Wanaharakati: Ziachieni simu za VodaCom!

Wanaharakati: Ziachieni simu za VodaCom!


Mkuu Belo, swali lako ni la msingi sana.

Nimekuwa nikijaribu kutafakari tangu nilipoiona thread hii mara ya kwanza (jana), kwa lengo la kutaka kuona ni kiasi gani ususiaji wa Vodacom unaweza kusaidia katika kuleta ufanisi wa mapambano dhidi ya ufisadi. Nataka kusema ninapoandika leo kujaribu kuchangia, ninakuwa nimejiridhisha kabisa kuwa naelewa mantiki nzima ya madhara v/s faida ya kususia Vodacom (hasa kwa lengo la kumkomoa mtu mmoja au wawili) kwa sababu zozote tunazoweza kubuni.

Kwa manufaa ya mjadala, ningependa kubainisha madhara machache halafu tuyalinganishe na sababu zilizotolewa na baadhi ya watu kuhalalisha kususia Vodacom.


  1. Vodacom inachangia maendeleo ya nchi kwa kulipa Kodi: Hulipa kodi zote inzotakiwa kulipa (PAYE za wafanyakazi wao, SDL, VAT etc). Kususia kutumia bidhaa zao kutasababisha kodi itokanayo na operation zao kushuka na hata kupotea kabisa kama wataamua kufunga biashara yao kutokana na hasara watakayoipata
  2. Vodacom inaajiri waTanzania: Japokuwa idadi kamili ya wafanyakazi wa Vodacom sinayo, inakadiriwa kuwa imeajiri zaidi ya waTanzania 600 nchi nzima. Wafanyakazi hawa hupata nafasi ya kuendeleza taaluma zao (kupitia training, na on-site experience, exposure to technology etc). Vile vile, hulipwa mafao yao vizuri na kuweza kujikimu wao na familia zao. Kwa kuwa na kipato hicho, wafanyakazi hao pia huchangia jitihada mbalimbali za kijamii wanazokabiliana nazo. Kwa ajira hiyo pia, waTanzania wenzetu hawa wanapata nafuu ya kisaikolojia itokanayo na kupata fursa za kujishughulisha.
  3. Misaada na michango ya jamii: Vodacom kama baadhi ya taasisi nchini, hushiriki katika kuchangia michezo, taaluma, afya, na mambo mengine mengi. Vodacom ikisusiwa, uwezo wake wa kusaidia jamii utapungua na hatimiye kuweza kupotea kabisa.
  4. Wadau wengine: Vodacom hutumia kampuni nyingi ndogo na kubwa za watanzania katika kupata huduma zake mbalimbali. kuna kampuni zinazotumika kuwafungia mitambo, kujaza mafuta (diesel) kwenye generators zilizopo kwenye vituo vyao (BTS sites), kuna wanaosambaza vouchers (wako wengi zaidi), sim Cards, wanaopata kazi za kutangaza biashara zao, kuna wanaofanya usafi kwenye maeneo ambayo hutumiwa na kampuni hiyo, n.k. Idadi ya wadau wanaopata kipato kupitia Vodacom ni kubwa. Vodacom ikisinyaa, nao watasinyaa.
  5. Hudama waitoayo. Pamoja na wengi kubainisha kuwa huduma za Vodacom ni ghali, lakini inaelekea inapata wateja wengi zaidi kuliko kampuni zinazotoza viwango vidogo zaidi. Kwa mtazamo wangu ni kuwa, kinachotakiwa na wateja wa Vodacom si u-ghali wa huduma bali ni ubora wake. Nadhani tutakubaliana wote kuwa huduma za simu za mkononi ni chachu kubwa ya maendeleo ya nchi yetu. Huduma hizi zinasaidia kuharakisha na kurahisisha mawasiliano na kufanikisha matumizi bora ya muda (time management). Vodacom ikishindwa ku-operate, si tu kwamba wananchi wengi watapata shida kwa kukosa huduma hizo katika baadhi ya sehemu walipo, bali pia ushindani wa kibiashara utapungua na hivyo kampuni nyingine kuongeza bei za huduma au kubweteka katika kutoa huduma hizo au kuzorota kwa mambo mengine. Kumbukeni Tritel na mtandao uliokuwa ukiishia Kimara.

