Johnny Sack
JF-Expert Member
- Jan 21, 2017
- 8,834
- 18,837
Wakili wa mmoja wa watu wanoshtakiwa pamoja na aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Hai, Lengai Ole Sabaya kwa uhujumu uchumi na utakatishaji fedha amejiondoa kumtetea mteja wake.
Wakili Fridoline Bwemelo amesema ameamua kujiondoa kumtetea mshtakiwa wa tatu katika kesi hiyo, Watson Mwahomange kwa kile alichodai kuwepo mgongano wa kimaslahi na kulinda maadili yake.
Bwemelo ameeleza uamuzi huo leo Jumatatu Machi 7, 2022 mbele ya Hakimu mkazi Mwandamizi, Dk Patricia Kisinda.
Alidai kuna mambo ambayo mshitakiwa huyo alimtaka ayaeleze mahakamani lakini akaona asingeweza kufanya hivyo kutokana na maadili yake ya kitaaluma.
”Mimi kwa kiapo changu kama ofisa wa mahakama sikuwa tayari kukieleza hicho ambacho naona kitaende kinyume na maadili yangu kama wakili au ofisa wa mahakama,” amesema.
Chanzo : Mwananchi
====
KESI YA SABAYA: Wakili Fridoline Bwemelo aliyekuwa akimwakilisha mshtakiwa namba tatu, Watson Mwahomange, katika kesi ya uhujumu uchumi na utakatishaji fedha, inayomkabili aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Hai Mkoani Kilimanjaro Lengai Ole Sabaya na wenzake sita, amejiondoa kumwakilisha mshtakiwa huyo kwa kile alichodai kuwa ni kutokana kuwepo kwa mgongano wa kimaslahi kati yake na mteja wake.
#AzamTVUpdates #KesiYaSabaya
Wakili Fridoline Bwemelo amesema ameamua kujiondoa kumtetea mshtakiwa wa tatu katika kesi hiyo, Watson Mwahomange kwa kile alichodai kuwepo mgongano wa kimaslahi na kulinda maadili yake.
Bwemelo ameeleza uamuzi huo leo Jumatatu Machi 7, 2022 mbele ya Hakimu mkazi Mwandamizi, Dk Patricia Kisinda.
Alidai kuna mambo ambayo mshitakiwa huyo alimtaka ayaeleze mahakamani lakini akaona asingeweza kufanya hivyo kutokana na maadili yake ya kitaaluma.
”Mimi kwa kiapo changu kama ofisa wa mahakama sikuwa tayari kukieleza hicho ambacho naona kitaende kinyume na maadili yangu kama wakili au ofisa wa mahakama,” amesema.
Chanzo : Mwananchi
====
KESI YA SABAYA: Wakili Fridoline Bwemelo aliyekuwa akimwakilisha mshtakiwa namba tatu, Watson Mwahomange, katika kesi ya uhujumu uchumi na utakatishaji fedha, inayomkabili aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Hai Mkoani Kilimanjaro Lengai Ole Sabaya na wenzake sita, amejiondoa kumwakilisha mshtakiwa huyo kwa kile alichodai kuwa ni kutokana kuwepo kwa mgongano wa kimaslahi kati yake na mteja wake.
#AzamTVUpdates #KesiYaSabaya