What??umesoma Sheria ?Una level gani ya Elimu.Hakuna unacho kijua rudi Shule tenaKukiuka taratibu za kumkamata mtuhumiwa au kukiuka taratibu za matumizi ya fedha za Umma hakuondoi hatia ya mshtakiwa
What??umesoma Sheria ?Una level gani ya Elimu.Hakuna unacho kijua rudi Shule tenaKukiuka taratibu za kumkamata mtuhumiwa au kukiuka taratibu za matumizi ya fedha za Umma hakuondoi hatia ya mshtakiwa
Kabla ya kumkagua mtuhumiwa wewe Askari ulikaguliwa na nani?Maswali ya kibatala yameonekana kumshushia hadhi ya uelewa Inspekta Mahita na kumpa umaarufu kibatala lakini kikhalisia hayana msaada wa kuwaondolea hatia watuhumiwa
Kuna udhalikishaji gani hapo?#WakiliWaJamhuri: Objection Mheshimiwa Jaji. Tunaomba maswali ya Kibatala yazingatie utu na kuacha udhalilishaji.
Narudia tena !Hutumii akili wa Elimu unatumia mihemuko .Rudi darasaniMaswali ya kibatala yameonekana kumshushia hadhi ya uelewa Inspekta Mahita na kumpa umaarufu kibatala lakini kikhalisia hayana msaada wa kuwaondolea hatia watuhumiwa
AMEN, AMENView attachment 1942798
Hii kesi watoto na wajukuu zetu wataisoma na kuelewa tuliyopitia.
Daaaah masikini 😂😂😂😂 hapo ni toa gambe weka gambe hakuna kuomba pooWakili msomi Peter Kibatala V/S Mtoto wa IGP Mahita.
KIBATALA: Inspekta Mahita nimekufuatilia wewe ndiye ulikuwa arresting Officer?
MAHITA: Sahihi.
KIBATALA: Kazi ya Kingai ilikuwa nini?
MAHITA: Alikua Mkuu wa Msafara.
KIBATALA: Mkuu wa msafara ni role gani kwenye arresting?
MAHITA: Kimya.
KIBATALA: Adamoo pale Bomang'ombe alikula Chakula gani?
MAHITA: Wote walikula.
KIBATALA: Sitaki kujua wote. Nakuuliza Adamoo alikula nini?
MAHITA: Alikula Nyama Choma na Mo Energy.
KIBATALA: Nani alilipia?
MAHITA: Afande Kingai.
KIBATALA: Kwahiyo polisi mlikamata gaidi mkamnunulia nyama choma na ndizi? Mkampa na Mo Energy ya kushushia?
MAHITA: Kimya
KIBATALA: Na wengine mlikula pia?
MAHITA: Ndio
KIBATALA: Nani alilipia vyakula vyenu?
MAHITA: Afande Kingai.
KIBATALA: Siku zote mlizokua Hotel Dar alilipia nani?
MAHITA: Afande Kingai.
KIBATALA: Umewahi kushiriki zoezi la Retirement za Pesa alizotumia Kingai?
MAHITA: Hapana.
KIBATALA: Umewahi kumkabidhi Afande Kingai risiti za matumizi yako ili aweze kufanya retirement?
MAHITA: Hapana.
KIBATALA: Kwahiyo Kingai alitumia pesa za umma bila kuzitolea maelezo wala ripoti.
MAHITA: Siwezi kumsemea.
KIBATALA: Je unafahamu kuwa katika PGO namba 236 (3)ix unapomkamata mtuhumiwa unapaswa ujitambulishe wewe binafsi?
JAJI: Mpatie PGO.
KIBATALA: Ngoja nimepelekee.
MAHITA: Mheshimiwa Jaji, Wakili Kibatala ananionyesha kitu kingine.
JAJI: Muonyeshe taratibu, mtakuwa mmeshamchanganya.
KIBATALA: Mheshimiwa Jaji ngoja nimsomee (ananza kusoma)
MAHITA (anapaza sauti): Mheshimiwa Jaji, Wakili Kibatala anasoma vitu tofauti.
JAJI: Shahidi hebu tulia. Unafikiri mimi sitasoma hiyo PGO?
KIBATALA: Je ulipomkamata Adamoo ulitamka maneno yaliyoandikwa kwenye PGO?
MAHITA: Hapana.
KIBATALA: PGO 236(3) sehemu ya 10 inataka urekodi jibu la Adamoo katika Notebook yako. Je ulifanya hivyo?
