JanguKamaJangu
JF-Expert Member
- Feb 7, 2022
- 2,308
- 5,458
Watu wawili wamefariki dunia na wengine 15 kujeruhiwa baada ya gari la abiria aina ya Toyota Coaster kuligonga kwa nyuma lori lililokuwa limeegeshwa pembezoni mwa barabara kuu ya Dar es Salaam- Morogoro eneo la Oilcom Nanenane.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro, SACP Fortunatus Muslimu amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo na kuwataja marehemu kuwa Said Abdallah ambaye alikuwa dereva wa gari hilo pamoja na Ramadhan Muya anayekadiriwa kuwa na umri wa miaka 28 hadi 35 ambaye alikuwa ni kondakta wa gari hilo.
Baadhi ya mashuhuda wa ajali hiyo wamesema kuwa chanzo ni mwendokasi.
Ajali hiyo imetokea ikiwa ni siku chache tangu watu 22 wafariki dunia katika ajali iliyohusisha basi la Kampuni ya Ahmeed baada ya kugongana uso kwa uso na lori lililokuwa likisafirishwa kwenda nje ya nchi lenye namba za IT 2816 katika eneo la Melela Kibaoni Barabara kuu ya Morogoro-Iringa.
Chanzo: Global Publishers
Pia Soma...
Morogoro: Watu 22 Wamefariki dunia kwenye ajali ya Basi la Ahmed linalofanya safari kati ya Tanga-Mbeya. Limegongana na Lori
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro, SACP Fortunatus Muslimu amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo na kuwataja marehemu kuwa Said Abdallah ambaye alikuwa dereva wa gari hilo pamoja na Ramadhan Muya anayekadiriwa kuwa na umri wa miaka 28 hadi 35 ambaye alikuwa ni kondakta wa gari hilo.
Baadhi ya mashuhuda wa ajali hiyo wamesema kuwa chanzo ni mwendokasi.
Ajali hiyo imetokea ikiwa ni siku chache tangu watu 22 wafariki dunia katika ajali iliyohusisha basi la Kampuni ya Ahmeed baada ya kugongana uso kwa uso na lori lililokuwa likisafirishwa kwenda nje ya nchi lenye namba za IT 2816 katika eneo la Melela Kibaoni Barabara kuu ya Morogoro-Iringa.
Chanzo: Global Publishers
Pia Soma...
Morogoro: Watu 22 Wamefariki dunia kwenye ajali ya Basi la Ahmed linalofanya safari kati ya Tanga-Mbeya. Limegongana na Lori