Wale mliooa wanawake wanaofanya kazi

Wale mliooa wanawake wanaofanya kazi

Pindi namuoa wala hakuwa na kazi nikapambana sana mpaka akaajiriwa,tangu aajiriwe sijawahi kumuomba hata mia mbovu,na ikitokea nimemuomba kiasi cha pesa huwa nakopa kabisa na huwa narejesha kwa wakati na kwa uaminifu mkubwa sana,

Ninachoshukuru kuna mambo mengi mno madogodogo ya kifamilia ambayo huwa nakuta yameshatatuliwa kwa viwango vya juu sana,ukisikia "baba Ray chakula kimeisha"ujue ni uga na mchele tu.,lakini sijui mboga,mafuta sijui viungo na vitu vidogo vidogo huwa naviona kila siku vipo tu.

Ukitaka mwanamke atumie pesa inayotokana na jasho lake bila hiyana usimuingilie mwache apange mwenyewe. Wewe timiza majukumu yako na hutojuta kuoa mwajiriwa.
 
Ngumu sana....ni 5% tu ya wanawake wanakuwa hivyo
Sasa watu mnapochagua wanawake huwa mnaangalia sura na matako tu 🤣🤣🤣!!!???

Nimekulia kwenye nyumba ambayo mwanamke ni mchoyo hakuna mfano. Hakuwa mama yangu mzazi ila yale maisha yalinipa funzo sana.
 
Utasikia mengi mazuri na mabaya lakini ukweli una pande mbili
1. Kuna idadi ndogo wanaochanga kinachopatikana na maisha yanaenda vizuri kabisa
2. Kuna idadi kubwa ambayo hela ya upande wa mwanamke haionekani na ikitokea ikanunua kitu kitakachofuata ni maneno maneno mengi ili kuonyesha tu alinunua yeye.

Jambo la msingi ni kuwa oa bila kutegemea kwamba kazi yake itakuwa na msaada kwenye mipango yako.
Kama akikubali kuchangia basi epuka kumwachia afanye jambo fulani peke yake, mfano kumwachia kulipa Ada ya shule ya mtoto au kulipa kodi kama umepanga. Mara zote zichanganyeni fedha zenu kwanza ndipo muanze matumizi maana wake zetu hawachelewi kutangaza "Mimi ndio nalipa ada ya mtoto mle ndani"

Nina bahati mmoja huyu mwanamke niliye naye ni mtiifu na anachopata anakileta kama kilivyo na ana kauli yake "tufanye maendeleo kwa ajili ya watoto wetu". Aina hii ya mwanamke atakumsaliti unajisikia vibaya. Sina maana kwamba ni mkamilifu ila kwenye eneo hili yupo vizuri.
wapi siyo mkamilifu mkuu??
 
Akiwa na tako na sura, ana haki ya kulalamika.

Lakini kama demu mwenyewe mbovu hatakiwi kulalamika.

Wengine kutoka nao tunapata thawabu kabisa .
Sasa watu mnapochagua wanawake huwa mnaangalia sura na matako tu [emoji1787][emoji1787][emoji1787]!!!???

Nimekulia kwenye nyumba ambayo mwanamke ni mchoyo hakuna mfano. Hakuwa mama yangu mzazi ila yale maisha yalinipa funzo sana.
 
Aisee tatizo watu wameshindwa kutofautisha kati ya Kusaidiana na Mwanamke kuprovide kwenye familia...!! Mwanamke anapokuwa anatoa kila kitu au mahitaji makubwa kwenye familia ni tatizo hiloo lakini kama mwanamke wako anakusaidia kwa vitu vidogo kama mafuta ya kula sijui chumvi hapo ndo Ndoa inatakiwa iweee... Sio mpaka chumvi eti mpaka baba nirudi toka kazini ndo inunuliwee...
Ishu si chumvi wanaume wengi wanawategemea wake zao kuhudumia mahitaj makubwa ya kifamilia Kama ada za watoto,matibabu,Kodi ya nyumba,vyakula,ujenzi nk hadi aibu
 
Kuna dada mmoja nilimsikia yani mimi namshukuru Mungu, mume wangu mambo ya saloon , chakula , kodi etc vyote anagharamia mshahara wangu hata haumhusu ndoa ndio ina miezi sasa mtu km huyo kwa badae ukimuambia achangie kitu si lazima iwe ugomvi???
 