MAHITA: Mheshimiwa Jaji, Kibatala anaongea vitu tofauti na PGO, nataka kumsaidia kidogo.
JAJI: Hiyo siyo kazi yako.
KIBATALA: soma hapa kwenye PGO
MAHITA: (anasoma).
KIBATALA: je ni sahihi kuwa Misingi yote inayoainishwa katika PGO kuhusu ukamataji lazima ifuatwe kwa kunyooka kama RULA?
MAHITA: Ni sahihi.
KIBATALA: Unafahamu kuwa unakuja kutoa ushahidi kuhusu statement ya Dama Kasekwa?
MAHITA: Sifahamu.
KIBATALA: Okay. Sasa, mwambie Jaji kwamba hujui kama ulikuja kutoa ushahidi kwenye Kesi ndogo katika kesi ya msingi kuhusu Adamoo.
MAHITA: Hilo sifahamu.
KIBATALA: Kumbe tupo na shahidi ambaye hajui amekuja kufanya nini Mahakamani?
#WakiliWaJamhuri: Objection Mheshimiwa Jaji. Tunaomba maswali ya Kibatala yazingatie utu na kuacha udhalilishaji.
JAJI: Naomba tuzingatie utu.
KIBATALA: Naomba unisomee hapa katika PGO kuhusu Notebook.
MAHITA: Nadhani tafsiri ya PGO hainilazimishi kukumbuka kila kitu Mahakamani.
KIBATALA: Sihitaji tafsiri yako, nimekwambia soma.
MAHITA: Anashindwa kusoma.
Jaji anaingilia kati na kusema "naona Mmechoka, natoa mapumziko tutarudi baada ya nusu saa"
Malisa GJ
View attachment 1942769
Unasoma home kuingia kwenye chumba cha mtihani unakutana na swali la topic ambayo hujasoma.Kile alichokalilishwa ni tofauti kabisa na anachoulizwa
Tena mnakula na nyama choma na mo energy, gaidi angeweza kuagiza hata bia magaidi wa kitanzania wako peace sanaUnamkamata mtuhumiwa wa ugaidi kisha unatembea naye ili akusaidie kutafuta gaidi mwingine
Tz sihami.
KATIBA BORA yajaKesi ya Zuma polisi walijichelewewsha muda wa kuingia mahakamani Jaji aliwapa onyo wakifanya siku ingine hivyo wataenda ndani..bongo polisi wanaanzisha sheria zao eti simu marufuku na wanaendelea kujadili Jaji anawasikiliza watu wasiojua kitu...
Ni kweli kabisa, walicho bakiza ni kumwinda na kumtungua vilevile kama kwa Lissu. Watz tusichoke kumfanyia maombi kwa MunguIvi kibatala ana ulinzi kweli? Maana sio kwa za uzo anazo ipiga sirikale hii mara kwa mara jamaa huwa anawa nyoosha sana
Wewe kichwani hamna kitu kabisa, pengine aheri hata ya huyo shahidi. Unaelewa kuwa hii ni kesi ndogo ndani ya kesi kubwa? Unaelewa hii kesi ndogo ni kwaajili ya kitu gani?Kukiuka taratibu za kumkamata mtuhumiwa au kukiuka taratibu za matumizi ya fedha za Umma hakuondoi hatia ya mshtakiwa
Mkuu kule SA kila MIHIMILI inajitegemea na kila muhimili upo kwenye mji wake. Na kila mmoja unafanya shughuli zake kwa MUJIBU wa KATIBA iliyo tengeneza Sheria zao. Hakuna alie JUU YA KATIBA.Kesi ya Zuma polisi walijichelewewsha muda wa kuingia mahakamani Jaji aliwapa onyo wakifanya siku ingine hivyo wataenda ndani..bongo polisi wanaanzisha sheria zao eti simu marufuku na wanaendelea kujadili Jaji anawasikiliza watu wasiojua kitu...
😆😂🤣KIBATALA: Kwahiyo polisi mlikamata gaidi mkamnunulia nyama choma na ndizi? Mkampa na Mo Energy ya kushushia?
Hivi unaelewa hata kesi ipo kwenye hatua gani hadi uanze kuzungumzia hatia?Kukiuka taratibu za kumkamata mtuhumiwa au kukiuka taratibu za matumizi ya fedha za Umma hakuondoi hatia ya mshtakiwa