WAKILI MWABUKUSI: Rais Samia atusikie, Mkataba wa Bandari haulindi uhai wa Nchi yetu
Katika mahojiano leo na wakili Mwabukusi anaangazia mambo zaidi kamati ya bunge, uwakilishi wa muswada wa mkataba bungeni na jinsi muda finyu waliopewa wabunge kuujadili ...
.
Wabunge Halima Mdee, Aida Kenani pamoja na Luhaga Mpina ambaye hakupata nafasi bungeni kuwakilisha hoja hivyo kuwakilisha maoni nje ya bunge kwa maandishi watambuliwe kwa kupewa maua yao hayo bila kumsahau dada yetu mpendwa wa taifa Mange Kimambi amesema wakili msomi Boniface Mwabukusi
Aliyevujisha mkataba ni mzalendo halisi na hii inatia moyo kuwa bado kuna Wazalendo wachache ndani ya serikali... na huyu atambuliwe wajibu wake mkubwa kulinda maslahi ya taifa
Serikali inawajibika kwetu umma yaani wananchi hivyo viongozi wote serikalini watambue mamlaka zote tulizowapa ni zili zilizotamkwa katika katiba kama hawawezi waache nyadhifa zao waende nyumbani ...
Advocacy tunayofanya ni kazi ya kuelimisha wananchi na ndiyo wajibu wetu kwani waziri Mbawara katika hadhira tofauti tofauti anasema mkataba huu ni makubaliano na akifika mbele ya viongozi wa dini n.k wanasema mkataba ...
Viongozi waache propaganda kwa kwenda sehemu mbalimbali Tanzania kupotosha wananchi kuwa marekebisho yatafanywa... hata wakienda mpaka kilele cha mlima Kilimanjaro haitasaidia kuzimisha kelele za wananchi ...
Linalotakiwa ni bunge hili hili lirudi haraka ili kwa kikao cha kingine liupitie tena maana ni hitajito la kikatiba wakati kunapotokea hali kama hii tunayoiona badala ya kujaribu kuutetea mkataba huu mbovu ...
Bunge halina uwezo wa kuita watu kuwahoji hata pale walipowatisha kwa kuwaita kina Paschal Mayalla, Dr. Reginald Mengi na wengine ni batili. Kwa bunge haliwezi kuwa prosecutor na mahakama
Kumtishia balozi Dr. Wilbrod Peter Slaa ambaye ni Whistle blower bona-fide kuwa aitwe bungeni ahojiwe kuhusu press conference zake za kuhusu sakata la DP World, hili ni kinyume cha katiba na batili maana bunge halina mamlaka hayo....
Hata mimi Boniface Mwabukusi nikiitwa Dodoma siwezi kutishwa na sitakwenda maana ni wito batili na haramu wala kukidhi sheria na katiba yetu kwa kuwa bunge halina mamlaka hayo
Mikataba ya kunyonya Mali ya asili yetu haikubaliki ni mikataba pekee ambayo ina manufaa kwa taifa na muwekezaji ndiyo tunayoiafiki siyo mkataba mbovu kama huu ...
Tunawashukuru wananchi kwa kupaza sauti katika suala hili ..... maana sasa Bunge halitaweza tena kututia vitanzi kama hivi vya DP World, Loliondo, Madini n.k bila wananchi kuhusishwa kimamilifu na siyo kuburuzwa ....
Kuna masharti yasiyo general policy ndani ya mkataba .... reciprocacy hakuna, huu mkataba una mlinda mwekezaji badala ya kumpa haki ya kudai fidia pale anapodhulumiwa...
High level consultation kwa kutumia katiba yetu Ibara ya 27.1 ya raia kuwa na haki ya kulinda Mali inafanyika na si muda mrefu waTanzania watapewa mrejesho na watafahamishwa
Ibara ya 28 ya katiba hairuhusu mtu yeyote kumilikishwa eneo lolote bali inaruhusiwa kutumika kwa shughuli hivyo mwekezaji hatakiwi kumilikishwa bali kuendesha shughuli za kibiashara ...
Bungeni kulikuwa na tukio na siyo mjadala maana hakuna mwanasheria mkuu hakuoneshwa siku hiyo na mwanasheria mkuu ana kiti chake maalum bungeni lakini hakuwepo na badala yake spika wa bunge kuliteka bunge kinyume na uendeshaji wa bunge huku akiwadhalilisha, kuwa harass wabunge Halima Mdee, Aida Kenani na kulibadilisha bunge kuwa kama darasa la chekechea / kindergarten la a,e,i,o,u huku dhihaka za kutunzana noti, miluzi, kugonga meza kiasi cha bunge kuwa eneo mithili ya ngoma ya mchiriku wakati jambo muhimu la eneo la nchi linamilikishwa kwa taifa lingine geni milele
Ya fuatayo yarekebishwe katika mkataba huu wa DP World katika yafuatayo : Sheria za nchi zizingatiwe masuala ya umilikaji ardhi, umilikaji wa bandari, uvunjwaji wa mikataba, tusikatazwe kutwaa eneo pale usalama wa taifa unapotishiwa tofauti na mkataba huu unavyotukataza kitu ambacho ni kinyume na katiba, spika aache kuligeuza bunge kuwa kikaragosi cha serikali, maandamano yaratibiwe maana katiba inaruhusu
Ushauri kwa Mh. Samia Hassan, ni kuwa mimi nina mashaka rais amepotoshwa maana hata wataalamu kama mwanasheria mkuu hakuonekana ndani ya televisheni siku ya tarehe 10 June 2023 jumamosi mjini Dodoma. Pia namshauri mchakato wa haraka ufanyike Serikali iurudishe mkataba huu tena bungeni na utaratibu wote utumike kikamilifu na uwazi mkubwa kusuka upya mkataba huu tata.
Freeman A. Mbowe ameeleweka na watu wenye uwezo wa kufikiri ila kuna watu wanataka kupotosha ujumbe mzuri aliowakilisha
Ni nchi mbili tu yaani Palestina kule mashariki ya kati na Tanganyika hapa Afrika Mashariki nchi zao zimepotezwa .....
Rais amwelekeze waziri aliyemkasimisha madaraka (Delegata potestas non potest delegari) kujiuzulu maana alimuamini waziri hakutumia imani hiyo vizuri lakini sasa amemuingiza katika matatizi makubwa na pia mkataba huu urejeshwe bungeni tena maana paka akifungiwa chumbani katika kona paka huyu huweza kujigeuza Simba... pia Spika Tulia Ackson ajiuzuli nafasi yake mara moja ya uspika kwa kushindwa kulipa bunge na wabunge nafasi ya kuishauri serikali kwa uwazi hilo linawezekana maana Job Ndugai alijiuzulu kufuatia utata ... na kadhia hii ya bandari ni moto kuliko ya Job Ndugai spika aliyepita ..
Wazee wa taifa wajitokeze haraka kumshauri rais kwa heshima kuwa kuwa wajisahihishe kuurejesha mkataba huu tena bungeni ....
Habari zaidi, soma: