Mkuu Belo, swali lako ni la msingi sana.
Nimekuwa nikijaribu kutafakari tangu nilipoiona thread hii mara ya kwanza (jana), kwa lengo la kutaka kuona ni kiasi gani ususiaji wa Vodacom unaweza kusaidia katika kuleta ufanisi wa mapambano dhidi ya ufisadi. Nataka kusema ninapoandika leo kujaribu kuchangia, ninakuwa nimejiridhisha kabisa kuwa naelewa mantiki nzima ya madhara v/s faida ya kususia Vodacom (hasa kwa lengo la kumkomoa mtu mmoja au wawili) kwa sababu zozote tunazoweza kubuni.
Kwa manufaa ya mjadala, ningependa kubainisha madhara machache halafu tuyalinganishe na sababu zilizotolewa na baadhi ya watu kuhalalisha kususia Vodacom.
- Vodacom inachangia maendeleo ya nchi kwa kulipa Kodi: Hulipa kodi zote inzotakiwa kulipa (PAYE za wafanyakazi wao, SDL, VAT etc). Kususia kutumia bidhaa zao kutasababisha kodi itokanayo na operation zao kushuka na hata kupotea kabisa kama wataamua kufunga biashara yao kutokana na hasara watakayoipata
- Vodacom inaajiri waTanzania: Japokuwa idadi kamili ya wafanyakazi wa Vodacom sinayo, inakadiriwa kuwa imeajiri zaidi ya waTanzania 600 nchi nzima. Wafanyakazi hawa hupata nafasi ya kuendeleza taaluma zao (kupitia training, na on-site experience, exposure to technology etc). Vile vile, hulipwa mafao yao vizuri na kuweza kujikimu wao na familia zao. Kwa kuwa na kipato hicho, wafanyakazi hao pia huchangia jitihada mbalimbali za kijamii wanazokabiliana nazo. Kwa ajira hiyo pia, waTanzania wenzetu hawa wanapata nafuu ya kisaikolojia itokanayo na kupata fursa za kujishughulisha.
- Misaada na michango ya jamii: Vodacom kama baadhi ya taasisi nchini, hushiriki katika kuchangia michezo, taaluma, afya, na mambo mengine mengi. Vodacom ikisusiwa, uwezo wake wa kusaidia jamii utapungua na hatimiye kuweza kupotea kabisa.
- Wadau wengine: Vodacom hutumia kampuni nyingi ndogo na kubwa za watanzania katika kupata huduma zake mbalimbali. kuna kampuni zinazotumika kuwafungia mitambo, kujaza mafuta (diesel) kwenye generators zilizopo kwenye vituo vyao (BTS sites), kuna wanaosambaza vouchers (wako wengi zaidi), sim Cards, wanaopata kazi za kutangaza biashara zao, kuna wanaofanya usafi kwenye maeneo ambayo hutumiwa na kampuni hiyo, n.k. Idadi ya wadau wanaopata kipato kupitia Vodacom ni kubwa. Vodacom ikisinyaa, nao watasinyaa.
- Hudama waitoayo. Pamoja na wengi kubainisha kuwa huduma za Vodacom ni ghali, lakini inaelekea inapata wateja wengi zaidi kuliko kampuni zinazotoza viwango vidogo zaidi. Kwa mtazamo wangu ni kuwa, kinachotakiwa na wateja wa Vodacom si u-ghali wa huduma bali ni ubora wake. Nadhani tutakubaliana wote kuwa huduma za simu za mkononi ni chachu kubwa ya maendeleo ya nchi yetu. Huduma hizi zinasaidia kuharakisha na kurahisisha mawasiliano na kufanikisha matumizi bora ya muda (time management). Vodacom ikishindwa ku-operate, si tu kwamba wananchi wengi watapata shida kwa kukosa huduma hizo katika baadhi ya sehemu walipo, bali pia ushindani wa kibiashara utapungua na hivyo kampuni nyingine kuongeza bei za huduma au kubweteka katika kutoa huduma hizo au kuzorota kwa mambo mengine. Kumbukeni Tritel na mtandao uliokuwa ukiishia Kimara.
Kuna mengi yenye manufaa kwa kuwa na Vodacom. Vodacom kama zilivyo kampuni nyingine nchini, haziwezi kukua/kustawi na kuweza kushiriki katika harakati za kuinua uchumi wetu kama hazitakuwa na mafanikio katika biashara zao. Na mafanikio yao yatatokana na ushirikiano kati yao na wadau wote pamoja na wateja wao popote walipo. Nchi hii haiwezi kukua kwa kususia bidhaa.
Kuisusia Vodacom ni uthibitisho tosha kabisa kwamba tutakuwa tunataka kushindwa kujikwamua kiuchumi na kijamii kwa kudhoofisha mdau muhimu katika kukuza uchumi wetu. Kuisusia Vodacom kutaanzisha hofu kwa kampuni nyingine zote. Na wao wataanza ku-invest kwa uangalifu wakitegemea kususiwa wakati wowote na hivyo kuwaingiza kwenye hasara.
Kususia Vodacom au kampuni nyingine yoyote ya simu hakuwezi asilani kumnyima sana usingizi mwekezaji aliewekeza katika kampuni hiyo. Kwani kadiri atakavyoona trend ya profit inabadilika, atahamisha share zake kwenye operation nyingine inayolipa zaidi na kufunga virago. Wakuu, wawekezaji huwa hawasubiri kula hasara kabla ya kuamua hatua za kuchukua kuokoa rasilimali zao. Na huchukua hatua kwa haraka ajabu.
Kwa kumalizia tu, nadhani thread hii ni ya hatari sana kwa ustawi wa Taifa letu. Ni thread ya aibu kwa uzaleno wa nchi yetu na inatia hofu kuhusu ukweli wa kuwa tunaitakia mema nchi hii.
Naomba nieleweke tu kwamba niliyoyasema hapo juu ni imani yangu na inaweza kuwa na mapungufu. Ila ileweke pia kuwa sina affiliation ya aina yoyote na Vodacom zaidi ya kuwatakia heri kama ninavyowatakia wawekezaji wengine nchini.
Recta!
Wacha ngonjera!!
Huo wimbo wa ajira na kodi hautaingia akilini bila ya kutoa takwimu! Come straight lay out the CIP of Vodacom utueleze wliwekeza shilingi ngapi? How much kodi wamelipa in the name of VAT kwa miaka yao and the rest and how much wamegawana na mafisadi wa CCM! Na ngapi zimekwenda kwa bibi!!
The peanut donations ni danganya toto its only the cost of sms for a few days ila kwa sababu wewe hujui unaona kivuno!!
Kama ita click in my head I go with you bus otherwise mimi sipandi basi la wajinga recta!!! Hata kama umetumwa na ccm kuwatetea lakini Voda ni ufisadi per se come sun come rain ila wewe kula hiyo pombe chafu ya msimbazi humpati mtu makini !!but as usual 90% ya waTZ kondoo wako behind you mpaka utumbukie!!