Kuna mengi yenye manufaa kwa kuwa na Vodacom. Vodacom kama zilivyo kampuni nyingine nchini, haziwezi kukua/kustawi na kuweza kushiriki katika harakati za kuinua uchumi wetu kama hazitakuwa na mafanikio katika biashara zao. Na mafanikio yao yatatokana na ushirikiano kati yao na wadau wote pamoja na wateja wao popote walipo. Nchi hii haiwezi kukua kwa kususia bidhaa.

Kuisusia Vodacom ni uthibitisho tosha kabisa kwamba tutakuwa tunataka kushindwa kujikwamua kiuchumi na kijamii kwa kudhoofisha mdau muhimu katika kukuza uchumi wetu. Kuisusia Vodacom kutaanzisha hofu kwa kampuni nyingine zote. Na wao wataanza ku-invest kwa uangalifu wakitegemea kususiwa wakati wowote na hivyo kuwaingiza kwenye hasara.

Kususia Vodacom au kampuni nyingine yoyote ya simu hakuwezi asilani kumnyima sana usingizi mwekezaji aliewekeza katika kampuni hiyo. Kwani kadiri atakavyoona trend ya profit inabadilika, atahamisha share zake kwenye operation nyingine inayolipa zaidi na kufunga virago. Wakuu, wawekezaji huwa hawasubiri kula hasara kabla ya kuamua hatua za kuchukua kuokoa rasilimali zao. Na huchukua hatua kwa haraka ajabu
.

Kwa kumalizia tu, nadhani thread hii ni ya hatari sana kwa ustawi wa Taifa letu. Ni thread ya aibu kwa uzaleno wa nchi yetu na inatia hofu kuhusu ukweli wa kuwa tunaitakia mema nchi hii.

Naomba nieleweke tu kwamba niliyoyasema hapo juu ni imani yangu na inaweza kuwa na mapungufu. Ila ileweke pia kuwa sina affiliation ya aina yoyote na Vodacom zaidi ya kuwatakia heri kama ninavyowatakia wawekezaji wengine nchini.



Recta!

Wacha ngonjera!!

Huo wimbo wa ajira na kodi hautaingia akilini bila ya kutoa takwimu! Come straight lay out the CIP of Vodacom utueleze wliwekeza shilingi ngapi? How much kodi wamelipa in the name of VAT kwa miaka yao and the rest and how much wamegawana na mafisadi wa CCM! Na ngapi zimekwenda kwa bibi!!
The peanut donations ni danganya toto its only the cost of sms for a few days ila kwa sababu wewe hujui unaona kivuno!!

Kama ita click in my head I go with you bus otherwise mimi sipandi basi la wajinga recta!!! Hata kama umetumwa na ccm kuwatetea lakini Voda ni ufisadi per se come sun come rain ila wewe kula hiyo pombe chafu ya msimbazi humpati mtu makini !!but as usual 90% ya waTZ kondoo wako behind you mpaka utumbukie!!
 
It is too late now but not too late enough.. kama uko kwenye mapambano dhidi ya ufisadi na hauko tayari kusalimu amri, nakushauri kuachilia namba za simu za Vodacom ASAP. As a matter of fact, hamia "kwingine" within the next 72 hours (beginning Monday). Do it or be ready to live with the consequences.

Nilikuwepo.

M.M.

Mkuu,

Ni wazo zuri. Ila naona hasara zake zitakua kubwa kuliko faida.

Binafsi sidhani kama hii mbinu hapa ndo mahali pake. Nijuavyo, hii mbinu ya kususia bidhaa/huduma za kampuni inatumika pale inapokuwa imethibitishwa kwamba shuguli za kampuni husika zinaathiri kwa kiasi kikubwa jamii flani au mazingira. Kwa mfano kampuni ya DeBeers inaponunua almasi kutoka kwa waasi/nchi zisizo na usalama (conflict zones) inakua inafadhili moja kwa moja mauaji na uhalifu mwingine wa kivita huko Sierra Leone na nchi zingine za Africa. Wanaharakati na wanamazingira walipoona haya walihamasisha wanunuzi wa almasi wasinunue bidhaa za DeBeers mpaka watakapojiridhisha kwamba hizo bidhaa/almasi hazijatoka kwenye maeneo yenye migogoro ya kisiasa/conflict zones. Hakika hii kampeni imefanikiwa.

