Wakili Albert Msando akatwa katwa mapanga Dar

Wakili Albert Msando akatwa katwa mapanga Dar

Nadhan huu ndiyo wakati muafaka wa kuzishusha AK 47 toka darin na kuanza kutembea nazo, ni kujilinda wenyewe kwa kwenda mbele maana policcm wako busy na CDM
 
Polee sana Albert Msando nakuombea upone haraka mkuu, huu ndyo wizi ulioingia sasa hivi ndugu yangu nae alifanyiwa hivi hivi kibaya zaidi walichukua hadi gari baada ya wiki na msako mkali tulikuja ipata maeneo ya bunju pembeni ya mti wameigongesha.
 
simu yako itapatikana ukiongea na kamanda SIRRO! siku hz mambo ya IMEI number tu! utawashka wote waliokukata panga
 
Je hii ni mbinu mpya ya uporaji au alilengwa kwa sababu zingine?!!!
Ilinikumba wiki mbili zilizopita natoka Ubungo naenda Buguruni, bahati zuri gari yangu ina tinted kali hivyo hawakugundua kama nyuma kuna watu.

Nilishangaa mtu sijamgonga sijapishana nae ila anaongozana na mimi anadai nimemgonga. Niliposimama jamaa zangu walokaa nyuma waliposhuka kusikiliza kesi jamaa nahisi wakaogopa wakakimbia!

Kwa wakati ule sikuelewa ni nini ila kwa ishu hii ndo nimepata picha ya kilichokuwa kinapangwa
 
Kumbe kisoma sana sio ndio kuelimika sasa wakili msomi kabisa pengine ana phd amewasaidia majambazi kumpora kisha analalamika huo ni uzembe wake kwanza inabidi achunguzwe na akikutwa alipanga huo mchezo ashitakiwe
Umelielewa tukio lakini?? Hivi ungekuwa wewe ungefanya nini??
 
  • Thanks
Reactions: bht
Mashambulizi ya mitego kama haya yamekuwepo sana hata kabla ya utawala huu ulipo, kuyahusisha na siasa itakuwa ni kujidanganya
 
Nampa pole ndugu Albert, huu ni dhahiri ujambazi wa aina mpya kabisa. Tumepata fundisho, mtu akijaribu kukusimamisha na kavaa vizuri , usikubali mwambie tuongozane mpaka kituo cha polisi karibu na hapo. Na mwambie chukua nbr ya gari kama anafikiri utakimbia.

Kwa wale wapendao kuzusha mambo na kuwachonganisha watanzania haya fursa hiyo, njooni muitumie kujenga hoja zenu za kinafiki
Huu wala sio aina mpya ya ujambazi. Mwanzoni mwa miaka ya 1990 jijini Dar es Salaam, jamaa walimfuatilia bwana mmoja, bila yeye kujua, aliyetoka kuchukua fedha (nyingi?) benki, alipoingia kwenye gari lake na kuondoka wao wakawa wanamfuatilia kwa nyuma, walikuwa wamepiga suti za kufa mtu! Alipotoka katikati ya jiji na kuelekea barabara inayopita Surrender Bridge wakaongeza spidi kidogo ili wamkaribie zaidi kisha wakagonga gari kwa nyuma, akasimamisha gari ili kuangalia namna gari lake lilivyoharibika. Wale jamaa nao wakatoka kwenye gari na suti zao wakionekana watanashati wakamwomba samahani na wakamwambia kuwa hakuna sababu ya kusubiri trafiki watawasumbua, hivyo aongozane nao kuelekea Kinondoni ambako walimwambia wana gereji yao watatengeneza gari lake na kumpoza kidogo. Akawakubalia.

Bahati nzuri kuna askari wa upelelezi walikuwa wamezishtukia zile njemba zenye suti tangu katikati ya jiji hivyo nao walikuwa wakifuatilia, na kitendo cha kugonga ile gari ya yule jamaa wakazidi kuhisi kuna kitu kitatokea. Walichofanya wale askari wakawasiliana na trafiki wa Surrender Bridge ili zile gari (ya yule jamaa aliyetoka benki na ile ya watanashati wenye suti) wazipige mkono zipaki pembeni. Na kweli, baada ya kukaribia Surrender Bridge gari hizo zikaamriwa na trafiki zipaki pembeni. Kilichotokea wale watanashati machale yaliwacheza na ghafla wakaona gari la polisi linakuja kasi eneo lile. Ni hapo eneo hilo lilipogeuka uwanja wa vita ghafla, maana wale watanashati ndio walianza kurusha risasi kuelekea kwa wale askari ili wapate upenyo wa kutoroka. Wakati hayo yakitokea yule jamaa ambaye gari lake liligongwa aliduwaa asijue kinachoendelea mpaka pale askari walipomzindua kuwa alikuwa anaenda kulizwa! Umakini unatakiwa na tusiamini watu kirahisi rahisi!
 
[HASHTAG]#Justice4Lema[/HASHTAG]
[HASHTAG]#FreeMaxenceMello[/HASHTAG]
[HASHTAG]#BBBenAlive[/HASHTAG]
[HASHTAG]#GetwellsoonMsandoAlbert[/HASHTAG]
[HASHTAG]#SayNO2dictatorialregime[/HASHTAG]
 
Mkuu edit hiyo title, hilo neno akatwa katwa, haliendani na habari.
 
Huu wizi umeshamiri Kwa kasi sana maeneo mbalimbali ya jiji na sio lazima use ndani ya gari hata Kwa miguu ikifika SAA 5 usiku kuendelea gari ikikufuatilia na kusimama karibu yako ikwepe. Kuna Shemeji yangu maeneo ya Africans zena kawawa kapigwa mapanga na gari dogo aina ya Toyota Porte ya light blue wamemshukia wakaanza kumcharangan kichwani na mbavuni. Mbezi beach, Mikocheni ,Tegeta, Sinza ,obay Masaki huu wizi umekithiri kuweni waangalifu.

Tunatumaini askari wawe wanasachi magari ya watu usiku kuepusha hili balaa.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom