Wakili Msomi Peter Kibatala alivyomkaanga mtoto wa IGP Mahita kwenye kesi ya Mbowe

Wakili msomi Peter Kibatala V/S Mtoto wa IGP Mahita.

KIBATALA: Inspekta Mahita nimekufuatilia wewe ndiye ulikuwa arresting Officer?

MAHITA: Sahihi.

KIBATALA: Kazi ya Kingai ilikuwa nini?

MAHITA: Alikua Mkuu wa Msafara.

KIBATALA: Mkuu wa msafara ni role gani kwenye arresting?

MAHITA: Kimya.

KIBATALA: Adamoo pale Bomang'ombe alikula Chakula gani?

MAHITA: Wote walikula.

KIBATALA: Sitaki kujua wote. Nakuuliza Adamoo alikula nini?

MAHITA: Alikula Nyama Choma na Mo Energy.

KIBATALA: Nani alilipia?

MAHITA: Afande Kingai.

KIBATALA: Kwahiyo polisi mlikamata gaidi mkamnunulia nyama choma na ndizi? Mkampa na Mo Energy ya kushushia?

MAHITA: Kimya

KIBATALA: Na wengine mlikula pia?

MAHITA: Ndio

KIBATALA: Nani alilipia vyakula vyenu?

MAHITA: Afande Kingai.

KIBATALA: Siku zote mlizokua Hotel Dar alilipia nani?

MAHITA: Afande Kingai.

KIBATALA: Umewahi kushiriki zoezi la Retirement za Pesa alizotumia Kingai?

MAHITA: Hapana.

KIBATALA: Umewahi kumkabidhi Afande Kingai risiti za matumizi yako ili aweze kufanya retirement?

MAHITA: Hapana.

KIBATALA: Kwahiyo Kingai alitumia pesa za umma bila kuzitolea maelezo wala ripoti.

MAHITA: Siwezi kumsemea.

KIBATALA: Je unafahamu kuwa katika PGO namba 236 (3)ix unapomkamata mtuhumiwa unapaswa ujitambulishe wewe binafsi?

JAJI: Mpatie PGO.

KIBATALA: Ngoja nimepelekee.

MAHITA: Mheshimiwa Jaji, Wakili Kibatala ananionyesha kitu kingine.

JAJI: Muonyeshe taratibu, mtakuwa mmeshamchanganya.

KIBATALA: Mheshimiwa Jaji ngoja nimsomee (ananza kusoma)

MAHITA (anapaza sauti): Mheshimiwa Jaji, Wakili Kibatala anasoma vitu tofauti.

JAJI: Shahidi hebu tulia. Unafikiri mimi sitasoma hiyo PGO?

KIBATALA: Je ulipomkamata Adamoo ulitamka maneno yaliyoandikwa kwenye PGO?

MAHITA: Hapana.

KIBATALA: PGO 236(3) sehemu ya 10 inataka urekodi jibu la Adamoo katika Notebook yako. Je ulifanya hivyo?

MAHITA: Mheshimiwa Jaji, Kibatala anaongea vitu tofauti na PGO, nataka kumsaidia kidogo.

JAJI: Hiyo siyo kazi yako.

KIBATALA: soma hapa kwenye PGO

MAHITA: (anasoma).

KIBATALA: je ni sahihi kuwa Misingi yote inayoainishwa katika PGO kuhusu ukamataji lazima ifuatwe kwa kunyooka kama RULA?

MAHITA: Ni sahihi.

KIBATALA: Unafahamu kuwa unakuja kutoa ushahidi kuhusu statement ya Dama Kasekwa?

MAHITA: Sifahamu.

KIBATALA: Okay. Sasa, mwambie Jaji kwamba hujui kama ulikuja kutoa ushahidi kwenye Kesi ndogo katika kesi ya msingi kuhusu Adamoo.

MAHITA: Hilo sifahamu.

KIBATALA: Kumbe tupo na shahidi ambaye hajui amekuja kufanya nini Mahakamani?

#WakiliWaJamhuri: Objection Mheshimiwa Jaji. Tunaomba maswali ya Kibatala yazingatie utu na kuacha udhalilishaji.

JAJI: Naomba tuzingatie utu.

KIBATALA: Naomba unisomee hapa katika PGO kuhusu Notebook.

MAHITA: Nadhani tafsiri ya PGO hainilazimishi kukumbuka kila kitu Mahakamani.

KIBATALA: Sihitaji tafsiri yako, nimekwambia soma.

MAHITA: Anashindwa kusoma.

Jaji anaingilia kati na kusema "naona Mmechoka, natoa mapumziko tutarudi baada ya nusu saa"

Malisa GJ

View attachment 1942769
Haki husimama na itakuwa labda Kwa udharimu
 
Kimsingi PGO inawatesa sana maana Huwa hawaifuati. Wanachofanya ni ubabe na udharirishaji . Hapo ndipo wanapigwa na Mawakili walishajua udhaifu WAO. Wapigwe tuuuu
 
Wamezoea kuwabambikia kesi watu wasio na msaada wa mawakili thabiti lakini sasa wanaumbuka kwa ushetani wao
Na hao ndio walinzi wetu ambao vichwani yaliyomo ndo kama hayo. Nchi hii tuna matatizo mengi sana
 
KIBATALA: Unafahamu kuwa unakuja kutoa ushahidi kuhusu statement ya Dama Kasekwa?

MAHITA: Sifahamu.

KIBATALA: Okay. Sasa, mwambie Jaji kwamba hujui kama ulikuja kutoa ushahidi kwenye Kesi ndogo katika kesi ya msingi kuhusu Adamoo.

MAHITA: Hilo sifahamu.

KIBATALA: Kumbe tupo na shahidi ambaye hajui amekuja kufanya nini Mahakamani?
Nchi imekua ya kisengerema sana hii..
Mnatesa watu kwa kuwa tu CCM haiwezi kushindana kisiasa na CHADEMA.

Mammae zako mwanasesere wa Polepole.

Mheshimiwa Mbowe sio GAIDI aachiwe huru na tume huru ni lazima
 
Hivi Kodi zetu ndiyo zinamlipa mshahara na lesheni huyu mahita,Kama ndivyo basi Ni matumizi mabovu ya Kodi zetu.hatuwezi kuwa na mtumishi wa umma mpumbavu kiasi hiki.kama huwezi kuwa shahidi feki kwa Nini ukubali kutoa ushahidi.
 
🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣 #WakiliWaJamhuri: Objection Mheshimiwa Jaji. Tunaomba maswali ya Kibatala yazingatie utu na kuacha udhalilishaji.
Dah,ndo nimejua leo kumbe ukiulizwa swali likakushinda kujibu unakuwa umeondolewa utu,
najiuliza utu wa mtu si ni pamoja na kujibu ulichoulizwa?
 
  • Nzuri
Reactions: BAK
Hakuna upumbavu nisiotaka kusikia eti wakili msomi.
Wtf nyie madebe mnatuaminisha.kuna wakili hajazama darasani?Kina Masha,Magai ,Imma hawa wakongwe na mkono wamepiga kazi haswa ya sheria
 
Kwanza walikaa vutuoni zaidi ya saa 48 pasipo kuwafikisha mahakamani, Polisiccm wanaenda kuumbuka waache kutumika na CCM kuwabambikia kesi wapinzani
Ccm wameshindwa hoja wanahisi yule kuhan wao bado yupo hai
 
Back
Top Bottom