Mwaka wa 10 huu nilimuoa akiwa Mwalimu mwenye diploma! Nilimjengea misingi bora ya maisha ya ndoa na nilipomuona anaelekea vyema nikamwambia kwangu ujinga noo!! nikamuendeleza mpaka kuwa na masters!

Sasa hivi ni afisaa mkubwa sana mahali, mshahara mkubwa na marupurupu mengi. Hajawahi kuleta tabu kabisa

Sijawahi kujuta, tupo happy chake changu na changu chake! Tunakaa pamoja na kujenga maisha kwa pamoja na familia yetu!!

Kikubwa ni misingi ya ndoa mwanaume unayoweka unapoanza mahusiano! Ukijifanya provider ndo vile tena.
Wanawake wa kibongo tena wale wenye roho za kimaskini ukiwa nao pamoja wana vipato huli hata sh.100 yao mbovu bila kelele,,,ila wao kubungua zako wataitana vijiji kwa vijiji 🤣🤣🤣...

Mwisho wa siku kila mtu na mtuwe ila kwa mimi binafsi policy ya wanawake ya chake chake ila chako chawote haipo katika katiba yangu hata kama najitosheleza kwa kila kitu.

Hao ndio hata kutoa zawadi ni kipengele na siku ukipewa ujue boxer ya 3000 ila wewe utoe iphone X ya 2m
 
Kuna dada mmoja nilimsikia yani mimi namshukuru Mungu, mume wangu mambo ya saloon , chakula , kodi etc vyote anagharamia mshahara wangu hata haumhusu ndoa ndio ina miezi sasa mtu km huyo kwa badae ukimuambia achangie kitu si lazima iwe ugomvi???
🤣🤣🤣🤣🤣🤣 jamaa aandike maumivu siku hela ikikata
 
Mrejesho.........Badala ya kwenda mbele ndo narudi nyuma!

Huyu mwenzangu ye kaajiriwa na serikali na mwisho wa mwezi sio haba. Tunakaa mikoa tofauti, Usiku wa kuamkia leo nikampa maneno matamtam sana ili nianze kuandaa mazingira ya kumuomba aniongezee laki na 10 ili niagizie vifaranga vipya kwenye mradi wangu maana bado haujaanza kutoa matunda. Nilipomwambia tu akaanza kuniambia ooh hela sina na wakati najua juzi kapokea mshahara.
Akiwa katikati ya mwezi hali mbaya huwa nafanya kila niwezalo nimtumie hata 50 ya matumizi kwa wiki ila yeye laki tu karuka viunzi.
Hapa najiona kama nimeruka stage kwenye maisha yangu, kutokana na kuoana na yeye now nashindwa hata kujilipua kwenda mbali kutafuta maisha, nakaa karibu nae ili niwajibike kama mwanaume kwake na kwa mtoto wetu lakini mwenzangu akipata hela anajiangalia sana yeye tu.
Sioni faida ya hii ndoa soon naongeza idadi ya single mothers mtaani.
Makubwa!!! Uache mke kwa kuwa kakunyima laki? Wanaume wanazidi kuyoyoma haki ya nani. Hizo buku 50 unazomuongezea akikwama wewe unachukulia kuwa ni msaada unampa? Angekuwa hafanyi kazi hiyo 50 unayompa ingetosha kumtunza yeye na mtoto?
 
Kusaidiana katika maisha ya ndoa ni kuzuri sana. Shida inakuja pale ambapo mwanaume anapigia hesabu kipato cha mkewe na chake hakiweki wazi shida inaanzia hapo.

