Wakinadada ni wabahili jamani

Wakinadada ni wabahili jamani

Maisha ni kusaidiana yes na inapendeza kumsaidia mmeo.Ili maendeleo yapatikane mwanamke pia anatakiwa ajitoe kwa hali na mali kumsaidia mumewe.Tatizo ni kuwa kuna baadhi ya wanaume wakisaidiwa wanabweteka na kuanza dharau.Mwengine hadi anafikia hatua ya kuukontrol mshahara wa mwenzie kama wake badala ya kukaa na kushauriana
 
Kuwabadilisha Wadada wa Humu ndani Kuondokana na uhitaji wao wa pesa kwa wanaume huku za kwao wamezibana ni Sawa na kwenda kuitangaza biblia Katika Nchi ya Saudi Arabia... Shtuka ukishaonja sanuka humu ndani nina Imani na Mabinti Watano tu...
 
Kuwabadilisha Wadada wa Humu ndani Kuondokana na uhitaji wao wa pesa kwa wanaume huku za kwao wamezibana ni Sawa na kwenda kuitangaza biblia Katika Nchi ya Saudi Arabia... Shtuka ukishaonja sanuka humu ndani nina Imani na Mabinti Watano tu...
Dogo tutajie hao "mabinti" watano...BTW, labda ni wanawake sio mabinti
 
Jaman mwanaume ni kichwa cha familia na kazi ya kichwa ni kucontrol mwili hayo ni majukum ya mwanaume ndo maana imeandikwa;
"Mwanaume atatafuta kwa jasho na mwanamke atazaa kwa uchungu"
Sisi jukumu letu ni kuzaa kwa uchungu na wala hutusikii tukisema mtuaaidie kuzaa kwa uchungu coz tunajua ni jukumu letu
Mwanaume kuchacharika siyo kulalamika
Nu hayo tu sorry kama ntakua nimekuudhi.
 


Habari zenu wanajamii forum,

Leo ngoja niongee na kina dada na tabia zao za ubahili.

Yaani utakuta hata mpenzi wako anakuwa mgumu kukusaidia inapotoke shida fulani lakini wao ni wepesi sana kuomba kusaidiwa sijui hizo hela zenu mnapeleka wapi jamani.

Hii nimeishuhudia hata kwa kaka yangu mke wake ni mgumu sana inapofika mumewe kaishiwa.

Hata utakuta msichana mnapendana sana ila suala la kutoa ni wagumu hawa viumbe aisee yaani yupo radhi akuachie ulipie kodi nyumba,ulipie watoto ada na mahitaji mengine yeye anauchunaa mpaka ukute mmekabwa sana ndio utaona anajitoa tena kiubahili
.

Labda niwaulize hela zenu wakina dada huwa mnazipeleka wapi hata kusema baba ni kichwa cha familia muda mwingine jamani wanaume tunachoka sana tuwe tunasaidiana jamani sometimes.

Ni hayo tu, nawasilisha


Mama'ko angekuwa mbahili wewe usingezaliwa?

Kama unabisha, muulize baba'ko.
 
Mhm wee ulishabugi mennnn....mwanaume yoyote lazima ajue kuwa pesa ya mwanamke ni kwa ajili ya yeye peke yake i.e to luk sexy.
Ada ya shule, matibabu, chalula, kumnunulia gari na kutia mafuta, outings, holidays, financial problems za familia yake na mengineyo ni jukumu la wewe mume. Ukilijua hilo wala hutapata presha nao.

Wee kazi yako hapo ni kuhakikisha haleti uzembe kwenye idara yake ya kuwa sexy nd presantable na kutotoa watoto na kuwalea vizuri...huo ndio msaada wa mke.
 
