Wanafunzi hawa waliopata zero wanaenda wap?

Wanafunzi hawa waliopata zero wanaenda wap?

Hata Rais wa Nchi moja Africa mashariki alipata zero,wenye koneksheni watajiendeleza kwa kozi za kuungaunga alafu waanze kuupiga mwingi kama mama Samia.
Divisheni ziro ni nickname tu na tafsiri yake halisia ni "Failed" (FLD)... yaani umepoteza muda tu na wewe hauna tofauti na Darasa la saba ila ni darasa la saba uliyechangamka.

Wabongo tukatunga na kuongezea kwa kuipa jina la "Division zero!" Sijui kwa maana gani... na hii divisheni ziro iko TANZANIA tu! Acheni story za vijiweni ni nchi gani ingine ina divisheni ziro?!

Na ni Rais gani huyo alipata divisheni ziro nchini?!... Unajua hayo ni matusi, kebehi na dharau kubwa sana kwa kiongozi mkubwa wa nchi na wanaoongozwa wote na wewe ukiwemo... unajua hilo?!

Mnapandikizwa chuki tu mnaingia LINE kiurahisi... urais ni taasis kubwa ndugu yangu acha kabisa!
 
tofauti ipo ndugu

kwanza inategemea na four mana ana uhakika wa kupata cheti hata kupata chuo kuomba kama veta zero imetoka hio labda arudie tena kama private candidate
Mueleweshe huyo... maana naona kajibu kwa hasira sana! Watu wa namna hiyo hawafai kabisa kuwa wazazi au washauri.
 
Duuu
Screenshot_20230129-135916.jpg
 
Kuna diplomasia
Uhamiaji
Kurasini
ZIMEPAKANA HIZO
Watoto wanakula bangi kama.chakula.
Mwalimu jichanganye wanakudunda...yaani hata class ukimshikia fimbo mwanafunzi wanakusaka nje ya shule wanakupiga hatari.
Ulizia walimu hapo
Kuna mmoja alimfata mwalimu akamwambia upo kwenye list kaa kwa kitulia usifatilie watu
.....nakaa maeneo ya karibu na hizo shule....
WATOTO NI WAHUNI KULIKO MAELEZO.
tena nahisi hayo matokeo wamestandadaiz.halali halali hamna wa kupata 3 pale.na woote hao walimaliza la saba kwa ufaulu wa A$B
Nasikia Physics bado ni tatizo. Ila angalia shule kama Kemibos wote wamepata A ya Maths, Biology, Civics, KHistory, Kiswahili
Screen Shot 2023-01-29 at 14.05.37.png
 
Maisha ni fomula sio Division na Kupata ziro sio kuwa na ziro maishani.
Unaweza ukawa na 1 mtaani ukaliftiwa na 0.

Akili mkichwa, division 0 ana alternative! 🙌

Wote wakifaulu mjini tutakosa mboga.
Ukitaka mambo yaende fanya kazi na ambaye hajasoma, kwani
wasomi wengi akili yao imelala, ni wavivu wa kujitoa. 🙌
 
Nashangaa sana mwanafunzi anasoma miaka 4 halafilu anatoka na Zero.
Inamaana hajapata chochote ?
Yaani sawa na std 7 leaver. ?
Ina maana test zote kaferi ?

Mi naona wahitimu wa Secondari waanzie kupewa Division 4. Yaani wasiandikiwe 0.
 
Maisha ni fomula sio Division na Kupata ziro sio kuwa na ziro maishani.
Unaweza ukawa na 1 mtaani ukaliftiwa na 0.

Akili mkichwa, division 0 ana alternative!

Wote wakifaulu mjini tutakosa mboga.
Ukitaka mambo yaende fanya kazi na ambaye hajasoma, kwani
wasomi wengi akili yao imelala, ni wavivu wa kujitoa.
Na wengi wao hao wenye 1 na majoni kisomo uraiani wanahangaika kwerikweri

Ova
 
Back
Top Bottom