Waliobanwa katika ajali wafariki

Waliobanwa katika ajali wafariki

Watanzania wote our middle name has been Majanga kasoro wateule wachache
 
Ndugu zao 2015 sijui watakipigia kura chama kipi? Hakika watanzania sasa imefika mahali tuamue. Kama ni mtoto wa Rais, Waziri Mkuu au hata ndugu yake angebanwa nina hakika hata kwa ndege vingebebwa. Hivi mnakumbuka wale waimbaji wa Ambassador tika Rwanda walipata ajli Tanzania na Rais waao alituma nddge na helcoputer na vifaa vya uokoaji? Kenya wale wamama waombaji walipata ajali kesho yake ndege ilitumwa haraka sana!! Ngoja watanzania wapate ajali mnakufa na hakuna wa kukusaidia. Then mkiambiwa sasa hakuna viongozi wanaowajali hegu jaribuni kubadili mfumo halafu mnakataa.
 
Wakati wa kampeni watu wanakaa mpaka chini, wakishika wenye ukoma na kugonganisha mikono.

baada ya kupata kura, wanapita kwa misafara yenye ving'ora.
 
Najiuliza swali, wale majambazi waliofukuzwa mpaka na helikopta ya Polisi Tz walikuwa muhimu kushinda hawa raia wawili ktk ile ajali? Au ile ilikuwa sehemu ya mazoezi ya jeshi? Nasadiki kuamini kwa Tz JAMBAZI MTZ ANA THAMANI KUSHINDA RAIA MWEMA. R.I.P young boys.
 
Heri mimi sisemi kitu hapa...........

MIZAMBWA
INANIUMA SANA!!!
 
Hii ishu kwa kweli inasikitisha sana, uzembe katika nchi hii umezidi.
 
Dah, katika hali kama ile kweli waandishi wa habari wamefika pale wakapiga picha na kuzirusha hewani, basi? Haki ya nani watz tumechoka, kuanzia rais hadi raia wa kawaida.

Tunawapigia kelele CCM na Kikwete kwenye hili wakati waandishi wa habari na raia wengine wa kawaida waliwahi kufika eneo la tukio. Wameshindwa kweli kufanya jitihada zozote kusaidia uokoaji? Kazi yao tu ilikuwa kupiga picha na kuwafanya tamasha katika vyombo vya habari hao vijana wawili wanavyogugumia kwa maumivu makali?

Ingekuwa nchi zingine raia wa kawaida waliowahi kufika eneo la tukio wangefanya maarifa yote kwa nguvu zao zote kuhakikisha wanafanya kitu pale. Suala la kulaumu serikali halisaidii chochote katika hali kama ile.

Unamwona kabisa mtu amebanwa kabisa kwenye vyuma we kazi yako ni kunyosha mikono na kuchukua picha tu? Kweli?

Serikali inaakisi raia wenyewe tulivyo. Mijamaa imefika pale imepiga picha na kuzipeleka studio, basi.

hao raia unaowalaumu walijitaidi kwa kadri ya uwezo wao wakamchomoa mmoja pia usiwafananishe raia wa tz na wa ulaya kule ulaya vifaa ni vingi sana na watu wana uwezo wa kuvi-operate hapa serikali haikwepi lawama wao ndo wanavifaa tunawalipa kodi kama mtanzania anaishi kwa mlo mmoja kweli ataweza kumiliki crane?pia usilaumu waandishi wamejitaidi kuonyesha matatizo ya ss maskini tusivyo dhaminiwa na hao waliokutuma uwatetee humu,ndugu yangu tafakari kabla ya kupost pia epuka kutumiwa kama ile mipira yetu ya wakubwa
 
Inaniuma sana kweli serikali yetu mnatakiwa mjipange,jicho la nani litaacha kutoa machozi kwa hurumu wakati vijana wakiongeo kwa machungu huku wakiomba msaada,lakini masikini kilio chao hakikusikika na hatimae kufariki,naongeo kama mzalendo wa nchi hii serikali mbadilike,kweli kilio cha samaki machozi huenda na maji,kwahirini mashujaa wate.
 
Tatizo tumekuwa mazuzu hadi kila kitu tunategemea serikali. Tungewa na ubinadamu hao watu tungewaokoa bila kusubiri serikali ilete vifaa vyake. Ila kwa sababu kila kinachotokea tunaona serikali ndio inahusika basi sishangai kuona hao watu wamekufa bila msaada. Nina uhakika huo muda wa masaa 16 yamepita malori na matrekta ambayo yangeweza kutoa msaada kwa kiasi kikubwa, ila uokoaji ni kazi ya serikali ndio maana tumewaacha wenzetu wafe na kukimbilia kulalamika huku Jf.
JAMANI nimebaki najiuliza:- hivi ajali si janga la kila mtu?? sasa hapo ajali ilikotokea wenye kijiji walikuwa wapi? je serikali ya kijiji nayo ilikuwa wapi? wako wapi madiwani wa CCM, CHADEMA, CUF nk. au pale hakuna mpiga kura wa chama chochote, je makanisa na misikiti haikuwepo?? alikuwa wapi mkuu wa wilaya, na hao usalama wa taifa cheni yao inaishia wapi? walikuwa wapi wote hawa masaa kumi na sita? je wakereketwa watakaokuja kutuomba kura 2015 walishindwa kuzuia njia ili magari yote yasimame kuongezea sauti? je wajenzi walikuwa wapi ili watumie misumeno kutoboa bodi ya hiyo gari? je ndani kungekuwa na bilioni moja isingetolewa? watanzania sisi ni wanafiki wa kutupwa najuta kuzaliwa humu!! kama akili yetu ni kuihoji serikali hata pale penye janga kiai kwamba hatuwezi kujiongeza wenyewe...najuta kuzaliwa humu!!!
 
