Sabaya afanyiwa upasuaji, kesi yaahirishwa

peno hasegawa

JF-Expert Member
Feb 24, 2016
12,767
21,323
Mawakili wa upande wa utetezi kesi namba mbili ya mwaka 2022, inayomkabili aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Hai, Lengai Ole Sabaya na wenzake wanne wameieleza mahakama ya Hakimu Mkazi Moshi kuwa hali ya Sabaya ni mbaya baada ya kufanyiwa upasuaji mkubwa wa kichwa Julai 27 mwaka huu.

By Maryasumta Eusebi

Moshi.
Mawakili wa upande wa utetezi kesi namba mbili ya mwaka 2022, inayomkabili aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Hai, Lengai Ole Sabaya na wenzake wanne wameieleza mahakama ya Hakimu Mkazi Moshi kuwa hali ya Sabaya ni mbaya baada ya kufanyiwa upasuaji mkubwa wa kichwa Julai 27 mwaka huu.

Sabaya na wenzake wanne wanakabiliwa na mashtaka saba likiwamo la uhujumu uchumi na matumizi mabaya ya ofisi wakati akiwa Mkuu wa wilaya hiyo.

Juni Mosi mwaka huu, Sabaya na wenzake wanne walipandishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Moshi na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) na kusomewa mashtaka yanayowakabili mbele ya hakimu mkazi Mfawidhi, Salome Mshasha.

Washitakiwa wengine katika kesi hiyo ni Sylvester Nyegu, John Aweyo, Nathan Msuya na Antero Assey.

Hata hivyo Sabaya ambaye ni mshtakiwa namba moja katika kesi hiyo alifikishwa mahakamani hapo leo kichwa chake kikiwa kimeviringishwa bandeji huku mkononi akiwa na kifaa cha kuchomekea dripu.

Awali wakili wa Sabaya, Fridolin Bwemelo aliieleza mahakama hiyo kuwa Sabaya amefanyiwa upasuaji mkubwa wa kichwa kutokana na uvimbe aliokuwa nao na kwamba anahitaji kupata uangalizi wa karibu.

"Sabaya amefanyiwa upasuaji mkubwa wa kichwa na sio upasuaji mdogo hivyo anahitaji apate huduma muhimu na uangalizi wa karibu,"

Wakamtaka mwendesha mashtaka wa kesi hiyo kuharakisha upelelezi wa kesi hiyo kwa kuwa walishaieleza mahakama hiyo kuwa upelelezi umekamilika.

Wakili upande wa mashtaka Sabitina Mcharo aliieleza mahakama hiyo kuwa upelelezi bado haujakamilika na kwamba wanasubiri kibali kutoka kwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali cha kuipa uwezo mahakama hiyo kuendelea kuisikiliza kesi hiyo.

Hata hivyo, Hakimu mkazi wa mahakama hiyo aliyekuwepo, Elibariki Philly aliahirisha kesi hiyo mpaka Agosti 12 mwaka huu.

Chanzo: Mwananchi
 
 
"General" nonsense.

Huo upasuaji wa kichwa alienda kufanyiwa kwa amri ya mahakama iliyotolewa lini? au inawezekana gerezani wakatoa ruhusa bila kuwasiliana na mahakama?
 
Bora apitilize.
Aliua wengi
Ni kweli aliwahudhi na kuwatesa wengi, kwa mapito anayopitia anaweza kutusaidia kiwaambia vijana wengine wakipata mmadaraka wawe watu wema, atakuwa mshuhudiaaji mzuri.Tunamwombea aishi, apewe nafasi na Mungu maana akifa mapito yake hayatakuwa funzo kwa wajinga wajao.
 
Mawakili wa upande wa utetezi kesi namba mbili ya mwaka 2022, inayomkabili aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Hai, Lengai Ole Sabaya na wenzake wanne wameieleza mahakama ya Hakimu Mkazi Moshi kuwa hali ya Sabaya ni mbaya baada ya kufanyiwa upasuaji mkubwa wa kichwa Julai 27 mwaka huu.

By Maryasumta Eusebi

Moshi.
Mawakili wa upande wa utetezi kesi namba mbili ya mwaka 2022, inayomkabili aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Hai, Lengai Ole Sabaya na wenzake wanne wameieleza mahakama ya Hakimu Mkazi Moshi kuwa hali ya Sabaya ni mbaya baada ya kufanyiwa upasuaji mkubwa wa kichwa Julai 27 mwaka huu.

Sabaya na wenzake wanne wanakabiliwa na mashtaka saba likiwamo la uhujumu uchumi na matumizi mabaya ya ofisi wakati akiwa Mkuu wa wilaya hiyo.

Juni Mosi mwaka huu, Sabaya na wenzake wanne walipandishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Moshi na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) na kusomewa mashtaka yanayowakabili mbele ya hakimu mkazi Mfawidhi, Salome Mshasha.

Washitakiwa wengine katika kesi hiyo ni Sylvester Nyegu, John Aweyo, Nathan Msuya na Antero Assey.

Hata hivyo Sabaya ambaye ni mshtakiwa namba moja katika kesi hiyo alifikishwa mahakamani hapo leo kichwa chake kikiwa kimeviringishwa bandeji huku mkononi akiwa na kifaa cha kuchomekea dripu.

Awali wakili wa Sabaya, Fridolin Bwemelo aliieleza mahakama hiyo kuwa Sabaya amefanyiwa upasuaji mkubwa wa kichwa kutokana na uvimbe aliokuwa nao na kwamba anahitaji kupata uangalizi wa karibu.

"Sabaya amefanyiwa upasuaji mkubwa wa kichwa na sio upasuaji mdogo hivyo anahitaji apate huduma muhimu na uangalizi wa karibu,"

Wakamtaka mwendesha mashtaka wa kesi hiyo kuharakisha upelelezi wa kesi hiyo kwa kuwa walishaieleza mahakama hiyo kuwa upelelezi umekamilika.

Wakili upande wa mashtaka Sabitina Mcharo aliieleza mahakama hiyo kuwa upelelezi bado haujakamilika na kwamba wanasubiri kibali kutoka kwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali cha kuipa uwezo mahakama hiyo kuendelea kuisikiliza kesi hiyo.

Hata hivyo Hakimu mkazi wa mahakama hiyo aliyekuwepo, Elibariki Philly aliahirisha kesi hiyo mpaka Agosti 12 mwaka huu.

Chanzo: Mwananchi
Sasa amerudi hospitali au Selo?
 
Ewaaaaaaa wema ni akiba na Ubaya ni akiba
Ana hali mbaya ana kesi ngumu hajaimaliza huku manundu nayo yanachomoza.

DAB anavyochungulia hii kesi sijui anajisikiaje.

Ukishindana na Mbowe utapata ushindi wa muda tu
 
Inawezekana alijaribu kusugua kichwa ukutani au anywhere ili kuharibu nervous akafeli.

Huwa inatumiwa huko majuu zaidi, ikifanikiwa unakufa.

Anyways kuna mazingira unafikia unatamani kifo.
Nimewaza sana huo uvimbe umekujaje ghafal mwanzo tuliona masihara vile.
 
Back
Top Bottom