Wakili wa Tigo adai kwao Compliance (Utii) kwa mamlaka ni kipaumbele kuliko Privacy (faragha) za Wateja

Kampuni ya tigo imejitia doa sana ambapo itawachukua muda mrefu sana kurudisha imani kwa wateja zao ambayo wameipoteza
 
Hebu tujiulize kidogo halafu tuendelee kubishana mpaka kesho....

Zipi ni requirements za serikali haya makampuni yanapoomba leseni kwa serikali..?
Tunaponunua laini kuna fomu ya makubaliano kati yetu na tigo kwa tigo kulinda haki zetu tunajaza na kusign?

JF tukijiunga huwa kuna requirement za JF tunapewa then tuna click agree ~ TUNAZISOMA HIZI REQUIREMENTS.. au tuna agree tu..
Kuna taratibu zake mkuu, hakuna anayekataa kwamba sheria zinawaruhusu kutoa taarifa za wateja.

Kwanza kabla hawajatoa taarifa za mteja ni lazima wajue zinaenda kutumika kwa sababu ipi.

Pili lazima kuwe na court order.

Tatu lazima mteja afahamishwe, ili kuconfirm kama kweli kuna kitu cha namna hiyo.

Police hawezi kuomba taarifa za mteja kisha ww lawyer ukatoa kisa tuu ni police.
 
Kuna taratibu zake mkuu, hakuna anayekataa kwamba sheria zinawaruhusu kutoa taarifa za wateja.

Kwanza kabla hawajatoa taarifa za mteja ni lazima wajue zinaenda kutumika kwa sababu ipi.

Pili lazima kuwe na court order.

Tatu lazima mteja afahamishwe, ili kuconfirm kama kweli kuna kitu cha namna hiyo.

Police hawezi kuomba taarifa za mteja kisha ww lawyer ukatoa kisa tuu ni police.

Hapo Tigo hawawezi kufunguliwa kesi na kudaiwa mabilioni ya shillingi kwa kutofuata taratibu za utoaji taarifa za mteja?..
Kupitia hiyo kesi pia wateja wengine kwa kukusanya sign hata 10000 kuishitaki Tigo kwa kushindwa kulinda taarifa za wateja....ref ikawa kesi hii na ile ya Abdul Nondo...
 

Japo hakuna sheria maalum ya ‘Data Protection’ (ukiniuliza mimi hii ilitakiwa kuwa imetungwa muda mrefu) lakini kuna sheria nyingine kadhaa zinazolinda faragha enough to sue ‘phone companies’.

Unashangaa mtu kama Haji Manara kulalamika hadharani namna mawasiliano yake yalivyonyakuliwa; serikali kimya (wizara ya mawasiliano na Technology) na yeye mwenyewe pamoja na ujanja wake kushindwa kuishitaki kampuni husika.

Ni hivi kila kampuni inabeba lawama za matendo ya wafanyakazi wake (vicarious liability). Isitoshe kumfungilia kesi mfanyakazi akulipe billion kadhaa hiyo hela hana so it’s waste of time, lakini TiGo wanazo hizo hela.

Kwa kanuni za ‘tort law’ ni jukumu la kampuni kulinda wateja sio mwajiriwa that include info za wateja na usalama wao.

Ningekuwa mwanasheria nchi hii ningekua tajiri sana, habari kama hizi nakusanya wahanga 20 hivi no legal fees, twendeni dai tsh billion 5 tukishinda 40% yangu.

Sijui kuna ajali chanzo dereva au basi lenyewe lilikuwa mkweche natafuta familia za abiria twendeni kudai fidia. Yaani sina muda kabisa na kesi za wanasiasa zenye malipo uchwara.

Hila kunaitajika ‘data protection legislation’ imefikia hatua hawa watoto awaogopi kabisa mtu anatangaza biashara ya ku hack mawasiliano kama vile ni kitu normal instagram.
 
Wakati nchi nyingi makampuni ya mawasiliano yakiwa yanaweka kipaumbele sana kwenye usiri wa taarifa za wateja wao, hapa kwetu hali ni tofauti kabisa.

