Wale mliooa wanawake wanaofanya kazi

Wale mliooa wanawake wanaofanya kazi

Mrejesho.........Badala ya kwenda mbele ndo narudi nyuma!

Huyu mwenzangu ye kaajiriwa na serikali na mwisho wa mwezi sio haba. Tunakaa mikoa tofauti, Usiku wa kuamkia leo nikampa maneno matamtam sana ili nianze kuandaa mazingira ya kumuomba aniongezee laki na 10 ili niagizie vifaranga vipya kwenye mradi wangu maana bado haujaanza kutoa matunda. Nilipomwambia tu akaanza kuniambia ooh hela sina na wakati najua juzi kapokea mshahara.
Akiwa katikati ya mwezi hali mbaya huwa nafanya kila niwezalo nimtumie hata 50 ya matumizi kwa wiki ila yeye laki tu karuka viunzi.
Hapa najiona kama nimeruka stage kwenye maisha yangu, kutokana na kuoana na yeye now nashindwa hata kujilipua kwenda mbali kutafuta maisha, nakaa karibu nae ili niwajibike kama mwanaume kwake na kwa mtoto wetu lakini mwenzangu akipata hela anajiangalia sana yeye tu.
Sioni faida ya hii ndoa soon naongeza idadi ya single mothers mtaani.
Hueleweki unakaa naye mikoa tofauti halafu unaogopa kwenda mbali....chai tupu jipange
 
My brother is my role mode. Wako na familia ya watoto watatu na wote wameajiriwa. Wana miradi mbali mbali nje ya ajira ambayo wote wanashirikiana kila wanapopata muda na hela ya hiyo mitadi ndio inaendesha familia. Mishahara yao ni kwa ajili ya maendeleo. Mfano wakitaka kujenga banda la kuku bro akinunua mchanga mke atanunua kokoto. Naomba Mungu anijalie nipate mke kama shemeji yangu
Ngumu sana....ni 5% tu ya wanawake wanakuwa hivyo
 
Mi nadhani kusaidiana sio jambo baya hasa kama mmekubaliana..

Unaweza kuta mnakubaliana vzr as wife ata cover expenses za nyumbani, chakula, umeme, maji na vingine alafu mume afanye maendeleo as ujenzi ada za watoto ( hii ni kama mume ana kipato kikubwa kumshinda mama)

Tatizo linakuja pale mume anaishia kunywa pombe na marafiki na kuhonga michepuko, maendeleo hayaonekani, hela yake haionekani, yuko radhi kupangia mchepuko full furnitured lkn mwanae anadaiwa ada shuleni, na mke anahangaika peke yake na familia. Hii inaumiza sana na wanawake wengi wapo kwny kundi hili.
Unachokisema ni kweli kabisa, wanawake wengi wamepitia experience hii kutoka kwa wanaume.
Tatizo Kuna watu wanaingia kwenye ndoa lakini wanataka kuishi kihuni.
Ukimpata ambaye ni mwelewa na mwanamke ukawa na akili nzuri basi mtapanga mipango na mambo yataenda vizuri kabisa.
Asante kwa tafakuri njema.
 
Pamoja na changamoto za wanawake wenye ajira,mimi nitaoa mfanyakazi tena nikipata mwalimu itapendeza zaidi.Hawa wa mama wa nyumbani nao ni shida tu nyumbani,wanakula na kunenepeana tu na hawati kufanya shughuli yoyote,ukimpa biashara inakufa, ukimfungulia duka,anauza mpka anamaliza na pesa hujui anakopeleka.
 
Tatizo hapo ni nyie kuanzisha familia ilhali nyie sio familia, hapo tambua mna miji miwili ambayo yawezekana inahudumiwa sawa. Usimlaumu, fanyeni utaratibu muishi pamoja.

Halafu kupokea mshahara sio kuwa na pesa, maana mishahara mingi ya waajiriwa huwa iko kwenye plans kabla haijaingia. Hivyo unapaswa umuandae mapema kama unahitaji pesa akuingize kwenye plan sio unakurupuka tu wakati kwa maelezo yako mwenyewe inaonyesha bado hamjawa na mipango ya kuwa na akiba.
Wanaume wanajisahau sana mtu anakukuta na kamshahara kako unaishi mwenyewe unapambana na shida zako from nowhere tu naye anataka aingie kwa bajeti eti apewe pesa nyie wanaume acheni kitonga .
 