JAMANI nimebaki najiuliza:- hivi ajali si janga la kila mtu?? sasa hapo ajali ilikotokea wenye kijiji walikuwa wapi? je serikali ya kijiji nayo ilikuwa wapi? wako wapi madiwani wa CCM, CHADEMA, CUF nk. au pale hakuna mpiga kura wa chama chochote, je makanisa na misikiti haikuwepo?? alikuwa wapi mkuu wa wilaya, na hao usalama wa taifa cheni yao inaishia wapi? walikuwa wapi wote hawa masaa kumi na sita? je wakereketwa watakaokuja kutuomba kura 2015 walishindwa kuzuia njia ili magari yote yasimame kuongezea sauti? je wajenzi walikuwa wapi ili watumie misumeno kutoboa bodi ya hiyo gari? je ndani kungekuwa na bilioni moja isingetolewa? watanzania sisi ni wanafiki wa kutupwa najuta kuzaliwa humu!! kama akili yetu ni kuihoji serikali hata pale penye janga kiai kwamba hatuwezi kujiongeza wenyewe...najuta kuzaliwa humu!!!
 
hii habari hata mimi jana ilini haribia siku, inasikitisha sana.
R.I.P marehemu.
 
Pasco, Utaifa kwanza, Sumu, Tandale one,Mguu wa chembe etc
Ritz,ZeMarcopolo,Mwigulu,Nape, Lukolo

Kwa hili hamna pa kujificha mwaka 2015 kama tutafika huko,ushauri wa bure anzeni kutafuta aslyum sasa nchi yeyote muitakayo.Uvumilivu basi.Mnakosa hata ubinadamu shame on you!!
 
Chonde,jamani,kwenye serikali CCM ina dhamana ya dola tu,watendaji wana mchanganyiko wa ki itikadi ,wapo CDM,CCM,CUF,NCCR,TLP N.K. Kwa hiyo madai kuwa CCM inahusika moja kwa moja katika utendaji si ya kweli.
Naelewa mtu akisha kinai,hakuna jema tena kwa CCM,lakini kama unaweza kutafakari kwa kina,hutaichukia CCM,ila upofu na uvivu wa kufikiri ndio unasababisha kuibwatukia CCM.Mnyonge mnyongeni,haki yake mpeni.Kwa mfumo wa maisha ya sasa,kila mtu ni fisadi,maisha wanayoishi watanzania kwa asilimia kubwa hayalingani na kipato halali,mbona hilo hamlisemei? Mnapiga yowe mafisadi,mafisadi,mahakama zipo,vyombo vya dola vipo ,chukua hatua.
 
Ingekuwa pembe za ndovu zimeminywa kwenye hayo malori sidhani kama serikali ingechukua hata masaa mawili kuzikomboa!!
mungu awalaze marehemu mahala pema peponi!!
 
inasikitisha sana,timu na mashine za kuokoa toka dar zinaweza fika pale ndani ya saa moja,sasa kama walikaa masaa 16,ni uzembe mkubwa huo.Hivi wanasheria ham wezi kushtaki kesi za namna hiyo kutetea wanyonge.
 
R.I.P my fellow wananchi mliopendeza haya ndio majanga ya kuzaliwa pande hii ya ulimwengu! tuko pamoja.
 
Nchi hii bwana zungumzia watu wamepora pesa hapo dakika chache watoa huduma wanafika mapema sana ila kwenye majanga wanajivuta sana,eee Mungu tupe roho ya upendo uvumilivu kwa kila mwananchi
 
hao raia unaowalaumu walijitaidi kwa kadri ya uwezo wao wakamchomoa mmoja pia usiwafananishe raia wa tz na wa ulaya kule ulaya vifaa ni vingi sana na watu wana uwezo wa kuvi-operate hapa serikali haikwepi lawama wao ndo wanavifaa tunawalipa kodi kama mtanzania anaishi kwa mlo mmoja kweli ataweza kumiliki crane?pia usilaumu waandishi wamejitaidi kuonyesha matatizo ya ss maskini tusivyo dhaminiwa na hao waliokutuma uwatetee humu,ndugu yangu tafakari kabla ya kupost pia epuka kutumiwa kama ile mipira yetu ya wakubwa

usipende kukurupuka ndugu! Waandish walijitahid kwa uwezo wao wote! Wakasìndwa,nadhan we ni mmoja wa magamba ndo mana unakurupuka tu! Fanya research kwanza utaaibika
 
DUH, imenisikitisha sana, wale jamaa nimewaona ktk taarifa ya habari ya ITV wakiwa wanaomba msaada, mpaka hivi leo ninasikia walikata roho wakiwa wanajitazama.r.i.p guys!
 
wamepoteza haki yao ya kimsingi ya kikatiba haki ya kuishi huku wanajiona. pole kwa ndugu zao.
 
Back
Top Bottom