Hilo limethibitishwa leo na Wakili Msomi Fred Kapara, ambaye ni Wakili wa Kampuni ya Tigo, alipoulizwa Mahakamani wakati akitoa ushahidi katika kesi inayomuhusu Mwenyekiti wa CHADEMA na wenzake wanne, kwamba kati ya Utii kwa mamlaka na Usiri wa taarifa za wateja kipaumbele kwao ni nini, bila kupepesa macho akajibu Utii (Compliance) kwao ndiyo kipaumbele (Priority) zaidi.

Sasa majibu ya kwanini kumekuwepo na uzimaji wa baadhi ya mitandao ya kijamii na kupanda mara dufu kwa gharama za bando za data yameshapatikana. Sababu kubwa ni kwamba huko kwenye hizo social networks zingine kwao Privacy za Wateja ndiyo Priority hivyo mamlaka zitashindwa kupata kile wanakitaka kwa urahisi.

Hii kesi mpaka waje wamalizike mashahidi wote 24 tutakuwa tumeshapata siri nyingi sana ambazo raia wa kawaida tulikuwa tunafichwa.

View attachment 1995845
Kwa hiyo mlitaka Migaidi na Mijambazi ijifiche kwenye hii mitandao ya simu kwa kisingizio cha USIRI kwa wateja?
 
Kwa hiyo mlitaka Migaidi na Mijambazi ijifiche kwenye hii mitandao ya simu kwa kisingizio cha USIRI kwa wateja?
Kuna taratibu za kisheria zinazoruhusu vyombo vya usalama kupata info kwenye investigation zao nchi zote duniani. Na wakitaka hizo info inabidi wapitie kwa uongozi wa kampuni.

For security reasons hivi polisi aende kuomba info za mtu kwa mfanyakazi wa kawaida si anafichua upelelezi wenyewe, unajuaje jamaa ata mtonya muhisika.

Makampuni ya Tanzania kila sakapoko kwenye IT department anatoa info za wateja kwa urahisi sana, hili jambo alikubaliki, including mods wa JF.
 
Maxence Melo alisimama imara pamoja na kulazwa lupango kwa wiki kadhaa kutetea haki ya wanachama wa JF.

alijitetea kwamba hawajui,sababu mnavaa chupi zisizo zenu.

tigo wakufiche na umefanya uduanzi!!!my brother kachunguze kwanini ulisajiri line kwa taarifa za nida,haikuwa ili tuwe tunasoma jina lako ukitaka kutumiwa hela.
 
Kwa maana hiyo chadema walitaka hata mtu mwovu akitumia mtandao ALINDWE TU NA UOVU kwa kuwa sheria ya usiri na faragha inamlinda.
#Hata ulaya hakuna kitu ya namna hii.
Hapana ndugu Crocodiletooth, unawahi mno kutoa conclusion ili ukidhi kiu ya utakacho wewe...

Hoja hapa siyo kumlinda au kutomlinda mhalifu kwa sababu mpaka hapa tulipo sasa hakuna aliyekwisha kuthibitishwa na mahakama kuwa ni mhalifu...

Msisitizo hapa ni kuwa, hata kama mamlaka za kudhibiti uhalifu zina hisi mtu fulani anatumia mitandao kwa nia ya kufanya uhalifu, basi utaratibu wa kisheria ufuatwe ili kupata taarifa za mtu huyo...!

Hili ndilo tatizo la ushahidi wa Freddy Kapala..!

Kwa kifupi, polisi wamemtumia "mhalifu au hacker" Freddy kujipatia taarifa za mteja wa Tigo TZ ili zitumike kama ushahidi wa kisheria mahakamani...!!

Sasa fikiri mwenyewe matokeo yake yatakuwaje..
 
Wakati nchi nyingi makampuni ya mawasiliano yakiwa yanaweka kipaumbele sana kwenye usiri wa taarifa za wateja wao, hapa kwetu hali ni tofauti kabisa.

Hilo limethibitishwa leo na Wakili Msomi Fred Kapara, ambaye ni Wakili wa Kampuni ya Tigo, alipoulizwa Mahakamani wakati akitoa ushahidi katika kesi inayomuhusu Mwenyekiti wa CHADEMA na wenzake wanne, kwamba kati ya Utii kwa mamlaka na Usiri wa taarifa za wateja kipaumbele kwao ni nini, bila kupepesa macho akajibu Utii (Compliance) kwao ndiyo kipaumbele (Priority) zaidi.

Sasa majibu ya kwanini kumekuwepo na uzimaji wa baadhi ya mitandao ya kijamii na kupanda mara dufu kwa gharama za bando za data yameshapatikana. Sababu kubwa ni kwamba huko kwenye hizo social networks zingine kwao Privacy za Wateja ndiyo Priority hivyo mamlaka zitashindwa kupata kile wanakitaka kwa urahisi.

Hii kesi mpaka waje wamalizike mashahidi wote 24 tutakuwa tumeshapata siri nyingi sana ambazo raia wa kawaida tulikuwa tunafichwa.

View attachment 1995845
Kwani Chadema ingekuwa nyie ndo wamiliki wa Tigo TZ alaf serikali ikaja inamtuhumu mtu mngegoma kutoa ushirikiano?
Kumbukeni tu jinai ni mambo yanaweza kuhatarisha usalama wa nchi na hiyo serikali inayoomba hizo data ndiyo imekupa leseni.

Chadema mngegoma kutooa hizo taarifa ingekuwa nyie ndo Tigo TZ?
 
Kwa maana hiyo chadema walitaka hata mtu mwovu akitumia mtandao ALINDWE TU NA UOVU kwa kuwa sheria ya usiri na faragha inamlinda.
#Hata ulaya hakuna kitu ya namna hii.
Sialiulizwa Kama iyo no inakosa au ameona hatia yyte kwa uyo mteja akasema hamna, hat y hajui Ni kwa nn anatoa ushahid kwa no ambayo yy hajaona kosa
 

Japo hakuna sheria maalum ya ‘Data Protection’ (ukiniuliza mimi hii ilitakiwa kuwa imetungwa muda mrefu) lakini kuna sheria nyingine kadhaa zinazolinda faragha enough to sue ‘phone companies’.

Unashangaa mtu kama Haji Manara kulalamika hadharani namna mawasiliano yake yalivyonyakuliwa; serikali kimya (wizara ya mawasiliano na Technology) na yeye mwenyewe pamoja na ujanja wake kushindwa kuishitaki kampuni husika.

Ni hivi kila kampuni inabeba lawama za matendo ya wafanyakazi wake (strict liability). Isitoshe kumfungilia kesi mfanyakazi akulipe billion kadhaa hiyo hela hana so it’s waste of time, lakini TiGo wanazo hizo hela.

Kwa kanuni za ‘tort law’ ni jukumu la kampuni kulinda wateja sio mwajiriwa that include info za wateja na usalama wao.

Ningekuwa mwanasheria nchi hii ningekua tajiri sana, habari kama hizi nakusanya wahanga 20 hivi no legal fees, twendeni dai tsh billion 5 tukishinda 40% yangu.

Sijui kuna ajali chanzo dereva au basi lenyewe lilikuwa mkweche natafuta familia za abiria twendeni kudai fidia. Yaani sina muda kabisa na kesi za wanasiasa zenye malipo uchwara.

Hila kunaitajika ‘data protection legislation’ imefikia hatua hawa watoto awaogopi kabisa mtu anatangaza biashara ya ku hack mawasiliano kama vile ni kitu normal instagram.
Nchi nyingine Wana sheria Kali za data protection na lazima kuingia makubaliano kati ya pande mbili, ila bongo swala la data protection inabidi liende bungeni maana watu wanaingilia privacy za watu kimasihara sihara tu na hamna Cha kuwabana
 
Back
Top Bottom