Mrejesho.........Badala ya kwenda mbele ndo narudi nyuma!

Huyu mwenzangu ye kaajiriwa na serikali na mwisho wa mwezi sio haba. Tunakaa mikoa tofauti, Usiku wa kuamkia leo nikampa maneno matamtam sana ili nianze kuandaa mazingira ya kumuomba aniongezee laki na 10 ili niagizie vifaranga vipya kwenye mradi wangu maana bado haujaanza kutoa matunda. Nilipomwambia tu akaanza kuniambia ooh hela sina na wakati najua juzi kapokea mshahara.
Akiwa katikati ya mwezi hali mbaya huwa nafanya kila niwezalo nimtumie hata 50 ya matumizi kwa wiki ila yeye laki tu karuka viunzi.
Hapa najiona kama nimeruka stage kwenye maisha yangu, kutokana na kuoana na yeye now nashindwa hata kujilipua kwenda mbali kutafuta maisha, nakaa karibu nae ili niwajibike kama mwanaume kwake na kwa mtoto wetu lakini mwenzangu akipata hela anajiangalia sana yeye tu.
Sioni faida ya hii ndoa soon naongeza idadi ya single mothers mtaani.

Kuna watu watakwambia eti wewe hujiamini ndio maana unataka kumuacha huyo mwanamke na blah blah blah zingine... achana kabisa na huyo kibaraka wa ibilisi atakurudisha kwenye zero
 
Bora wewe, kiasi kikubwa cha matumizi yake anajitegemea mwenyewe. Kuna jamaa yangu, mke anachukua 20,000 daily kwa ajili ya kula na mafuta ya gari. Saloon anaomba hela na mshahara wake huwa haujulikani unafanya kitu gani. Akiulizwa ugomvi wa kufa mtu

halafu bado yuko nae mpaka muda huu nnavyoandika hapa?
 
Binafsi mke wangu anafanya kazi lakini sijawahi mwambia achangie hata kitu kimoja i stand my self as a men

Halafu wakati unamfukuzia kigezo kimoja wapo kilichokuvutia kwake na kumfanya mke wako ni hiyo ajira aliyonayo? ambayo kwa sasa ni useless kwa upande wako humo ndoani?
 
Uko sahihi kabisa na hii kitu hupelekea wanawake wengi tupate funzo .

Pesa zangu ..zangu..za mwanaume za kwetu..mwanaume hawezi fanya Kama tulivyokubaliana Kila mtu atumie pesa zake na tusiulizane

Na wewe umeolewa?
 
My brother is my role mode. Wako na familia ya watoto watatu na wote wameajiriwa. Wana miradi mbali mbali nje ya ajira ambayo wote wanashirikiana kila wanapopata muda na hela ya hiyo mitadi ndio inaendesha familia. Mishahara yao ni kwa ajili ya maendeleo. Mfano wakitaka kujenga banda la kuku bro akinunua mchanga mke atanunua kokoto. Naomba Mungu anijalie nipate mke kama shemeji yangu

my sympathy to that dude you call your bro!
 
Pamoja na changamoto za wanawake wenye ajira,mimi nitaoa mfanyakazi tena nikipata mwalimu itapendeza zaidi.Hawa wa mama wa nyumbani nao ni shida tu nyumbani,wanakula na kunenepeana tu na hawati kufanya shughuli yoyote,ukimpa biashara inakufa, ukimfungulia duka,anauza mpka anamaliza na pesa hujui anakopeleka.

Cha kustaajabisha wanaume kama wewe eti ndio mnaonekanaga mna akiiiiil na mnaojiamini kisa tu mna kimbilia kuoa wasomi. Wakati kihalisia nyie ni dhaifu maana unaoa mwanamke ambaye atakusaidia kufikiri jinsi ya kuendesha familia na uko tayari kugawana nae madaraka ambayo ulipaswa kuwa nayo mwenyewe tu. Pole in advance kwa kitakachoweza kutokea huko mbeleni.
 
Ukimpata mwelewa maisha yanakuwa matamu sana kwakuwa mnasaidiana kila kitu

Muelewa hatoshi tu,tatizo yanayo jiri.
Hakuna salama katika ndoa ya mwanamke muajiriwa hata awe muelewa wa aina gani.

Huyo muelewa unatakiwa ujue ya kuwa ni mwanamke na ni binadamu pia. Hapa kuna kazi so ndogo.
 
Back
Top Bottom