Tukirejea nyumbani, sidhani kama ni muafaka kufananisha Vodacom na DeBeers. Wananchi wanaonufaika kwa huduma na ajira za Vodacom ni wengi. Isitoshe watuhumiwa wa ufisadi wanaomiliki hisa Vodacom ni "minority interest", japo mtaji wao si haba. Hivyo basi, mimi naona hoja ya kususia bidhaa za Vodacom kwavile baadhi ya wanahisa wanatuhumiwa kwa ufisadi ni hoja dhaifu.

Tuendelee kupambana na ufisadi kwa njia za kisheria na kisiasa. Tukipiga vita watuhumiwa binafsi, wataanguka lakini nafasi zao zitachukuliwa na wengine. Tukiupiga vita mfumo wa kifisadi na tukaushinda, basi hata watu binafsi wanaonufaika na mfumo wataangamia na kuisha.
 
Any developments here with this very useful thread. Au tunasubiri bado masaa 24 yaliyobaki? Sijui au pengine yameisha.
 

Mkuu Belo, swali lako ni la msingi sana.

Nimekuwa nikijaribu kutafakari tangu nilipoiona thread hii mara ya kwanza (jana), kwa lengo la kutaka kuona ni kiasi gani ususiaji wa Vodacom unaweza kusaidia katika kuleta ufanisi wa mapambano dhidi ya ufisadi. Nataka kusema ninapoandika leo kujaribu kuchangia, ninakuwa nimejiridhisha kabisa kuwa naelewa mantiki nzima ya madhara v/s faida ya kususia Vodacom (hasa kwa lengo la kumkomoa mtu mmoja au wawili) kwa sababu zozote tunazoweza kubuni.

Kwa manufaa ya mjadala, ningependa kubainisha madhara machache halafu tuyalinganishe na sababu zilizotolewa na baadhi ya watu kuhalalisha kususia Vodacom.


  1. Vodacom inachangia maendeleo ya nchi kwa kulipa Kodi: Hulipa kodi zote inzotakiwa kulipa (PAYE za wafanyakazi wao, SDL, VAT etc). Kususia kutumia bidhaa zao kutasababisha kodi itokanayo na operation zao kushuka na hata kupotea kabisa kama wataamua kufunga biashara yao kutokana na hasara watakayoipata


Inasemekana kuwa hawa hawajalipa kwa kipindi kirefu kodi ya makampuni na hata kulikuwa na utata kuhusu ulipaji wao wa VAT.
Je unaweza kutuwekea data hapa kwa miaka mitano ya nyuma kwa mafanikio haya unayonadi hapa, wamelipa PAYE kiasi gani, Corporation tax kiasi gani, VAT kiasi gani, tax zitokanazo na importation yao ya vitu mbalimbali walilipa kiasi gani? Vinginevyo ni porojo zile zile tunazoletewa na kuzisikia toka kwa promoters wa mafisadi huku zikiwa hazina chembe za ukweli ili kututamanisha ushirika na wezi wakubwa hawa.
 
Kwani issue hapa ni kususia huduma za voda au ni suala kujihami na la kiusalama zaidi kwa wale wanaharakati hususan wanaotumia mtandao wa vodacom...?

Ni vigumu kumuelewa Mwanakijiji kwa kua hajaweka complete information ni kama kitendawili na watu wanajaribu kutegua which kwa maoni yangu in the forum like this angetakiwa awe muwazi zaidi toka mwanzo ili watu waweze kuchambua hoja yake vizuri... but kuna mwanachama mmoja ametoa ushauri kwa mamlaka husika ziangalie suala la privacy kwenye mambo ya simu hasa za mkononi kwamba kwa sasa office ya IGP, DCI, TISS wana uwezo wa kusikiliza chochote kinachoongelewa na watu wanaotumia mtandao wa Vodacom, so kwa kuangalia hilo labda Mwanakijiji anajaribu kutuambia/kuwaambia wanaharakati wa ufisadi kua wawe makini na hasahasa waachane na hizo line sababu zinaweza zikawapa hawa watu sehemu nzuri ya kuanzia katika mapambano yao na watu wanaopambana na ufisadi....( may be hivyo vyombo hapo juu navyo ni vibaraka wa ufisadi)

