Wanafunzi hawa waliopata zero wanaenda wap?

Wanafunzi hawa waliopata zero wanaenda wap?

Tatizo lako unashindwa kuelewa umuhimu wa kuelimika au kuwa na jamii iliyosoma. Hakuna kitu kigumu na cha hatari kama kuwa na jamii isiyo na elimu. Hata kuishi mitaani vizuri ni rahisi ukiwa umeelimika kuliko kuwa mbumbumbu..
Ni vema kuelimika lakini Akili ni muhimu pia! Kuna wasomi wanafanya mambo ya ajabu kweli hata ukiwasikiliza ni pointless!
 
Mkuu umeongea point, Ujue watanzania wengi bado tunaamini Div 1 ni tikite ya mtu kufanikiwa kwenye maisha, yaani ameisha toboa maisha,
Kabisa. Kwa sasa Division ni 'Connection' hapa mjini. Ukiwa na koneksheni mambo yanaweza kwenda ahueni.
 
Hao ni kati ya wale waliokuwa na matazamio (ambitious) kwa mambo yaliyo nje ya uwezo wao na hawakukubaliana na Ukweli kwamba maisha sio lelemama (sio mtelezo)au sio matamu kama pipi. Ndo hao wanapata msongo wa mawazo (stress) akingali ni kijana mdogo (kiumri) hajaoa na hana maono(Vision). Ukimwuliza unataka uwe nani katika Jamii, utamsikia anabwatuka "nataka niwe kama Lissu" Hahahaaa. halafu nijenge bonge la nyumba huko Bunju.....
Kabisa, na ndio wamejaa mtaani.
 
😭😭😭😭
 

Attachments

  • Pyramid-Shape.jpg
    Pyramid-Shape.jpg
    15.7 KB · Views: 6
Tuletee tajiri asiye msomi tukufungulie Bibliography yake. Wakinga tu na waha ndo matajiri wasio wasomi kwa sababu ya kutajirika kwa ndumba na madawa kama kina Sandaland wa Kariakoo. Matajiri wasio na akili wala nidhamu

Leta hao wasio na elimu
Ila mkuu kwenye kila mafanikio ya mtu kuna siri kubwa sanaa so bora tukomee hapo
 
Tofauti mbona ni kubwa ukipata 4 nzuri unaenda chuo unaanza cheti diploma then degree ila alopata 0 hawezi kwenda chuo na Cheti Hana mpaka aresit
Duuh bas kazi ipoo. Lol.
 
Kwahiyo mwenye "D" zote na "C" mbili atleast akapata division 4 ya point 26 ambayo anaweza kwenda chuo au kusoma kidato cha tano (5) huku ana-reseat ni sawa na wenye "F" zote?! we vipi?!

Division 0 maana yake ni Failure!.. ni kama la saba tu wala haesabiki kwenye kundi la waliosoma sekondari. (Huyu kapoteza muda tu..., yaan alienda kukua,kujifunza uhuni wa kijinga, kupata mademu, mabwana na kupata washkaji na kuvuta bange basi!)

Division 4 hana ufaulu wa kwenda kidato cha tano ila anaweza kusoma mambo mengine au kurudia shule na akafanya vizuri.
uko bitter sana na mie, vipii kwani nimekugusaa? Si unge comment kwa kutulia mbna km unanichambaaa?? Wee shost nijie taratibuu. Lol
 
Nakumbuka kama niliwahi kupendekeza kuwa, kuwe na vyuo vya ufundi vya VETA kwa kila wilaya TANZANIA Bara, na pengine kwa Kila Mkoa huko Zanzibar (kwa kuwa mkoa kwao ni mdogo kuliko wilaya hapa kwetu).
Tukifanya hivyo wanafunzi wengi wangeweza kujiunga kwenye Vyuo hivyo vitakavyo fundisha kozi mbalimbali zikiwemo kozi maalum kwa eneo husika.Mf: Kozi za kilimo na ufugaji maeneo yanayo fanya shuhuli hizo

Hii ni pamoja na kuwa na kozi ndogo ndogo kama Kuziba pancha, kuosha magari, Ukondacta kwenye magari, nk
Tukiwa na Vijana wengi wenye juzi mbalimbali kama kuchomea, kupaka rangi kwenye Magari, mechanics nk ni rahisi kuvutia viwanda vije kuekeza hapa.... na Ndicho China imefanikiwa kuvutia viwanda vingi kwa kuwa na trained labor/Skilled labor (China kupita VETA ni lazima kama ilivyokuwa kwenda Jeshini hapa kwetu miaka ya nyuma)
 
1.Kemebos,
2.st francis,
3.feza boys,
4.kibaha,
5.marian boys,
6.ilboru,
7.feza girls,
8.Tabora boys,
9.marian girls,
10.kilakala,
Hizi shule ufaulu wao ni kufuruuuu

Sijui hii mitoto imechanjiwa au ni nn 🤯🤯🤯
 
Kupata zero maana yake yeye ameshindwa kukariri vitu ya darasani na sio kuelewa, kwa sababu bata hao wa Div 1 ukimuweka leo mtaani hawezi ishi kabisa

Hao division one wanaishi wapi. Tuwape watu sifa wanapo stahili na sio kukosoa tu. Mtu kapata one ya Saba lakini unataka aonekane hana uwezo wa kuishi mtaani, kisa kapata one.
 
Kwa hio wa Div 1 watakuja kuajiriwa na nani? Serikali? Huwa hatutakua kuukubali ukweli kwamba kwa sasa nyakati zimechange sana, mtaani kuna Graduate wasio kuwa na idadi, hizi mentality za kukariri kwamba ufaulu mzuri ni tiketi ya maisha mazuri ni za kizamani sana, Time will tell

Do your part ukiwa shuleni, mambo ya kuajiriwa na kujiajiri yatakuja baadae. Tusihamasishe watu kuzembea kusoma kwa kuwadanganya wanaweza kupata zero na kuja kuwa mabilionea. Unaweza kupata one pia Ukawa bilionea.
 
Mkuu umeongea point, Ujue watanzania wengi bado tunaamini Div 1 ni tikite ya mtu kufanikiwa kwenye maisha, yaani ameisha toboa maisha,

Kupata division one ni kosa?. Yani tunafanya mtoto aliyepata division one hana maana, ila mwenye zero ndio ana akili. Mtoto aliyepata one amefanya kwa nafasi yake na anasatahili pongezi , mambo ya kuajiriwa na kuajiri yatategemea baadae.
 
Back
Top Bottom