Wana-jf nimefiwa na mke wangu!!

Wana-jf nimefiwa na mke wangu!!

Nasikitika kuwafahamisha kuwa nimepata msiba leo alfajiri mke wangu kipenzi amenitoka. Kimsingi mazishi yamefanyika leo saa 10 kwenye makaburi ya changanyikeni...wife ameniachia watoto wawili wa kike 11 & 8.

images
 
Pole sana Sajenti aisee dah. Mungu akupe nguvu katika kipindi hiki kigumu
 
Pole sana Sajent,
Mungu aliye mpangaji wa mambo yote akutie nguvu wewe na watoto.
Maskini kifo kitu kibaya jamani
 
Pole sana Mkuu Sajenti. hayo ndiyo majaribu ambayo Muumba ametuandalia waja wake. Lakini hakutuacha wakiwa kwa sababu ametupa nguvu za kukabiliana nayo. Kuwa na moyo mkuu wa uvumilivu na utashinda huzuni uliyokuwa nayo. Naamini wengi humu tu pamoja na wewe katika maombi ili mama apumzishwe mahali pema peponi, na familia ipate nguvu ya kupita katika majaribu haya makubwa
 
Nasikitika kuwafahamisha kuwa nimepata msiba leo alfajiri mke wangu kipenzi amenitoka. Kimsingi mazishi yamefanyika leo saa 10 kwenye makaburi ya changanyikeni...wife ameniachia watoto wawili wa kike 11 & 8.

Pole sana Sajenti, watoto na wafiwa wote

May Her soul rest in eternal peace
 
Pole sana Sajent. Mwenyezi Mungu awape faraja wewe na watoto, awapitishe salama katika kipindi hiki kigumu.

Mungu ailaze roho ya marehemu mahala pema peponi. Amen.
 
Pole sana mkuu.
Mungu akutie nguvu
Nashangaa wanaolike thread hii.
Una like Sajenti kufiwa au una like taarifa za msiba?
OTIS
 
Pole sana sana Mkuu
Mwenyezi Mungu akujalie kila la heri katika kipindi hiki kigumu na pia ailaze roho ya marehem mahali pema peponi
 
pole sana kaka, Mungu ailaze roho ya mpendwa wetu mahali pema peponi, sisi tutaendeleza yale mema yake ya kupinga ufisadi humu JF kwa kumkumbuka.
 
Sajenti, Pole sana kwa kuondokewa na mke wako kipenzi. Mwenyezi Mungu akujalie ustahimilivu na nguvu za kusimama imara katika kuendelea kulea watoto wenu.
 
pole sana ndg, bwana alitoa na bwana ametwaa jina lake lihimidiwe.
 
Pole sana mkuu. Bwana ametoa, bwana ametwaa. Jina lake lihidimiwe. Alazwe pema
 
Pole ndugu yangu, Mungu ambaye ndiye mfariji wa kila kitu akufariji na akupe nguvu katika kipindi hiki kigumu, Bwana alitoa na ametwaa jina lake lihimidiwe. AMEN

Nasikitika kuwafahamisha kuwa nimepata msiba leo alfajiri mke wangu kipenzi amenitoka. Kimsingi mazishi yamefanyika leo saa 10 kwenye makaburi ya changanyikeni...wife ameniachia watoto wawili wa kike 11 & 8.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom