mama chupaki
JF-Expert Member
- Aug 23, 2015
- 940
- 768
Mbinu mpya za majambazi.
Asante kwa tahadhariMkirindi wala usisimame wala kuwasikiliza nakwambia wee chochea chombo tu mkuu. Kitendo cha kusimama tu umekwisha.
Jumamosi nimetoka zangu mbezi kwenye kwaito ya harusi ya rafiki yangu nikawa nimepakia mtu lifti nikamshusha pale mwenge ila muda mrefu kuanzia pale njia panda ya kawe kuna gari moja hivi ni saloon ilikuwa inanifuata nyuma na ilikuwa imebomoka taa moja niliona taa hiyo tukiwa kwenye taa za pale Lugalo. Ile nafika mataa ya moroco naona lile gari linaniwashia taa za honi nyingi nikajua leo ninalo nikahakikisha tu lock zote ziko vizuri baada ya mataa kuruhusu wakaendelea na honi zao na kuniwashia mataa ya kuniashiria nisimame na vile gari zilikuwa sio nyingi wakawa wanajitahidi kuniovertake na honi wanapiga mfululizo nilikanyaga mafuta huko mbele kote nilikuta green lights sikuwaona tena hadi naingia uswazi kwangu Tandika.
Ilikuwa naibiwa siku hiii na hawa ni wale wanakwambia kuwa umewagonga umewavunjia taa.kuna wanaotembea na pamber linaning'inia kuna waotembea na gari imebonyea upande mmoja yaani huu ni wizi mpya. Tuchukue tahadhari wengi inasemekana wanapark kwenye mabaa na kwenye kumbi za harusi ukitoka tu unao![]()
Ila vituo vya polisi si vinafungwa usiku???? Itakuwaje??Na kweli na km wana kuandama na taa zao za hazard sehemu nzuri ya kusimaa ni kituo cha polisi au sehemu yenye mkusanyiko wa watu wengi nadhani ni suluhisho zuri tumefika pabaya kwa kweli sasa
Hilo nalo nenoHivi kuna wakili anaeruhusiwa kufanya kazi za uwakili lakini asie msomi??
Mara ya kwanza ilinitokea hii kitu, nje ya uwanja wa taifa kwenye mechi ya Tanzania vs Cameroon.. Daaah jamaa akawa analalamika nimemkanyaga, nikawa namwambia pole akaniachia, ile kupiga hatua moja tu nasikia simu yangu haipp mfukoni. Nikageuka nikakuta wanapeana ile simu nikamshika anirudishie simu akarudisha kwa aibu. WATU WA DAR HAWAKUNISAIDIA
Kuanzia siku ile nikawa nimeshajifunza, hivyo mpaka leo mtu akinizingua kwa style hiyo hawezi kunipata.