Waliobanwa katika ajali wafariki

Waliobanwa katika ajali wafariki

dah nchi hii noma sana,kuna wanaougua mafua wakapelekwa ulaya kupata matibabu asap kwa pesa ya mlipa kodi,wengine wanapata ajali humu humu nchini wanashindwa kuokolewa kwa zaidi ya masaa 16 mpaka wanakata roho inasikitisha sana.
 
Na kabla ya 2015 tutaona mengi ya kudhirisha udhaifu wa huyu rais tulienae.
 
Paul kagame alivyobrespond baada ya ambasada kupata ajali
 
Inasikitisha. Lakini kuna mtu alishasema humu kua nchi imelaaniwa kwa sababu tumechagua wapumbavu watuongoze, sasa naanza kumuelewa/
 
Walichelewa kuwaokoa ili wahudhurie misiba na kutoa michango ya pole.wataonekana na jamii zaidi .
 
Hivi bado tuna waziri wa usalama wa raia? Hii inasikitisha sana.
 
Ni hivi....kwa kifupi..."MTANZANIA HANA THAMANI!".....y'all here me?
 
Qoute- Nashangaa vijana watanzania kukosa uzalendo /JK. Uzalendo kwa lipi? Elimu duni ,afya duni, ajira hazipo na hili la majeruhi kukosa msaada zaidi ya masaa kumi when all was required is someone in authority to authorize/order kampuni za ujenzi etc deploy a crane to accident zone immediately.
 
Jamani kwa sasa tuko busy kukishugulikia CDM, tutashugulkia mangapi. Na ukizingatia tulikuwa na shuguli ya harusi Njombe na ma hangover kibao. Aaha, jamani hebu mezeeni
 
Inkoskaz
Hivi kweli tuna jeshi la usalama barabarani? Huko wa IGP Mwema, yuko wapi Afande Mpinga....kwanini haya yanatokea kama vile hakuna serikali? Jana nimeshuhudia kwenye ITV taarifa ya habari saa 2 usiku walikuwepo askari polisi wakirandaranda eneo lile kumbe hawakuwa na msaada wowote hata kutoa taarifa ktk kitengo cha maafa ili kurescue wale watu. Watz watz watz mimi binafsi siamini kama tuko salama! Tafakari.
Mkuu JBITUNGO masaa 16 ni mengi sana ni two third ya siku
 
Last edited by a moderator:
Kwa wale mnaofuatilia taarifa ya habari, kuna vijana waliokuwa wakizungumza wakiwa wamebanwa na malori baada ya kupata ajali na kuomba msaada kupitia vyombo vya habari.

Majeruhi wawili waliobanwa katika lori la mizigo katika ajali iliyotokea eneo la Maseyu barabara ya Morogoro - Chalinze wamefariki Dunia baada ya kuchelewa kuokolewa kwa zaidi ya masaa 16 kutokana na kukosekana kwa vifaa vya uokoaji.

Jambo la kusikitisha, pamoja na kwamba wamekaa hai kwa muda mrefu lakini vyombo sahihi vya kuwakwamua kutokana na kubanwa na malori vimekosekana hadi wakafa wanaona.

Mungu isaidie Tanzania, watu wanakufa baada ya kuwa hai kwa zaidi masaa 10.

Swali la kujiuliza, vipi kama Lori hilo lingekuwa limembana waziri au mkuu wa mkoa akiwa ndani ya gari lake?.

Bila kuoneana aibu, hapo serikali mmefanya uzembe! R.I.P my fellow poor


Meseji yako Mkuu imenifanya nitokwe chozi hasa pale uliposema ikiwa angebanwa Waziri au Mkuu wa mkoa. Kwa kweli Mkuu sisi wanyonge hatuna chetu. Nadhani kwa kuwa Mbunge wao yuko mbali angewapigania wapiga kura wake. R. I. P. Both.
 
Hivi jamani mkoa mzima walikosa kweli vifaa vya kuwaokoa...
Ccm na serikali yake hawana msaada kwa maskini wa nchi hii
 
Mkuu Bora69, kwa specific tukio tufanyeje? Ni ukweli ulio wazi zaidi 85% ya ajali zinasababishwa na uzembe, ila jana watu wamebanwa katika ajali na hapakuwa ja jitihada za maana za kuwanasua hadi wamekufa hapo ndio ninaposikitika. Ingekuwa ni mtu wa hadhi fulani jitihada zote zingefanyika ila kwa kuwa ni wanyonge ndio hivyo tena.
Mkuu Copper, tunachotakiwa kufanya mimi...wewe na kila Mtanzania ni kuamka katika huu usingizi mzito na kuchukua hatua. Ni maafa ..ajali na mambo mengi sana yametokea na yanaendelea kutokea. Kila siku zinaundwa TUME kwa kutumia pesa yetu Walipa Kodi. Tokea MV BUKOBA mpaka Leo hii sijawahi kusikia ripoti ya matokeo ya TUME na uwajibikaji kutokana na uzembe.