Hakuna anayetaka shida katika maisha, ila wanaume wa kizazi hiki wanaoa wanawake wenye kazi ili kukwepa majukumu ya familia zako. Hata maneno ya Mungu anasema kuwa Mwanaume atakula kwa jasho na mwanamke atazaa kwa uchungu.
Uko sahihi kabisa, swala la kukaa 100% huchangii chochote kama kiwete ndio halitakiwi. Majukumu mume ukijaliwa kipato kikubwa uyatimize kwa 100% inaleta furaha sana mjengoni ila kama huwezi basi walau ujikaze kwa 70% uprovide ila ile ya kutulia tu kama kochi mke anafanya 100% haifai.
 
Bora wewe, kiasi kikubwa cha matumizi yake anajitegemea mwenyewe. Kuna jamaa yangu, mke anachukua 20,000 daily kwa ajili ya kula na mafuta ya gari. Saloon anaomba hela na mshahara wake huwa haujulikani unafanya kitu gani. Akiulizwa ugomvi wa kufa mtu

Duh sasa hii too much huyu angekaa tu home awe anapewa 20 yake kila siku asidie kazi na miradi ya familia
 
Mrejesho.........Badala ya kwenda mbele ndo narudi nyuma!

Huyu mwenzangu ye kaajiriwa na serikali na mwisho wa mwezi sio haba. Tunakaa mikoa tofauti, Usiku wa kuamkia leo nikampa maneno matamtam sana ili nianze kuandaa mazingira ya kumuomba aniongezee laki na 10 ili niagizie vifaranga vipya kwenye mradi wangu maana bado haujaanza kutoa matunda. Nilipomwambia tu akaanza kuniambia ooh hela sina na wakati najua juzi kapokea mshahara.
Akiwa katikati ya mwezi hali mbaya huwa nafanya kila niwezalo nimtumie hata 50 ya matumizi kwa wiki ila yeye laki tu karuka viunzi.
Hapa najiona kama nimeruka stage kwenye maisha yangu, kutokana na kuoana na yeye now nashindwa hata kujilipua kwenda mbali kutafuta maisha, nakaa karibu nae ili niwajibike kama mwanaume kwake na kwa mtoto wetu lakini mwenzangu akipata hela anajiangalia sana yeye tu.
Sioni faida ya hii ndoa soon naongeza idadi ya single mothers mtaani.
Halafu kwa nini umfanye mwenzio mjinga kwa kumpa maneno matamtam ili umpige mzinga?😆😁 Maneno matamu unatakiwa uyatoe kila siku kwa ajili ya kuimarisha uhusiano. Na unyimwe tu kwa kweli.
 
Mimi nisha ambiwa kabisa kama nataka mtoto asome private school natakiwa nimlipie ada mimi,yeye atashughulika na chakula lakin cha ajabu sasa ata kabla sijaingiza hela kila siku natumiwa magazeti ya msg jitahidi basi na wewe uwe unanisaidia vitu vidogo vidogo apo nyumbani,na kila nikipata pesa ana anza kuipangia matumizi ashasahau kwamba kanipa jukumu la kulipa ada na kujihudumia mwenyewe ,yani apa nilipo nishamwambia kabisa kama mambo yenyewe ndo ivi siwezi kuzaa tena
 
Mwanamke alioajiliwa na hana makuzi na malezi bora, ni mzigo na kero kubwa pesa yao ionekani nyumbani, ni muendo wa vikomba, michango ya sherehe, safari za kwao, nk sioni maana yoyote yaye kufanya kazi, nimesha surrender......kaa nyumbani kama hutaki changua moja mimi au Kazi..
Akishakaa nyumbani hiyo michango ya sherehe, vikoba na safari za kwao utagharamia wewe? Au unaona si vitu muhimu? Mwache afanye kazi. Kuishi na mtu mzima ambaye hana kazi ni hatari kwa afya yako ya akili. Atapata msongo na wewe utakuangukia.
 
Back
Top Bottom