Mazhuly
Member
- Aug 12, 2018
- 17
- 5
Haki husimama na itakuwa labda Kwa udharimuWakili msomi Peter Kibatala V/S Mtoto wa IGP Mahita.
KIBATALA: Inspekta Mahita nimekufuatilia wewe ndiye ulikuwa arresting Officer?
MAHITA: Sahihi.
KIBATALA: Kazi ya Kingai ilikuwa nini?
MAHITA: Alikua Mkuu wa Msafara.
KIBATALA: Mkuu wa msafara ni role gani kwenye arresting?
MAHITA: Kimya.
KIBATALA: Adamoo pale Bomang'ombe alikula Chakula gani?
MAHITA: Wote walikula.
KIBATALA: Sitaki kujua wote. Nakuuliza Adamoo alikula nini?
MAHITA: Alikula Nyama Choma na Mo Energy.
KIBATALA: Nani alilipia?
MAHITA: Afande Kingai.
KIBATALA: Kwahiyo polisi mlikamata gaidi mkamnunulia nyama choma na ndizi? Mkampa na Mo Energy ya kushushia?
MAHITA: Kimya
KIBATALA: Na wengine mlikula pia?
MAHITA: Ndio
KIBATALA: Nani alilipia vyakula vyenu?
MAHITA: Afande Kingai.
KIBATALA: Siku zote mlizokua Hotel Dar alilipia nani?
MAHITA: Afande Kingai.
KIBATALA: Umewahi kushiriki zoezi la Retirement za Pesa alizotumia Kingai?
MAHITA: Hapana.
KIBATALA: Umewahi kumkabidhi Afande Kingai risiti za matumizi yako ili aweze kufanya retirement?
MAHITA: Hapana.
KIBATALA: Kwahiyo Kingai alitumia pesa za umma bila kuzitolea maelezo wala ripoti.
MAHITA: Siwezi kumsemea.
KIBATALA: Je unafahamu kuwa katika PGO namba 236 (3)ix unapomkamata mtuhumiwa unapaswa ujitambulishe wewe binafsi?
JAJI: Mpatie PGO.
KIBATALA: Ngoja nimepelekee.
MAHITA: Mheshimiwa Jaji, Wakili Kibatala ananionyesha kitu kingine.
JAJI: Muonyeshe taratibu, mtakuwa mmeshamchanganya.
KIBATALA: Mheshimiwa Jaji ngoja nimsomee (ananza kusoma)
MAHITA (anapaza sauti): Mheshimiwa Jaji, Wakili Kibatala anasoma vitu tofauti.
JAJI: Shahidi hebu tulia. Unafikiri mimi sitasoma hiyo PGO?
KIBATALA: Je ulipomkamata Adamoo ulitamka maneno yaliyoandikwa kwenye PGO?
MAHITA: Hapana.
KIBATALA: PGO 236(3) sehemu ya 10 inataka urekodi jibu la Adamoo katika Notebook yako. Je ulifanya hivyo?
MAHITA: Mheshimiwa Jaji, Kibatala anaongea vitu tofauti na PGO, nataka kumsaidia kidogo.
JAJI: Hiyo siyo kazi yako.
KIBATALA: soma hapa kwenye PGO
MAHITA: (anasoma).
KIBATALA: je ni sahihi kuwa Misingi yote inayoainishwa katika PGO kuhusu ukamataji lazima ifuatwe kwa kunyooka kama RULA?
MAHITA: Ni sahihi.
KIBATALA: Unafahamu kuwa unakuja kutoa ushahidi kuhusu statement ya Dama Kasekwa?
MAHITA: Sifahamu.
KIBATALA: Okay. Sasa, mwambie Jaji kwamba hujui kama ulikuja kutoa ushahidi kwenye Kesi ndogo katika kesi ya msingi kuhusu Adamoo.
MAHITA: Hilo sifahamu.
KIBATALA: Kumbe tupo na shahidi ambaye hajui amekuja kufanya nini Mahakamani?
#WakiliWaJamhuri: Objection Mheshimiwa Jaji. Tunaomba maswali ya Kibatala yazingatie utu na kuacha udhalilishaji.
JAJI: Naomba tuzingatie utu.
KIBATALA: Naomba unisomee hapa katika PGO kuhusu Notebook.
MAHITA: Nadhani tafsiri ya PGO hainilazimishi kukumbuka kila kitu Mahakamani.
KIBATALA: Sihitaji tafsiri yako, nimekwambia soma.
MAHITA: Anashindwa kusoma.
Jaji anaingilia kati na kusema "naona Mmechoka, natoa mapumziko tutarudi baada ya nusu saa"
Malisa GJ
View attachment 1942769