Mhm wee ulishabugi mennnn....mwanaume yoyote lazima ajue kuwa pesa ya mwanamke ni kwa ajili ya yeye peke yake i.e to luk sexy.Ada ya shule, matibabu, chalula, kumnunulia gari na kutia mafuta, outings, holidays, financial problems za familia yake na mengineyo ni jukumu la wewe mume. Ukilijua hilo wala hutapata presha nao.Wee kazi yako hapo ni kuhakikisha haleti uzembe kwenye idara yake ya kuwa sexy nd presantable na kutotoa watoto na kuwalea vizuri...huo ndio msaada wa mke.
shikamoo bro
 
Mwanamke anatakiwa ajiongeze mwenyewe.siyo kila kitu unaona ana struggle mume wako wewe kimyaa siyo kabisa mambo hayo.kama una kazi ya kukuingizia kipato otherwise kama ni wanyumbani shughuli yako moja tu.
 
sio wote aise namshukuru mungu wangu pesa anatoa kadi zetu za benki zipo sehem inayojulikana kwetu wawili nikiishiwa nabeba kadi yake naye pia akiishiwa anabeba kadi yangu life raha tu ila nachoshukuru mke wangu ni mvivu sana kwenda benki so unakuta muda mwingi mm natembea na kadi tu kutekeleza maendeleo ya familia yangu
 
Hii inachangiwa na mwanaume kuwa na matumizi ya siri kwa pesa zako hii ilinitokea kwa mke wangu coz mambo yangu mengi nilikuwa nafanya kimyakimya afu nikiishiwa naomba ela apo lazima uulizwe ela umepeleka wapi? Ila kama mipango unaweka wazi ata ukiishiwa ukisema utasaidiwa coz huwezi saidiwa ela na mkeo kumbe unampelekea malaya wako pembeni uko kuwa wazi tu kwa mkeo uone mabadiliko
 
Maisha ni kusaidiana..........
Mie kama ninayo huwa natoa
Life is so beautiful If we help each other

Ninaweza kuwa sina na bado nikafanya namna ya kumsaidia apate hiyo pesa anayoihitaji, Kama ambavyo yeye hapendi kuona sina hela ndivyo ambavyo sipendi kumuona hana pesa.
Niko hivyo hivyo sijawahi kubadilika since then, namnunulia zawadi, sometimes na clear bill, am that independent and am happy.
Sema kipindi nipo chuo nilimdate mkaka mmoja hivi akatangazia wenzie kuwa namuhonga, nilimuacha siku hiyo hiyo. Nikagundua ukidate na mtu ambaye hajakua ni tatizo sana, since there sikuwahi kuwa na mtu ambaye akili yake haijakomaa.
 
Jaman mwanaume ni kichwa cha familia na kazi ya kichwa ni kucontrol mwili hayo ni majukum ya mwanaume ndo maana imeandikwa;
"Mwanaume atatafuta kwa jasho na mwanamke atazaa kwa uchungu"
Sisi jukumu letu ni kuzaa kwa uchungu na wala hutusikii tukisema mtuaaidie kuzaa kwa uchungu coz tunajua ni jukumu letu
Mwanaume kuchacharika siyo kulalamika
Nu hayo tu sorry kama ntakua nimekuudhi.
Wala hamzai kwa uchungu sikuhizi,operation za uzazi zimekuwa kama kunywa chai.
 
Mi nachokaga kitu kimoja, akiwa peke yake anaishi kwa hela zake mwenyewe ni mbahili balaaa, sasa muoe weeeeee!!! matumizi anafanya kujiachia tu, daaah!!

hahahaha labda toka mwanzo ulionyesha unazo naye anatumia nafasi.......maisha kushirikishana wakati mwingine yanazidisha upendo kama hakuna unafiki ndani yake
 
hahahaha labda toka mwanzo ulionyesha unazo naye anatumia nafasi.......maisha kushirikishana wakati mwingine yanazidisha upendo kama hakuna unafiki ndani yake

Aisee kwahiyo hata kama nina pesa inabidi nisimuoneshe sasa.baadhi ya wanawake ni ngumu sana kukaa nao.kwanini mtu usiwe flexible tu kama zipo si zetu wote.
 
Back
Top Bottom