asubuhi na fika pale mtu wa kwanza naulizia mapokezi pale nikaambiwa bado, mwanamke alishuka gorofani maana sehemu ya kujifungulia pale sinza ipo juu, ile tunakutana alikua ana lia! Nilijikaza kiume ingawa machozi yalikua yananilenga mno! Tulivyo achana nisiseme uongo nilitoka nje nikalia kwa kweli! Akaja mama mmoja simjui ila alisha nisoma, akanipeleka kwenye mgahawa akanunua chai akanipa, akaniambia wewe ni mwanaume kuwa mwanaume!

Nikarudi nyumbani kuandaa chakula jioni nikaenda tena hali ni ile ile.

Mungu ni mwema asubuhi siku ya sita saa 12 asubuhi nafika pale nikajitambulisha nikaambiwa panda juu, kufika naonyeshwa mtoto mama bado hakaa sawa katika operation dakika kumi zilizopita, nilishukuru aisee mtoto wa kiume uzito kg 4.2.
 
Uzazi wa pili Kipindi kile corona imepamba moto 2020 ingawa ilikua vyepesi sana lakini kidogo akili iliyumba.

Uzazi wa kwanza ndio sita sahau!
Kwanza kabisa hospitali ya jirani walisema uzazi wa kwanza lazima mwananyamala ama sinza.
Nikaomba sinza tukaelekezwa maana tulikuwa wa geni dar, hatuna mwenyeji hata mmoja.
tukaenda, kipimo tukaambiwa kurudi tarehe fulani, siku hio tulivyorudi nikaambia anabaki nirudi nikaandae chakula na vinginevyo, bahati nzuri tulipewa abc za kujifungua so vifaa alikuwa navyo.
Siku ya kwaza ikakata, siku ya pilli nayo ikakata!
Nikashauriwa na daktari kwamba njia imekataa kufunguka inatakiwa dawa fulani kama kumbukumbu ziko vizuri ni dinoproston, bei 50,000 kidonge kimoja! Nilizunguka mji wa dar es laam karibu kila famasia hio dawa hamna, siku inayofuata nikarudi pale namwambia ness nimekosa akanijibu ongea na watu vizuri dawa ipo hapa hapa lete hela nikuchulie!
Nusu saa nyingi dawa ikapatikana!
Akapewa dawa hata haikusaidia, siku ya nne ikaisha , siku ya tano asubuhi na fika pale mtu wa kwanza naulizia mapokezi pale nikaambiwa bado, mwanamke alishuka gorofani maana sehemu ya kujifungulia pale sinza ipo juu, ile tunakutana alikua ana lia! Nilijikaza kiume ingawa machozi yalikua yananilenga mno! Tulivyo achana nisiseme uongo nilitoka nje nikalia kwa kweli! Akaja mama mmoja simjui ila alisha nisoma, akanipeleka kwenye mgahawa akanunua chai akanipa, akaniambia wewe ni mwanaume kuwa mwanaume!

Nikarudi nyumbani kuandaa chakula jioni nikaenda tena hali ni ile ile.

Mungu ni mwema asubuhi siku ya sita saa 12 asubuhi nafika pale nikajitambulisha nikaambiwa panda juu, kufika naonyeshwa mtoto mama bado hakaa sawa katika operation dakika kumi zilizopita, nilishukuru aisee mtoto wa kiume uzito kg 4.2.
Hongera sana mkuu wewe ni mume bora kabisa. Utakuwa baba bora pia.

Umenikumbusha kipindi changu, baba watoto alivyokuwa na heka heka safari za hospital -nyumbani kama zote. Akirudi nyumbani kufuata chakula akikuta mdada anazubaa zubaa anaingia jikoni mwenyewe anapika (ndio nilijua kumbe anajua kupika😂😂😂).
 
Nakumbuka nlimpelekea shemeji yangu msosi akiwa anakaribia kujifungua(tulikua tunaheshimiana sana) sasa nmefika nkamkuta ameambiwa na manesi atembee tembee huko njee, nikamfata nkamsalimu nkamwambia nmekuletea chakula.
Cha ajabu akanijibu kwa hasira "CHAKULA NDIO NINI?"
Nlishikwa na asira nkamfata nesi nkamkabidhi kile chakula nkampa na teni.... sikukanjaga tena wodi ya mama wajawazito mpaka leoo...
 
Mke wangu uchungu ilianza saa kumi na moja jioni kuamkia mwaka mpya 1999/2000 tukaenda hospitali saa moja kufika saa kumi ngoma bado,akaitwa daktari Bingwa akaamuru niondoke .
Natoka nje ya hospital jasho jembamba likinitoka watu wako kwenye kusheherekea mwaka mpya mie nalia machozi ,saa kumi na mbili daktari ambaye ni schoolmate anatoka nje ya hospitali ananiambia kamuangalia Binti yako mpya.
Inaogofya Ile miye leo ni Babu wa watoto wake wawili
 
Nilirud usiku chicha bovu, nikamkuta wife amekaa kwa kochi akaniambia chupa imepasuka, simply nikamuambia tutanunua nyingine. Nikaingia bafuni nikaoga nikalala, kustuka simuoni kitandani nikamfuata sebleni nikamuuliza chupa ikipasuka ndo hulali?

Nikarud nikapiga mbonji asubui ndo akanielewasha vzr ikabid tukimbilie BOCHI hospital na uchungu ukawa unekolea tumefika mapokezi wakamuambia twende Moja kwa Moja kwa Dr (Mbaga, tumefika kwake anasema hawez mpokea bila usajili nikarud kusajili narud kwa Dr eti ametika kaenda kunywa chai. Nikamuibukia canteen nikamuwashia moto wa kutosha na kumkunja juu.

Akarud kumpima ajakuta njia umegoma kufunguka yote thus aka rule operation, begi la vifaa tumeacha home. Ikabid ni rush home nimechukua narud mvua ilikua imenyesha na barabara Ina udongo mfinyanzi gari ika acha njia ikagongq nguzo ya umeme. Nimefika hosp wife kashaingiq kwenye upasuaji.

Saa 9:12 nikapata mtoto wa kwanza na saa 9.15 nikapata mtoto wa pili zen ni kawa baba kwa mara ya kwanza .
 
Picha limeanza saa tisa usiku,,baby mama uchungu umempata na kumbuka baby mama wangu hujifungua kwa operesheni

So mwelekeo ni muhimbili na ndio mtoto wangu wa kwanza,nipo makazi africana mbezi,,mungu mkubwa nje kuna nissan march kadogo kadogo hivi ndio nikakapiga start hao muhimbili,,yaan baby mama anaugulia maumivu mwamba namtaja Allah kwa sana na kumtukuza atufikishe salama

Dah ilikuwa experience ya kipekee sana
hujifungua kwa opereshen alafu mnasubiria mpaka uchungu umkamate hebu muwe mnajiongeza
 
Back
Top Bottom