.... but hayo ni mawazo yangu tu na najaribu kuuweka huu mjadala kwenye upande huo zaidi.... lakini mtenguaji wa kitendawili hiki ni Mwanakijiji na nadhani sasa ameshapata miji mingi na niwakati wake sasa wakukitegua na kueleza alikua na maana gani kuanzisha hii thread.. (may be siko mbali na ukweli)
 
We ndugu uko nchi gani? Tunaomba usituletee udini hapa. Tanzania si taifa la kiislamu kususia bidhaa za Israel. Be carefull usituletee laana katika taifa letu.
Taratibu, taratibu, usilete jazba. Tunazungumza kiungwana humu ndani. Kwa taarifa yako mimi sio Muislam, ni Mkristo aliyezaliwa na kulelewa katika familia ya Kikristo, na nitakuwa Mkristo daima. Naona suala la Israel linawachanganya wengi. Israel ya Biblia na serikali ya Israel ya Netanyahu ni vitu viwili tofauti. Sina haja ya kutoa somo hapa zaidi, lakini kwa kifupi uelewe hivyo. Wapingao sera za serikali ya Israel sio Waislamu tu, bali binadamu wote popote pale walipo wapendao usawa na ubinadamu. Kutetea sera za serikali ya Israel za ukoloni, unyanyasaji na ubaguaji haukufanyi wewe uwe Mkristo bora.

Kwa taarifa yako, kama ulikuwa huna habari, sio wote ambao tupo JF tunaishi Tanzania. Tumesambaa ulimwenguni mwote...lakini bado tu Watanzania. Kwa hiyo, wakati wowote utakapotokea ufisadi wa aina yoyote tutapiga kelele, maana huko Tanzania bado wapo ndugu zetu, mama, baba mjomba, shangazi etc. ambao maisha yao yanazidi kuwa duni kutokana na ufisadi mkubwa ambao unaendela kushamiri.

Utaipata laana kama utalala usingizi mzito wakati binadamu wenzako wanateseka. Kama unafanya hivyo, ndugu yangu, laana ulishaipata zamani.
 


Recta!

Wacha ngonjera!!

Huo wimbo wa ajira na kodi hautaingia akilini bila ya kutoa takwimu! Come straight lay out the CIP of Vodacom utueleze wliwekeza shilingi ngapi? How much kodi wamelipa in the name of VAT kwa miaka yao and the rest and how much wamegawana na mafisadi wa CCM! Na ngapi zimekwenda kwa bibi!!
The peanut donations ni danganya toto its only the cost of sms for a few days ila kwa sababu wewe hujui unaona kivuno!!

Kama ita click in my head I go with you bus otherwise mimi sipandi basi la wajinga recta!!! Hata kama umetumwa na ccm kuwatetea lakini Voda ni ufisadi per se come sun come rain ila wewe kula hiyo pombe chafu ya msimbazi humpati mtu makini !!but as usual 90% ya waTZ kondoo wako behind you mpaka utumbukie!!


Mkuu Mkereme, naheshimu mawazo yako.

Hizo takwimu nadhani unaweza kuzitafuta mwenyewe.

Haikuwa nia yangu na wala sio lengo la post yangu kuanika takwimu za uchangiaji wa Vodacom katika pato la Taifa kwa namna yoyote. Mkuu, sikuwa na haja ya kufanya hivyo kwani sio jukumu langu na pia ni dhahiri hata takwimu halisi zikitolewa zinaweza kuonyesha uchangiaji mkubwa zaidi ya ninavyoweza kuupata. Ni kazi ya mamlaka husika kufuatilia kama zinaona zinakosa mapato yoyote yanayotegemewa. Vile vile zinaweza kuanika ukwepaji wowote wa kodi wanaoweza kuubaini.

