Wako wapi hawa Makamanda machachali wa Polisi?

Wako wapi hawa Makamanda machachali wa Polisi?

Hello wazee,ni kitambo kama maajabu kutowaona katika pilika pilika za polisi hawa makamanda maana kama wengekuwa ma RPC basi tungesikia tu au kama wanapewa au kuhamishwa vitengo maana kiutaratibu inapotokea kiongozi anahamishwa au kupewa kijiti tunataarifiwa wazi.

1.Kamanda AHMED MSANGI,jembe langu sana hili,wengi tulilifahamu,jamaa katembea sehemu ngumu ngumu kama RPC na mara ya mwisho alitokea MBEYA akatupwa MWANZA na cheo cha kamishna msaidizi.Vipi huyu bwana yu wapi? kastaafu au? .2.Kuna bwana mmoja wa kuitwa NSATO MARIJANI alishawahi kuwa kamanda wa operation na mafunzo kipindi cha magufuli,na inasemekana walihenya jkt pamoja na magufuli,alipotea ghafla tuu baada ya kumpa kijiti mzee LIBERATUS SABAS.

3.MZEE WETU MUROTO japo alikuwa anazingua sana,kwa kuwadhalilisha watuhumiwa mitandaoni na kwenye press vipi nae yu wapi?

4.Vipi kuhusu mzee MAMBOSASA maana mara ya mwisho sirro alimtoa DSm na kumpeleka CCP MOSHI kama mkuu wa chuo ila kwa sasa kuna mkuu wa chuo mwingine pale.
5ABDULLRAHMAN KANIKI alikuwaga naibu IGP miaka mingi tangu kwa igp mwema hadi ernest mangu pale.

Tumwage mchele,si kwa ubaya ni story tuu za hapa na pale na. kama kuna wengine tuwataje,polisi ni chombo chetu japo kuna kukwazana.
Ahmed Msangi ni DCP yupo bado kazini, Kova yupo vizuri sana sana kimaisha ana vishughuli vyake vya kumpa uhakika wa kula na mafuta ya V8, Wengine sijui lakini nadhani muroto boss wa ulinzi GGM mgodi wa geita sio kazi mbaya sina uhakika na mshahara wake lakini aliyetoka hiyo nafasi niaka ya 2016 alikuwa analipwa kama M 8 kwa mwezi pamoja na benefits kibao
 
Alistaafishwa mapema ...umri ulikuwa bado
ok
Ahmed Msangi ni DCP yupo bado kazini, Kova yupo vizuri sana sana kimaisha ana vishughuli vyake vya kumpa uhakika wa kula na mafuta ya V8, Wengine sijui lakini nadhani muroto boss wa ulinzi GGM mgodi wa geita sio kazi mbaya sina uhakika na mshahara wake lakini aliyetoka hiyo nafasi niaka ya 2016 alikuwa analipwa kama M 8 kwa mwezi pamoja na benefits kibao
hiuo kampuni ya ulinzi ya GGM ni ipo chinni ya polisi?
 
Ahmed Msangi yupo office ya DCI.

Aliyepata kazi mgodini ila alishastaafu pia mgodini ni Abdallah Msika.

Makamanda wema:

Basilio Matei - alikuwa rpc Arusha 2010
Tibaigana - Dar Es Salaam

DC Msangi sio mtu poa, anaonesha ana ukatili.

Kwasasa moja ya senior police wema ni DC Henry Mwaibambe, hata akizungumza unaona. Alikuwa rpc Tanga, na Geita.
 
Mzee Mambosasa yupo amefungua sehemu nzuri sana hapa mjini Kuna ukumbi wa sherehe, bar, restaurant, mazingira mazuri na Kuna swimming pool pamoja na sehemu za kuchezea watoto. Mara nyingi tunakula na kupiga bia moja mbili tatu katika bar yake tukiwa na familia. Akiwakuta atakuja katika meza atawasalimia kwa heshima, kuwakaribisha na kuwashukuru kwa kuja yupo very humble.
 
Back
Top Bottom