Kuna mdau Uzi # 36 namnukuu "Wao(Viongozi/wanaSiasa) wakishikwa homa na Wake zao haooo wanakimbilia India kwa gharama ya Kodi zetu". Mkuu Copper unafikiri hapa tatizo liko wapi????? Kama sisi Watanzania tusipoamka na kudai Haki zetu za kimsingi!! Kutwa tunalalamika na hamna linalobadilika...mpaka hawa WanaSiasa wanatoa kauli Kama "Ni Upepo tu Utapita" au "Wivu wa Kike"....seriously!!!?????? MTANZANIA akihoji na kutaka kupata ufafanuzi kuhusu hela yake ya Kodi anakuwa na Wivu wa kike!!???
Hawa tuliowapa jukumu na dhamana ya kutuongoza na kulinda usalama wetu wamelewa na madaraka.
Unafikiri hilo janga lililotokea juzi lingempata hata Katibu kata achilia mbali Mbunge au Waziri unafikiri wangekaa masaa 16 mpaka mauti kuwakuta!!?????

Mambo Kama haya hayataki siasa wala upuuzi wa kisiasa. Haya ni maisha ya Watanzania Walipa Kodi.
Ndio maana nimesema na nitaendelea kusema Watanzania TUAMKE ili kuleta mabadiliko na Maendeleo ya nchi yetu.
Maana Tanzania ya sasa sio Tanzania tunayoijua na tunayoikumbuka wadau tuliozaliwa miaka ya sitini.
CHUKUA HATUA.
 
Wewe usifikiri una akili kuliko wote humu na mtazamo wako wa kimagamba.

Siasa imekuathiri hadi kwenye mfumo wa ubongo wako. Hivi huwa hamuoni aibu kila kitu kuingiza siasa? Eti mtazamo wa kimagamba, huoni hata aibu. Mtu anakufa hapo badala ya kutoa msaada unasubiri serikali. Akifa unajifanya unapiga kelele. Ukiambiwa hujatoa msaada eti unasema ni mtazamo wa kimagamba upuuzi mtupu. Masaa 16 umebaki tu umekodoa mimacho yako unasubiri serikali.
 
Waliotoa habari walikosea. walitakiwa waseme Chademe wanaandamana au kuna loro lenye meno ya tembo limeanguka. Mpaka said mwema angetia timu.
 
Mimi binafsi nafikiri umefika muda sisi Watanzania kuwa responsible na maisha yetu na mambo yanayotuhusu kwenye jamii zetu. Tunalalamika sana bila kupata suluhisho la Matatizo yanayotukabili katika maisha yetu ya kila siku.
Tumeweka ushabiki katika mambo ya Mipira...Big Brothers n.k na kusahahau mambo muhimu kwenye maisha yetu ya kila siku.

Asilimia 90 ya ajali zinazotokea na maafa hapa Tanzania zinatokana na UZEMBE uliopitiliza. Halafu sisi Watanzania tunabaki tukilalamika bila kuwa na mipango fasaha ya kutatua matatizo yetu.
Tusitegemee Serikali ikafanya kila kitu. Kwa sababu hao Viongozi/WanaSiasa wameshalewa na madaraka.

Tuacheni kulalamika Watanzania na tuchukue hatua madhubuti ili kujikomboa na haya MAJANGA.
Hii kazi ni yangu mimi...wewe na kila Mtanzania anayetaka mabadiliko na Maendeleo.
Tuache Ushabiki na lawama za kutupiana mipira. CHUKUA HATUA.

RIP MAREHEMU....POLENI SANA WAFIWA NA WATANZANIA WOTE MLIOGUSWA NA HILI JANGA.


...Nimeipenda Busara yako. Kila Yanapotokea Maafa tunapiga sana Kelele na kulalamika lakini hakuna kinachoendelea. Meli, Moto, Magorofa kuporomoka nk lakini husikii hata mtu akiwajinishwa zaidi ya hadithi zisizoisha za TUME.
Tuanze kuchukua HATUA za kujilinda wenyewe na Maafa haya. Na Hatua kuu ya Mwanzo kabisa tunayopaswa kuchukua ni Kuwaondoa kwenye Madaraka WAHUNI hawa Tunaowapa Sifa ya VIONGOZI wakati hawana Uwezo wala Upeo wa Kuongoza.
Na tunaweza kufanya hivyo kwa Amani 2015.
TUJIANDAE
 
Ningekuwa MBUNGE ningemuuliza pinda swali la namna hii:KWA KUWA NI KAWAIDA KWA SERIKALI SIKIVU SANA KUTUMIA NGUVU KUPAMBANA NA CHADEMA JE! SERIKALI SIKIVU ILISHINDWAJE KUTUMIA NGUVU ILE ILE IKISAIDIWA NA INTEREJENSIA KUWAOKOA VIJANA WALIOBANWA KTK AJARI?
 
Back
Top Bottom