Ninachotaka kusema ni ukweli kuwa UFISADI hauwezi kuondolewa kwa kuua uwekezaji (wa ndani na/au wa nje). Sioni sababu wala faida zitazopatikana kama tamaa yetu itabaki kuwa Vodacom ife. Ususiaji wa namna hiyo ni UFISADI mkubwa zaidi ya ule tunaojaribu kupambana nao. Maana UFISADI huo unaua nguvu yoyote ambayo Taifa linaweza kuwa nayo.

Mkereme, Mimi si mfanyakazi, mwekezaji wala mtu yeyote mwenye interest ndani ya Vodacom. Vile vile, mimi siwezi kutumwa na chama cha siasa kutetea niliyoandika hapo juu. Niliyoyaandika ni imani yangu (si ya kisiasa) kuhusu uwekezaji wa Vodacom nchini na umuhimu wa ustawi wa kampuni kama hizo.

Ukweli ni kwamba, kukimbilia umasikini haiwezi kuwa dawa/silaha ya kupambana na ufisadi wala suluhu ya matatizo yoyote tuliyonayo. Haihitaji jitihada sana kujua hilo.
 
Kama ndo hivyo basi angewapelekea hao wanaharakati kwenye private mail zao.

Nnavyofahamu ukishabandika thread basi unaalika wanajamii wote waijadili.

Yes, lakini haina maana kwamba we kila unalolisoma hapa basi unalichukulia kama amri kumi za Mungu, chuja tafakari ondoka na yanayo faa, ndiyo maana hiki ni kisima cha great thinker, just think about it and adjudicate, afterall the decision is yours!

But as for me.. I say No to 'VODAMAFISDI COM'
 
Voda doesnt need u.. thats the thing... And u cannot harm it in that fashion. Nikama panzi kusimama mbele ya tembo nakusema "hupiti hapa leo" its just STUPID!
 
Hivi ile ultimatum ya 72hrs bado haijapita? Mwanakijiji tunasubiri kufafanuliwa what will happen kabla hatujatupa line zetu za Vodacom.
 
mwanakijiji njoo uwaambie wanaharakati ambao hawakupata ujumbe wako wa kutupa line za voda nini kimewatokea baada ya yale masaa 72 kupita
 
Nadhani hayo masaa 72 yana karibia kuisha. Ngoja tuone kita kacho tokea.
 
usingoje sana ndugu yangu; yawezekana "usione" chochote kwani si vyote vinaonekana.
Asante MMKJJ, kama sio vya kuonekana, maana wengine wetu ambao sio wanaharakati, hukututendea haki kutoonya, vitisho na altimatum ya kuihama voda bila kutoa sababu za msingi, we were a bit disturbed na katuacha na maswali bila majibu kuhusu nia yako halisi.
Hata hivyo asante kwa angalizo, tunajiendelezea zetu na voda yetu, huku tukikamuliwa na kufa kizungu na tai shingoni.
 
Asante MMKJJ, kama sio vya kuonekana, maana wengine wetu ambao sio wanaharakati, hukututendea haki kutoonya, vitisho na altimatum ya kuihama voda bila kutoa sababu za msingi, we were a bit disturbed na katuacha na maswali bila majibu kuhusu nia yako halisi.
Hata hivyo asante kwa angalizo, tunajiendelezea zetu na voda yetu, huku tukikamuliwa na kufa kizungu na tai shingoni.

ndugu yangu nimesema "yawezekana".. sijui what will happen or how.. ninachojua ni kuwa something will happen. Nimeangalia sana watu wanachosema na kujaribu kuhisi kwanini nimesema nilichosema. Well.. I wish I could give more info but Ican't isipokuwa aliyepewa ujumbe kaupata.
 
Gharama za huduma za voda ndicho kilio cha watu wengi, anayeshauri kuachana na vidacom nia yake ni nzuri. Hiki kilio kitawafikia vodacom na kuwafanya watakakari upya. Huwezi ukauumiza umma kwa bei mbaya za huduma kisha unyamaziwe kwa sababu umeajili watanzania. HAPANA
 
Mkuu Mkjj naomba ufafanuzi ni wanaharakati gani unaozungumzia? Wanaharakati is a broad term. Mimi ambao ni mwanaharakati wa mazingira kwanini nitupe line? Na wale ambao ni wanaharakati wa haki za binadamu je?
 
Back
Top Bottom